5/31/2021

5/30/2021

TANESCO YASIFIWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MIRADI.*

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limepongezwa na kusifiwa kwa utekelezaji thabiti wa Miradi mbalimbali ya Umeme ikiwemo miradi mikubwa ya kimkakati na miradi midogo midogo ya usambazaji Umeme Nchini kote. 
Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony Mtaka Tarehe 30 Mei 2021 alipotembelea banda la TANESCO katika maonyesho ya Teknolojia yanayoendelea katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. 
Sambamba na pongezi hizo, Mhe Mtaka ameshauri wataalamu wa Tehama wa Shirika kushirikiana na vyuo vya elimu ya juu ili kuboresha mifumo ya utoaji huduma ikiwemo  huduma za ununuzi wa umeme wa LUKU  na kuwezesha wateja kununua umeme kisha umeme huo kuingie  katika mita  bila kumlazimu mteja kwenda kuweka umeme katika mita.
Mhe. Mtaka amesema pamoja na mambo mengi mazuri ambayo TANESCO imekuwa ikiyafanya, ni vvyema Shirika likafanya  ushirika na taasisi za elimu ya juu ili kukuza ubunifu na kuwezesha wataalamu wa ndani kutumika katika kutekeleza miradi mbali mbali bila kuhitaji wataalamu kutoka nje ya nchi na ikiwezekana wataalamu wa Shirika waweze kufanya na kusimamia hata miradi mingine mikubwa inayotekelezwa katika nchi jirani.
 “Hii nikutokana na uzowefu ambao wataalam wa TANESCO watakuwa wameupata baada ya kukamilisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati” Alisema Mhe. Mtaka

Mhe. Mtaka aliongeza kuwa, Miradi  ya umeme vijijini inatekelezwa  kwa weledi wa hali ya juu, ni vyema sasa TANESCO ikawezesha wataalam wake kwa kushirikiana na Taasisi zingine za serikali kuanza kupeleka wataamamu katika kandarasi za usimamizi wa miradi nje ya Nchi.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Anthony  Mtaka akipokea maelezo  kutoka kwa Meneja wa TANESCO  Mkoa wa Dodoma   Mhandisi Kenneth Boimanda  wakati Mkuu huyo wa Mkoa alipotembelea Banda la TANESCO katika maonyesho ya teknolojia yanayo endelea katika Uwanja wa jamuhuri jijini Dodoma Leo  30 Mei 2021

Mhandisi Erasto Chiswanu akielekeza wanafunzi wa Shule Sekondari ya  Wasichana ya  Msalato jinsi Mradi wa Julius Nyerere unavyo tekelezwa  wakati wanafunzi hao walipo tembelea banda la TANESCO  katika maonyesho ya Teknolojia  yanayo endelea katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma Leo 30 Mei 2021
 

    

5/29/2021

JESHI LA POLISI LIMETOA MAFUNZO KWA MAFUNDI WA MAGARI

 

Na Mwandishi Wetu
JESHI la Polisi kitengo cha Usalama barabarani, limetoa mafunzo kwa mafundi magari waliyokuwa ndani ya Kituo cha Mabasi cha Magufuli, Mbezi Luis, Dar es Salaam kwa lengo la kuwafundisha jinsi ya kutambua vifaa ambavyo vipo kwenye magari hayo.
Mafunzo hayo yametolewa leo Mei 29, 2021 na Mkuu wa Usalama Barabarani, ASP Ibrahim Samwix ,kwa lengo la msfundi hao kutambua mfumo wa injini ya gari unavyofanya kazi ili kuwaraisishia namna ya utengenezaji wa magari.
Pia,Mkuu huyo  aliwafundisha kuhusu kifaa cha aina ya turbo kinavyofanya kazi, na namna ya kukitambua kama kikiwa  kibovu, kwa sababu mafundi wengi wamekuwa wakifanya masuala ya ufundi kwa mazoea.
ASP Samwix alitoa pia mafunzo katika kifaa cha mfumo wa rejeta namna kinavyofanya kazi, kwa sababu mafundi wengi na madereva wamekuwa wakishindwa kutunza mabasi wanayopewa kutokana na mapungu madogo madogo.
Kabla ya mafunzo hayo, Mkuu huyo alianza na madereva kwa kuelimisha jinsi ya kufuata sheria za barabarani na kuendesha gari kwa mwendo ambao unatakiwa ili kuepusha ajali na kuokoa maisha ya wananchi.
Kwa wa upande wa madereva hao ambao walikuwa zaidi ya 40, walilishukuru Jeshi la Polisi kwa mafunzo hayo, kwa sababu yanawakumbusha kufuata sheria za barabarani, kutokana na kwamba wengi wanafanya kazi hiyo kwa mazoea.
Pia, wanasema ni mara yao ya kwanza kupatiwa mafunzo, kwa hiyowao wameona ni bahati kubwa kwa sababu wamejifunza mambo mengi kwa wakati mmoja kwa sababu wakati mwingine tunahisi kuwa tumesahaulika
Waneomba elimu hiyo na mafunzo hayo yawe endelevu kwa manufaa yao na kwa manufaa ya watumiaji wa barabara, wao wapo tayari muda wowote na pia wataendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo.
Kwa upande wa abiria, Athuman Omary ambae ni Mkazi wa Tabata, Dar es Salaam alitoa shukrani kwa jeshi hilo kwa elimu ambayo walikuwa wanaitoa kwa dereva na wamiliki wa mabasi kwa sababu inaonesha ni jinsi gani wanajali maisha ya abiria.
Pia, Mkazi wa Ubungo, Mwajuma Juma aliwata madereva hao kutumia mafunzo waliyoyapa kwa kupunguza ajali za usalama barabarani kwa sababu kuna baadhi ya madereva hawafuati sheria hizo kwa makusudi.
Kwa upande wawamiliki wa mabasi, wamelipongeza jehi hilo kwa mafunzo ambayo wamepewa madereva wao pamoja na mafundi wa mabasi, wanasema hiyo itaondoa ajali za barabarani, itasaidia ulinzi wa magari yao na pia ushirikiano baina ya askari na wao utakuwa wa manufaa.



Mkuu wa Usalama Barabarani  Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli Mbezi luis Dar es eslaam ASP Ibrahim Samwix  akizungumza na mafundi  wa magari waliyokuwa ndani ya Kituo cha Mabasi cha Magufuli, Mbezi Luis, mkoa wa Dar es Salaam kwa lengo la kuwafundisha jinsi ya kutambua vifaa ambavyo vipo kwenye magari hayo.
Mafunzo hayo yametolewa leo Mei 29, 2021 
Mkuu wa Usalama Barabarani  Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli Mbezi luis Dar es eslaam ASP.Ibrahim Samwix (kushoto) akiendelea na kazi kama anayoonekana pichani.

    

MKUU WA MAJESHI JENERALI VENANCE MABEYO ATEMBELEA UBALOZI WA TANZANIA- PRETORIA

 Leo Jumamosi tarehe 29 Mei, 2021. Mkuu wa Majeshi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo, alitembelea Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Afrika Kusini.

Jenerali Mabeyo yupo Nchini Afrika Kusini kuhudhuria sherehe za kumuaga Mkuu Majeshi wa Afrika Kusini Jenerali Solly Zacharia Shoke zilizofanyika kitaifa Jana Mjini Pretoria. Kuhudhuria sherehe hizi, ni utaratibu uliowekwa na nchi wanachama wa Jumuiya za SADC ya maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) katika kuimarisha mashirikiano hususan katika Nyanja ya Diplomasia ya Ulinzi (Defence Diplomacy) na Amani katika eneo la nchi za SADC.

Jenerali Mabeyo, alikaribishwa Ubalozini na Mhe. Balozi Mej. Jen. Gaudence Salim Milanzi (Mst) na watumishi wa Ubalozi, Mhe. Balozi Milanzi alitoa taarifa fupi ya eneo la uwakilishi ya Afrika Kusini, Botswana na Falme ya Lesotho.

Katika taarifa hiyo, Mhe. Balozi alieeza kuwa hali ya uwakilishi inaridhisha kiulinzi na kiusalama, Ubalozi umeendelea kukuza mashirikiano na nchi za eneo la uwakilishi ikiwa ni pamoja na SADC. Kwa kufuata miongozo ya sera ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyoelekeza kuendeleza Diplomasia ya kisiasa na kutekeleza Diplomasia ya uchumi. 

Aidha, Mhe. Balozi alieleza kuwa hali ya UVIKO-19 iliathiri eneo la uwakilishi na athari kubwa imeonekana katika uchumi kama nchi nyingine duniani zilivyoathirika. Mapema mwezi huu Afrika Kusini imeanza kuonyesha dalili za uchumi wake kutengamaa, kutokana na sarafu yake ya Rand kuimarika dhidi ya sarafu ya dola ya Marekani.

Naye upande wake Jenerali Mabeyo aliielezea ziara yake kwa ujumla nchini Afrika Kusini imekuwa ni ya mafanikio, na pia kuna mambo kama Mkuu wa Majeshi amejifunza katika ziara hii. 

Jenerali Mabeyo alieleza kuwa hali ya nyumbani ni shwari na kazi inaeendelea.  Jenerali Mabeyo alisema Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amelenga kuendeleza maendeleo ndani na nje ya nchi mfano katika kutekeleza Sera ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwelekeo unaelekeza kuimarisha Diplomasia kwa kujenga mahusiano na nchi duniani kwa  kuimarisha Diplomasia ya siasa na Diplomasia ya uchumi. Jenerali Mabeyo alisisitiza kuwa ili malengo haya yafanikiwe kunahitajika kuwe na ushirikiano baina ya  watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na taasisi zingine zote ili kufanya utekelezaji wa diplomasia uendelee kuleta mafanikio siyo tu kwa Serikali bali kwa wananchi wa Tanzania kwa ujumla.

Jenerali Mabeyo alimwaomba Balozi na watumishi wa Ubalozi kuielewa dira ya Diplomasia kama ilivyoainishwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, ili kuweza kutelekeza majukumu yao kwa wepesi. 

Mwisho,  Jenerali Mabeyo  alitoa rai kwa watumishi wa Ubalozi kujenga mahusiano na nchi za eneo la uwakilishi kama Sera ya Mambo ya Nje inavyo elekeza.

Imetayarishwa na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pretoria.








    

CHAMA CHA WANASHERIA WANAWAKE (TAWLA) CHAFANYA MKUTANO MKUU WA 31 WA MWAKA


Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson Mwansasu akizungumza katika mkutano wa 31 wa mwaka wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) unaofanyika kwenye Hoteli ya Coral Beach Masaki mkoani Dar es Salaam leo Jumamosi 29,2020.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson Mwansasu akizungumza katika mkutano wa 31 wa mwaka wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) unaofanyika kwenye Hoteli ya Coral Beach Masaki jijini Dar es Salaam leo Jumamosi 29,2020 Katikati ni  Lulu Ngw'anakilala Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWLA na kushoto ni Mwanachama wa TAWLA Flaviana Charles Rwechungura.

Balozi Mwanaidi Maajal Mwanachama wa (TAWLA) akiongoza mjadala katika mkutano huo unaofanyika kwenye hoteli ya Coral Beach Masaki jijini Dar es salaam

Lulu Ngw'anakilala Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya (TAWLA) akimkaribisha mgeni rasmi ili kuzungumza na wanachama wa taasisi hiyo katika mkutano huo.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson Mwansasu kushoto, Lulu Ngw'anakilala Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TAWLA na Mwanachama wa (TAWLA) Flaviana Charles Rwechungura wakishiriki katika mkutano huo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanasheria Wanawake Tike Mwambipile akipiga makofi wakati mgeni rasmi Mh. Dk. Tulia Ackson hayupo pichani alipokuwa akizungumza.

Mwanachama wa (TAWLA) Flaviana Charles Rwechungura akizungumza katika mkutano huo.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Tulia Ackson Mwansasu kushoto akifuatilia mada katika mkutano huo.

Picha mbalimbali zikionesha wanachama wa Chama cha Wanasheria wanawake Tanzania (TAWLA) wakiwa katika mkutano huo unaofanyika kwenye hoteli ya Coral Beach jijini Dar es salaam.