Posts

Showing posts from December, 2023

WAZIRI KAIRUKI AKAGUA UJENZI WA MRADI WA NYUMBA MSOMERA

Image
Asisitiza Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu inalenga kuboresha maisha ya wananchi Na Happiness Shayo Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) amekagua mradi wa ujenzi wa nyumba katika kijiji cha Msomera Wilayani Handeni kwa ajili ya wananchi wanaohama kwa hiari kutoka Ngorongoro kwenda Msomera, ikiwa ni awamu ya pili ya ujenzi wa nyumba hizo. Mhe. Kairuki amefanya ziara hiyo leo Desemba 31,2023 kwa lengo la kuangalia maendeleo ya ujenzi wa nyumba hizo ambapo zoezi la kuwahamishia wananchi Msomera linaendelea. Katika kijiji cha Msomera wilayani Handeni Mkoani Tanga Serikali inajenga nyumba 2500 huku nyumba nyingine 1500 zikitarajiwa kujengwa katika kijiji cha Kitwai B wilayani Simanjiro na nyumba 1000 zitajengwa katika kijiji cha Saunyi wilayani Kilindi na kufanya jumla ya nyumba 5000 kwa mradi wote. “Tulishaendesha zoezi katika awamu ya kwanza kwa ajili ya kuhamisha wananchi kutoka katika eneo la hifadhi ya ngorongoro,tumemaliza vizuri na zaidi ya nyumba 500 ziliweza

KUTOKA MAGAZETINI DESEMBA 31, 2023

Image
 

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MAPINDUZI MKOA WA DAR ES SALAAM NDUGU ABASI MTEMVU ACHANGISHA HARAAMBEE MAALUM KATIKA KANISA LA WAADVENTISTA

Image
Mwenye kiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dsm Ndg. Abas Zuberi Mtemvu Akiongozana na Mnec wa Ccm Mkoa Ndg. Juma Simba Gadafi Pamoja na M/kiti wa Ccm Wilaya ya Kinondoni Ndg. Shaweji Mkumbura,  Wamehudhuria Katika Ibada ya Kanisa la Adentista wa Sabato Yombo Dovya Wilaya ya Temeke, Ambapo M/kiti wa Ccm Mkoa Ndg. Abas Zuberi Mtemvu Amealikwa Katika Kanisa Hilo kwa Lengo la Kufanya Haraambee Maalum ya Kuchangia Ujenzi wa Kanisa Hilo Pamoja na Vifaa vya Kisasa Kwaajiki ya Kwaya Katika Kanisa Hilo,  Katika Haraambee Hiyo M/kiti Alifanikiwa Kuchangisha Fedha Taslim Shilingi Milioni 11,000,000 Na Ahadi Shilingi 9,000,000 Viongozi wa Kanisa la Waadventista wa Sabado Dovya Wamemahukuru Ndg. Abas Mtemvu kwa Kuwa na Moyo wa Kujitolea Pamoja na Kukubali Mualiko wa Kuwa Mgeni Rasmi Katika Haraambee Hiyo.  

UHAMIAJI YATANGAZA NAFASI ZA KAZI

Image
 

DKT. BITEKO AMSHUKU RAIS, DKT. SAMIA KWA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI BUKOMBE

Image
  📌 *Shule mpya 30 za msingi zajengwa* 📌 *Kila Kata wilayani Bukombe sasa ina Shule ya Sekondari* 📌 *Barabara mpya zajengwa, mtandao wafikia kilometa 1400* 📌 *Bukombe sasa ina hospitali mbili, vituo vya afya sita, zahanati 18* 📌 *Apokea Wanachama wapya wa CCM, watokea CHADEMA* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amepongeza jitihada kubwa zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kutekeleza kwa kasi miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Bukombe ikiwemo Barabara, Shule na ujenzi wa zahanati, vituo vya afya na hospitali. Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo sambambabna shukrani wakati akizungumza katika mkutano wa hadhara na  Wananchi wa Kijiji cha Bukombe, Kata ya Bukombe, Wilaya ya Bukombe mkoani Geita, ikiwa ni sehemu ya ziara yake jimboni Bukombe.   Viongozi mbalimbali walihudhuria mkutano huo  wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigella. “Kama kuna mtu

MKURUGENZI CMA AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA UZALENDO NA HAKI KULETA MAENDELEO MWAKA 2024.

Image
 NA MWANDISHI WETU Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Bw. Usekelege Mpulla (pichani) amewataka watumishi wa tume kufanya kazi kwa uzalendo,weledi,uadilifu,na ufanisi pamoja na kuzingatia haki katika kuwahudumia wananchi, ili kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa waajiri na waajiriwa katika kutatua migogoro ya kikazi kwa mwaka 2024. Wito huo umetolewa leo 29 Disemba,2023 katika ofisi za Makao makuu ya tume Mkoani Dodoma, wakati akitoa salamu za mwaka mpya wa 2024 kwa wadau,wafanyakazi,  na wananchi wote, ikiwa ni Pamoja na kuelezea mikakati ya mwaka unaofuata katika kuhakikisha tume inatekeleza majukumu yake na kuongeza utendaji kazi katika kushughulikia migogoro ya kikazi Tanzania Bara. Mpulla ameongeza kwamba, tume imejipanga vyema kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wadau mbalimbali wenye migogoro ya kikazi, na kwakutambua umuhimu wa kuboresha shughuli za tume wameamua kuanza na kikao cha tathmini ya utendaji kazi wa tume ili kuweza kubaini mapungufu na kuboresha utendaj

KUTOKA MAGAZETINI DESEMBA 30, 2023

Image