Posts

Showing posts from October, 2023

WIZARA YA MADINI YAJA NA MKAKATI KABAMBE KUWAANDAA WATANZANIA WENYE USHINDANI

Image
  #Yageukia Vyuo vikuu, kati kutengeneza wataalam #Iko mbioni kurekebisha mitaala kuongeza tija Sekta ya Madini #Yadhamiria kutafsiri Vision 2030 kwa vitendo Serikali iko mbioni kupitia na kurekebisha mitaala ya elimu kwa Vyuo Vikuu na vya Kati kwa ajili ya kutengeneza wataalam wa kutosha na wenye ushindani mkubwa kuhudumia Sekta ya Madini nchini. Hayo yalielezwa na Kamishna wa Tume ya Madini, Janet Ruben Lekashingo, Oktoba 30, 2023, jijini Dodoma, katika mahojiano maalum na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Madini. Alisema katika kutafsiri Maono 2030, Madini ni Maisha na Utajiri, Wizara ya Madini imeamua kuongeza nguvu katika nyanja ya uboreshaji wa tija kwa watumishi pamoja na watoa huduma katika sekta ya madini. Kamishna Janet alisema katika kusimamia ushirikishwaji wa Watanzania katika mnyororo mzima wa Sekta ya Madini, Serikali itashirikiana na Kampuni zilizowekeza sekta ya madini hapa nchini ili kujua uhitaji wao kwenye huduma wanazopatiwa na Watanzania katika miradi

TANZANIA YA TATU KWA MAZINGIRA MAZURI YA UWEKEZAJI BARANI AFRIKA

Image
  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Mhe. Prof. Kitila Mkumbo amebainisha kulingana na tafiti za kimataifa Tanzania ni nchi ya tatu kwa Mazingira mazuri ya Uwekezaji barani Afrika, ikitanguliwa na Nigeria na Afrika Kusini. Amesema hayo leo Oktoba 31, 2023 jijini Dar es Salaam katika ufunguzi wa jukwaa la Biashara lililowakutanisha wawekezaji kutoka Tanzania na Ujerumani. Aliongeza kuwa maboresho yaliyofanyika katika sheria, sera na kiutumishi chini ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan yamepelekea kufanya vizuri katika Uwekezaji barani Afrika. Prof. Mkumbo amebainisha kuwa maeneo aliyojadiliana ambayo Ujerumani yanaweza kuwekeza ni pamoja na Nishati jadilifu, kuzalisha umeme wa maji, jua na upepo pia uzalishaji wa madini ya kimkakati ya kutengeneza betri na kuunganisha magari ikiwemo Volkswagen. " Tunakaka Tanzania kuchukua nafasi yake katika ukanda Afrika katika kuwekeza Viwanda vya kutengeneza magari". Prof. Mkumbo ameon

BUNGE LAPITISHA AZIMIO LA MAPENDEKEZO YA KURIDHIA MKATABA WA KUANZISHA TAASISI YA DAWA YA AFRIKA YA 2019

Image
  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo tarehe 31, Oktoba 2023, limepitisha azimio la Mapendekezo ya Kuridhia Mkataba wa Kuanzisha Taasisi ya Dawa ya Afrika ya Mwaka 2019 (Treaty for Establishiment of the African Medicines Agency -AMA ) katika bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Jijini Dodoma wakati wa Bunge la 12 Mkutano wa13 kikao cha kwanza Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu amesema kuwa utekelezaji wa AMA, upo uwezekano kwa nchi kupata manufaa zaidi ikiwa ni pamoja na kuimarika kwa mfumo wa udhibiti wa bidhaatiba na hivyo kuweza kudhibiti bidhaa ambazo kwa sasa hazijaanza kudhibitiwa kama vile viambata hai, damu na bidhaa zake, tiba za kijenetiki na chembe msingi Waziri Mwalimu amesema AMA itasaidia Tanzania kuwezesha kuongeza viwanda vya bidhaa tiba vya hapa nchini na kuwasilisha taarifa kwa nchi wanachama wa AMA za kuomba usajili zenye vigezo vinavyofanana na hivyo kupunguza usumbufu na muda wa kusajili bidhaa zao katika nchi hizo “AMA itasaidia kuimarika kwa

RAIS SAMIA PAMOJA NA MGENI WAKE RAIS WA JAMHURI YA SHIRIKISHO LA UJERUMANI WAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu ziara ya mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mhe. Dkt. Frank-Walter Steinmeier nchini Tanzania. Mkutano huo na Waandishi wa Habari umefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Oktoba, 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akizingumza na waandishi wa habari kuelezea yaliyojili kwenye mazungumzo na mgeni wake Rais wa Ujerumani   Mheshimiwa Frank-Walter Steinmeier Ikulu jijini Dar es Salaam     Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mhe. Dkt. Frank-Walter Steinmeier akizungumza kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari kuhusu ziara yake nchini Tanzania. Mkutano huo umefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Oktoba, 2023. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Y. Makamba (Mb,) akifuatilia mkutano wa Rais Samia na Rais wa Ujerumani Mheshimiwa Frank-Walter Steinmeier na waandi

KITUO CHA MABASI CHA KISASA CHENYE THAMANI YA SH.13 BILIONI KUJENGWA GEITA

Image
  KUPITIA Mradi wa Uboreshaji wa Miji Tanzania (TACTS) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia (WB) inatarajia kujenga kituo cha mabasi cha kisasa mjini Geita chenye thamani ya shilingi bilioni 13. Hayo yamebainishwa leo Oktoba 31,2023 na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Zahara Michuzi mara baada ya kukagua eneo lililotengwa kwa mradi huo ambalo limemegwa kutoka hifadhi ya msitu wa Usindakwe. Zahara amesema kituo hicho cha mabasi (stendi) kinakwenda kutatua kero ya muda mrefu kwa mji na mkoa wa Geita kwani stendi ya sasa haina ubora wa miundombinu inayostahimili kutoa huduma bora. “Hatuna stendi yenye hadhi ya mkoa wenye dhahabu na madini, mheshimiwa Rais kwa kuliona hilo ametupatia hiyo stendi na sasa hivi tupo katika hatua ya upembuzi yakinifu na hatua za manunuzi. “Tupo hatua za kuweza kupata mkandarasi mzuri mwenye uzoefu wa kujenga stendi hizi, zenye ubora na kuvutia katika mji wetu, kwa hiyo hizo taratibu zimeanza na zinaendelea.” Amesema hadi Disemba, 2023 taratibu zote za awa

KATAMBI: MAPITIO YA SERA YA WATU WENYE ULEMAVU YAMEANZA

Image
Na Mwandishi Wetu, DODOMA   Serikali imeanza kufanya mapitio ya Sera ya Taifa ya Maendeleo na Huduma kwa Watu wenye Ulemavu ya Mwaka 2004 ili kukidhi mahitaji yaliyopo. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe.Patrobas Katambi ameyasema hayo Oktoba 31, 2023 bungeni alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Viti maalum (CCM), Mhe. Stella Ikupa ambaye amehoji mkakati wa serikali kufanya marekebisho ya Sheria namba 9 ya Mwaka 2010 ya Watu Wenye Ulemavu. Akijibu swali hilo, Mhe.Katambi amesema mkakati wa serikali kwa sasa ni kufanya mapitio ya Sera ya Taifa ya Maendeleo na Huduma kwa Watu wenye Ulemavu ya Mwaka 2004 ambapo utekelezaji wake umeanza. Aidha, amesema baada ya kukamilika kwa mapitio ya Sera ya Mwaka 2004 hatua za marekebisho ya Sheria hiyo zitaanza kwa kuzingatia mapungufu yatakayobainishwa katika tathmini ya utekelezaji wa Sera hiyo. Katika swali la nyongeza, Mbunge wa Viti maalum (CCM), Mhe.Mariam Kisangi amehoji serikali ime

RAIS SAMIA AFANYA MAZUNHGUMZO NA MGENI WAKE RAIS WA UJERUMANI FRANK-WALTER STEINMEIR

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mhe. Frank-Walter Steinmeier mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Oktoba, 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mhe. Frank-Walter Steinmeier mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Oktoba, 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mhe. Frank-Walter Steinmeier mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Oktoba, 2023 Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani Mhe. Frank-Walter Steinmeier akiongoza ujumbe wa Nchi yake kwenye mazungumzo Rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan aliyeongoza ujumbe wa Tanzania Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 31 Oktoba, 2023. Rais wa Jamhur

RAIS WA UJERUMANI STEINMEIR AWASILI NCHINI

Image
W aziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Y. Makamba na  Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mheshimiwa Frank-Walter Steinmeier wakifurahia ngoma za jadi (hawapo pichani)  kwenye hafla ya mapokezi ya Rais huyo katika  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam    Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mheshimiwa Frank-Walter Steinmeier akipunga mkono mara baada ya kuwasili nchini. Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mheshimiwa Frank-Walter Steinmeier akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mheshimiwa Frank-Walter Steinmeier akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Y. Makamba (Mb.) wakati alipompokea katika  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Y. Makamba na  Rais wa Jamhuri ya S

RAIS WA IPU AWAOMBA WATANZANIA USHRIKIANO ILI KUONESHA UTOFAUTI

Image
  Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson ameomba ushirikiano kutoka kwa Watanzania wote ili kuionyesha Dunia utofauti wa Tanzania kuishika nafasi hiyo.   Dkt. Tulia ambaye pia ni Spika wa Bunge la Tanzania ametoa kauli hiyo leo Bungeni Dodoma katika halfa ya kumpokea akitokea Nchini Angola ambako alishinda nafasi ya Rais wa IPU katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 27, 2023.   Amesema Tanzania inayo nafasi ya kufanya vizuri katika nafasi hiyo iwapo kutakuwepo ushirikiano kutoka kwa watu wote. “Nafasi hii ni yetu wote, ukiwa na ushauri wa namna ya kuupeleka umoja huu mbele tuletee ili tufanye vizuri, usisuburi tushindwe. “Ifike mahali tukitaka nafasi nyingine kimataifa tupate kwa kuwa tulifanya vizuri kwenye hii, tutasikiliza ushauri wenu, ninaamini tutafanya vizuri na Dunia itajua kwamba tulishawahi kushika hii nafasi, viongozi wa dini muendelee kutuombea,” alisema. Alitoa wito kwa Watanzania kuondoa tofauti zao kwenye masuala ya uwakilishi wa Tanz