Posts

Showing posts from February, 2023

MHE. JENISTA AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUTOA USHIRIKIANO WA KIUTENDAJI KWA VIONGOZI WAPYA ILI KUENDELEA KUUBORESHA UTUMISHI WA UMMA

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akizungumza na watumishi wa ofisi yake kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wake Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia) kuzungumza na watumishi hao mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi. Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa pili kutoka kushoto) akipokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake kutoka kwa mtangulizi wake, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa kwanza kulia) mara baada ya Bw. Mkomi kuripoti rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete. Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma aliyemaliza

TANZANIA, BENKI YA DUNIA ZASAINI MKATABA WA MIKOPO NAFUU NA MISAADA YA SHILINGI TRILIONI 1.3

Image
Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam Tanzania na Benki ya Dunia zimetiliana Saini mikataba miwili ya mkopo nafuu na msaada yenye thamani ya dola za Marekani milioni 579.93, sawa na shilingi trilioni 1.332.8, kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ukiwemo mradi wa maji safi na usafi wa mazingira pamoja na mradi wa kuboresha afya ya mama na mtoto. Waliotia Saini mikataba hiyo Jijini Dar es Salaam, ni Waziri wa Fedha na Mpango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bw. Nathan Belete. Dkt. Nchemba alisema kuwa kati ya fedha hizo, dola za Marekani milioni 550 sawa na shilingi za Tanzania trilioni 1.264 ni mkopo wenye masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia na kiasi kingine cha dola za Marekani milioni 29.93 sawa na shilingi bilioni 68.79 ni msaada kutoka Energy Sector Management Assistance Program (ESMAP) na Mfuko wa Global Financing Facility. Dkt. Nchemba alifafanua kuwa Mradi wa Mpango Endelevu wa Maji na Usafi wa Mazingira umetengewa dola za Marekani mili

TANZANIA KUANZA SAFARI ZA NDEGE MOJA KWA MOJA HADI SAUDI ARABIA

Image
  Tanzania inategemea kuanzisha s afari  za ndege za moja kwa moja hadi Saudi Arabia ambapo safari  ya kwanza kati ya Dar es Salaam  na  Jeddah i natarajiwa kuanza  tarehe 26 Machi 2023. Hayo yamebainishwa katika mazungumzo ya Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe.  Ali Mwadini  na  Meneja Mkuu wa Masoko, Kanda ya Kati wa Shirika la Ndege la Saudi Arabia Bw. Abdulrahman Alabdulwahab  na  kujadili maandalizi ya uzinduzi wa safari za ndege za moja kwa moja kati ya Tanzania na Saudi Arabia. Katika mazungumzo yao viongozi hao pia w alijadili mikakati ya kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania ili kuongeza idadi ya watalii na kurahisisha usafirishaji wa bidhaa za Tanzania hususan nyama na matunda.

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE FEB 28, 2023

Image
 

DKT. NCHEMBA ATETA NA MABALOZI WA CANADA NA JAPAN NCHINI.

Image
 Na Benny Mwaipaja, WFM , Dar es Salaam Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba amekutana na kufanya mazungumzo na Mabalozi wawili, Balozi wa Canada na Japan kwa nyakati tofauti ambapo walizungumzia ushirikiano kati ya nchi hizo katika sekta mbalimbali za uzalishaji ikiwemo sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi, na sekta binafsi ili kukuza uchumi. Mazungumzo hayo yamefanya kwenye Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es Salaam. Akizungumza na Balozi wa Canada, Mhe. Kyle Nunas, Dkt. Nchemba aliishukuru Serikali ya Canada kwa kutoa fedha kiasi cha dola ya Canada milioni 87.3 kwa ajili ya Mfuko wa Afya na ahadi mpya ya kutoa dola za Canada milioni 75 katika kipindi cha mwaka 2021 hadi 2026, ambazo amesema zitasaidia kuboresha afya ya jamii. Aidha, Dkt. Nchemba aliipongeza Canada kwa kuahidi kutoa kiasi kingine cha dola za Canada milioni 32 katika mwaka wa fedha 2023/2024 kwa ajili kuendeleza  sekta binafsi ambayo ni muhimu katika maendeleo ya nchi na ni injini

WATUMIAJI HUDUMA NDOGO ZA FEDHA WAASWA KUTUMIA HUDUMA HIYO KWA TAASISI ZILIZOSAJILIWA

Image
  NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID WATUMIAJI wa Huduma ndogo za fedha wameaswa kutotumia huduma kwa mtu au taasisi ambayo haijasajiliwa na Benki Kuu ya Tanzania. Hayo yamesemwa na Kaimu Msimamizi wa Huduma Ndogo za fedha BoT, Bi. Mary Ngasa wakati wa majadiliano baada ya kuwasilisha mada “Usimamizi wa Huduma Ndogo za Fedha, (Microfinance Supervision) ” kwenye semina ya siku moja kwa Wahariri wa vyombo vya habari kuhusu masuala ya Fedha na Uchumi iliyoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) jijini Dar es Salaam Februari 27, 2023. Alisema hadi sasa kuna jumla ya taasisi za watoa huduma ndogo za fedha zinazofikia 1,000 ambazo zimesajiliwa na BoT, Tanzania Bara. Akifafanua alisema “Ibara ya 12 ya Sheria hiyo imeipa mamlaka Benki Kuu ya Tanzania Kusajili, Kusimamia na Kudhibiti biashara ya huduma ndogo za Fedha Tanzania Bara, lengo kuu hasa ni kuwasaidia wananchi kuepuka changamoto za udanganyifu zilizokuwa zikiwakumba kabla ya kuanzishwa kwa sheria.” Alifafanua Alisema Ibara ya 16 ya S