Posts

Showing posts from September, 2021

AFISA MTENDAJI MKUU NFRA AWEKA WAZI UTEKELEZAJI MRADI WA KUONGEZA UWEZO WA UHIFADHI NAFAKA KATIKA MAENEO NANE

Image
Saymon Kobilesky Mhandisi Mjenzi wa Maghala ya Kuhifadhia Chakula mjini Sumbawanga kutoka Kampuni ya Unia Araj Poland akitoa Maelezo kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bw. Bw. Milton Lupa wakati alipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula mjini Mpanda mkoani Katavi  hivi karibuni. Kushoto ni Marwa Range Kaimu Meneja wa NFRA Kanda ya Sumbawanga. Proches Kiwango Fundi Sanifu wa Mradi wa Maghala ya NFRA Mpanda akitoa maelezo kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Bw. Milton Lupa wa pili kutoka kushoto wakati alipokagua mradi huo unaotekelezwa na Kampuni ya Unia Araj Poland hivi karibuni, kushoto ni Marwa Range Kaimu Meneja wa NFRA Kanda ya Sumbawanga na Katikati ni Bw. Hudson Kamoga Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Kilimo Muonekano wa mradi wa ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula Mpanda mkoani Katavi. Proches Kiwango Fundi Sanifu wa Mradi wa Maghala ya NFRA

BALOZI MASHIBA AWATOA HOFU MADEREVA WA TANZANIA HUKO MALAWI

Image
 Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Benedict Mashiba amewatoa hofu Watanzania kuwa Madereva wa Malori wa Tanzania wapo salama licha ya kulengwa na wenzao wa Malawi. Kwa mujibu wa Balozi Mashiba, visa vya kushambuliwa kwa Malori yanayoe deshwa na Madereva wa Tanzania nchini Malawi vilianza Jumatatu Septemba 27, 2021 ambapo Madereva wa Malori wa Nchini Malawi waliitisha mgomo wakidai maslahi Bora kutoka kwa waajiri wao. Taarifa za vyombo vya habari zikinukuu vyanzo mbalimbali kutoka nchini Malawi vilisema, Madereva wa Malawi waliamuru Malori yote ya mizigo kuegeshwa na yasiobekane barabarani Hadi hapo madai yao yatakapopatiwa ufumbuzi.  Hata hivyo Madereva wa Malori kutoka Tanzania hawakujihusisha na mgomo huo kwasababu hakuwa ukiwahusu na waliendelea na kazi Hali iliyowakasitisha wenzao na hivyo kuyashambulia Malori yao kwa mawe na kuharibu vioo.  Balozi Mashiba jana Septemba 29, 2021 alikutana na baadhi ya Madereva wa Tanzania na kushauriana nao kuhusu namna Bora ya kuepuka mashamb

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI SEPTEMBA 30, 2021

Image
 

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO SEPTEMBA 29, 2021

Image
 

BENKI YA DUNIA YAJA NA NEEMA KWA TANZANIA

Image
  Na. Farida Ramadhan na Josephine Majura WFM- DODOMA Benki ya Dunia imeahidi kuisaidia Tanzania kukabiliana na athari za kiuchumi zilizosababishwa na ugonjwa wa UVIKO – 19 pamoja na kusaidia kutekeleza miradi itakayosaidia kukuza ajira kwa vijana, kuboresha miundombinu ya afya na elimu pamoja na kuendeleza rasilimali watu. Ahadi hiyo imetolewa Jijini Dodoma na Makamu wa Rais wa Benki hiyo, Dkt. Hafez Ghanem alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba. Aliyataja maeneo muhimu yatakayosaidia kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa ajira hususan kwa vijana kuwa ni pamoja na kuwekeza katika mifumo ya teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA), kuimarisha sekta ya nishati ya umeme, kuboresha miundombinu ya usafirishaji na kuimarisha sekta binafsi ili iweze kuchangia katika kutoa ajira na kukuza uchumi wa nchi. “Tumejadiliana mambo mengi lakini suala la muhimu ni kuhakikisha sekta binafsi inawekewa mazingira mazuri ya kuwekeza katika m