Posts

BENKI YA CRDB YATOA GAWIO LA SHILINGI BILIONI 36.1 KWA SERIKALI

Image
  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay (wa tatu kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wa pili kushoto) wakikabidhi mfano wa hundi kwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba (katikati) ikiwa ni sehemu Gawio la Serikali lililotolewa na Benki ya CRDB, katika hafla iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Hazina, jijini Dodoma leo Juni 29, 2022. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais - Tamisemi, David Silinde (wa pili kulia), Naibu Waziri wa Kazi, Ajira, Vijana, Patrobas Katambi (kulia) pamoja na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Lawrence Mafuru. Dodoma, 29 Juni, 2022 - Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba amepokea gawio la shilingi bilioni 36.1 linalotokana na uwekezaji wa Serikali ndani ya Benki ya CRDB kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay.    Makabidhiano hayo ya hundi kifani yalifanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha Dodoma na kuhudhuriwa na Naibu Wazi

JENERALI MABEYO AMUAGA AMIRIJESHI MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA, RAIS SAMIA SULUHU HASSAN

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mkuu wa Majeshi ya i nchini (CDF) Jenerali Venance Mabeyo. Jenerali Mabeyo alifika Ikulu Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumuaga Mhe. Rais Samia wakati akimaliza kipindi cha Utumishi wake katika Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania.

RAIS SAMIA ATEUA MKUU MPYA WA MAJESHI

Image
    NA MWANDISHI WETU RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amirijeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mhe. Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo Meja Jenerali Jacob John Mkunda(pichani juu) kuwa Jenerali, kisha kumteua kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (Chief of Defence Forces – CDF). Kabla ya Uteuzi huo alikuwa Mkuu wa Tawi la Operesheni na Mafunzo katika Makao Makuu ya Jeshi (Chief of Operations and Training) na anachukua nafasi ya Jenerali Venance Salvatory Mabeyo ambaye amestaafu kwa mujibu wa sharia. Rais Samia pia amempandisha Cheo Meja Jenerali Salum Haji Othman kuwa Luteni Jenerali na amemteua kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (Chief of Staff – CofS). Kabla ya uteuzi huo Meja Jenerali Othman alikuwa Kamishna wa Utafiti na Maendeleo Jeshini (Commissioner for Research and Military Development) katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Vile vile amemteua Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule kuwa Balozi ambapo kabla ya uteuz

PSSSF YAPOKEA GAWIO LA BILIONI 11.85 KUTOKA CRDB KWENYE UWEKEZAJI WA HISA

Image
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekabidhi gawio lenye thamani ya  Shilingi bilioni 11.85 kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF CPA Hosea Kashimba kwa niaba ya Mfuko, kwenye hafla fupi iliyofanyika leo  jijini Dodoma. Akikabidhi hundi hiyo Mhe. Mchemba  amesema, "nimefurahishwa pia kuona taasisi na mashirika mbalimbali ya Serikali, Halmashauri, pamoja na vyama vya ushirika wanapokea gawio la jumla ya Shilingi bilioni 16.4. Hii inafanya jumla kuu ya gawio tunalolipokea leo kuwa Shilingi bilioni 36.1. Ni jambo la kujivunia sana kwa Benki yetu ya kizalendo". Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA Hosea Kashimb a Mkurugenzi wa Fedha, PSSSF, Bi. Beatrice Musa-Lupi (wakwanza kushoto) akiungana na maafisa wengine kwenye hafla ya kupokea gawio kutoka benki ya CRDB jijini Dodoma Juni 29, 2022.

MAONESHO YA 46 YA SABASABA 2022: NSSF YAWAKARIBISHA WANACHAMA NA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA NAMBA 13 WAPATE HUDUMA

Image
  NA MWANDISHI WETU, SABASABA MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii   (NSSF) unashiriki katika Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam na kuwakaribisha wanachama wake na wananchi kutembelea banda la Ushirikiano namba 13 la Mfuko huo lililoko mtaa wa Mabalozi.  Maonesho hayo yametoa fursa nzuri kwa Mfuko kukutana na wananchama wake ikiwa ni pamoja na kutoa Elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Umma, amesema Aisha Sango, Afisa Uhusiano Mwandamizi, NSSF. "Sisi NSSF tunasema Tunajenga Maisha Yako ya Sasa na Baadaye" karibu tukuhudumie, alisema Bi. Sango. Maonesho hayo yaliyoanza Juni 28, 2022 yamebeba kaulimbiu isemayo “Tanzania Mahali Sahihi Pa Biashara na Uwekezaji.” Afisa Uhusiano Mwandamizi, Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bw. Sebera Fulgence, (kulia), na maafisa wengine wa Mfuko huo, wakiwahudumia wananchama waliotembelea banda la Ushirikiano namba 13 la Mfuko huo Juni 29, 2022. Afisa Matekelezo Mkuu, NSSF, Bi. Asha Salum (kushoto), akimsikliza mwana

PSSSF YAWAKARIBISHA WANACHAMA NA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LAO MAONESHO YA SABASABA

Image
  NA MWANDISHI WETU, SABASABA MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umewaalika wanachama wake na wananchi kwa ujumla kutembeela banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yaliyoanza Juni 28, 2022 kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa. Afisa Uhusuano Mwandamizi wa PSSSF, Bi. Fatma Elhady amesema imekuwa ni fursa nzuri kwa Mfuko kushiriki katika Maonesho hayo ili kuwawezesha Wanachama na wananchi kwa ujumla kupata taarifa za huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko. “Tunawakaribisha sana Wanachama wetu na wananchi kutembelea Banda namba 13 la Ushirikiano lililoko mtaa wa Mabalozi.” Alisema. Kauli mbiu ya Maonesho hayo ni "Tanzania Mahali Sahihi Pa Biashara na Uwekezaji." Afisa wa Kitengo cha Nyaraka, PSSSF, Bw. Gabriel Maro (kushoto), akifafanua jambo kwa Mwanachama wa Mfuko aliyetembelea Banda la Mfuko huo Juni 29, 2022. Katikati ni Afisa Uhusiano Mkuu, PSSSF, Bw. Abdul Njaidi. Afisa Uhusuano na kwa Wanac

Wasanii Tanzania Kufunguliwa Milango Zaidi Soko la Hollywood

Image
  Na Mwandishi Wetu, LA, California Wasanii mbalimbali wa Tanzania hasa wa muziki na filamu wameahidiwa kufunguliwa milango zaidi katika soko na kiwanda kikubwa zaidi duniani cha burudani cha Hollywood nchini Marekani ili kupata mafanikio zaidi katika kazi zao.  Ahadi hiyo imetolewa na mmoja wa watendaji na wawekezaji wa masuala ya sanaa na burudani nchini Marekani, Bw. Tyrone Davis, alipokutana na kufanya mazungumzo ya kina na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kutoka nchini Tanzania, Dkt. Hassan Abbasi, siku ya Jumanne Juni 28, 2022, jijini hapa.  Pamoja na sasa kujikita zaidi katika kampuni za fedha na masuala ya teknolojia nchini Marekani akiwa Mtendaji Mkuu wa taasisi ya Urban Icon na pia Mwenyekiti wa taasisi ya kifedha ya IN CARD, Bw. Davis anabaki kuwa mmoja wa wadau wakubwa wa Hollywood.  Katika miaka yake ya takribani miaka 20 katika kiwanda cha Burudani nchini Marekani, Bw. Davis anaendelea kubaki mmoja wa watu wanaofahamiana na kila mdau muhimu wa Hollywoo

JKCI KUPIMA MAGONJWA YA MOYO, CHANJO YA UVIKO-19 MAONESHO YA SABASABA 2022

Image
 T aasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) inapenda kuwajulisha wananchi kuwa inashiriki maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayofanyika katika Uwanja wa Maonyesho wa Biashara wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere uliopo barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 28/06/2022 hadi tarehe 13/07/2022. Katika maonesho haya JKCI inafanya upimaji wa afya ya moyo kwa watoto na watu wazima. P ia inatoa chanjo ya UVIKO-19 kama kinga ya ugonjwa huu pamoja na kufanya kipimo cha kuchunguza UVIKO -19 (rapid test) kwa wale wanaosumbuliwa na tatizo katika njia ya kupumulia. Taasisi hiyo pia ina wataalamu wa lishe ambao wanatoa elimu ya lishe bora ambayo inawapa wananchi uelewa na  kufuata mtindo bora wa maisha ambao utawasaidia kuepukana na magonjwa ya moyo na kisukari ambayo ni magonjwa yasiyoambukiza na mtu anaweza kuyaepuka kwa kufuata ushauri wa kitaalamu wa lishe.   Kwa wale watakaokutwa na matatizo ya moyo watapatiwa matibabu hii ikiwa ni pamoja na kupewa rufaa ya ku

CDF MABEYO AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA UWANJA WA GOFU, HOTELI YA NYOTA TANO, KITUO CHA MICHEZO IHUMWA DODOMA

Image
  Mkuu wa Majeshi ya ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo,akicheza mchezo wa Gofu kuashiria uzinduzi wa Mradi wa wa Uwanja wa Gofu, Hoteli ya nyota tano na kituo cha michezo katika eneo la Jeshi Ihumwa leo Juni 28,2022 Jijini Dodoma Mkuu wa Majeshi ya ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo,akiweka jiwe la Msingi  ujenzi wa Uwanja wa Gofu, Hoteli ya nyota tano na kituo cha michezo katika eneo la Jeshi Ihumwa leo Juni 28,2022 Jijini Dodoma. Mkuu wa Majeshi ya ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo,akipata maelezo mradi wa ujenzi kutoka kwa Msimamizi wa Mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Gofu, Hotel ya nyota tano na kituo cha michezo Meja Amanzi Mandengula wakati wa hafla ya kuweka jiwe la Msingi katika eneo la Jeshi Ihumwa leo Juni 28,2022 Jijini Dodoma. Mkuu wa Majeshi ya ulinzi nchini Jenerali Venance Mabeyo,akikata utepe kuashiria  ujenzi wa Uwanja wa Gofu, Hoteli ya nyota tano na kituo cha michezo wakati wa hafla ya kuweka jiwe la Msingi katika ujenzi huo eneo la Jeshi Ihumwa leo Juni 28,2