HUDUMA YAMAJI YAZIDI KUIMARIKA KATAVI
Wataalam wa sekta ya maji wakikagua mfumo unaochukua maji kutoa ziwa Tanganyika katika mrdi wa maji wa kijiji cha Karema. Sehemu ya mradi huo imekamilishwa kwa kuwatumia wataalam wa Wizara ya Maji kupitia utaratibu wa force account. 1. Mkurugenzi Msaidizi, Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Maji Bw. Alex Tarimo (kushoto) akijidhirisha kuhusu upatikanaji wa maji katika kijiji cha Werema, wilayani Tanganyika ambapo wananchi wanapata huduma hiyo katika vizimba 14 vya umma. Mkurugenzi Msaidizi, Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Maji Bw. Alex Tarimo (kushoto), akimsikiliza Afisa Tarafa wa kijiji cha Karema, wilayani Tanganyika Bw. Mbonimpaye Mtiyonza Nkoronko, anayeelea kuhusu huduma ya maji katika eneo lake la kazi, ambapo huduma hiyo inatolewa kwa saa 24, katika vituo 14 vya wananchi, na baadhi waliounganishiwa katika makazi yao. Huduma ya maji mkoani Katavi inazidi kuimariki baada ya miradi ya maji iliyokuwa ikitekelezwa kukamilika na wananchi kuanza kupata huduma hiyo