9/30/2020

HUDUMA YAMAJI YAZIDI KUIMARIKA KATAVI

   Wataalam wa sekta ya maji wakikagua mfumo unaochukua maji kutoa ziwa Tanganyika katika mrdi wa maji wa kijiji cha Karema. Sehemu ya mradi huo imekamilishwa kwa kuwatumia wataalam wa Wizara ya Maji kupitia utaratibu wa force account.

1.   Mkurugenzi Msaidizi, Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Maji Bw. Alex Tarimo (kushoto) akijidhirisha kuhusu upatikanaji wa maji katika kijiji cha Werema, wilayani Tanganyika ambapo wananchi wanapata huduma hiyo katika vizimba 14 vya umma.


 

   Mkurugenzi Msaidizi, Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Maji Bw. Alex Tarimo (kushoto), akimsikiliza Afisa Tarafa wa kijiji cha Karema, wilayani Tanganyika Bw. Mbonimpaye Mtiyonza Nkoronko, anayeelea kuhusu huduma ya maji katika eneo lake la kazi, ambapo huduma hiyo inatolewa kwa saa 24, katika vituo 14 vya wananchi, na baadhi waliounganishiwa katika makazi yao.

Huduma ya maji mkoani Katavi inazidi kuimariki baada ya miradi ya maji iliyokuwa ikitekelezwa kukamilika na wananchi kuanza kupata huduma hiyo karibu na makazi yao.

Meneja wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoani Katavi Mhandisi Peter Mugula amesema kuimarika huko ni matokeo ya  jumla ya miradi ya maji 14 kukamilika. Ameongeza kuwa miradi 24 ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji na inatarajiwa kukamilika kabla ya Desemba 2020.

Mhandisi Mugula amesema hadi mwezi Agosti 2020 asilimia 62 kutoka asilimia 51 ya wakazi waishio vijijini tayari walishapata huduma ya maji, na mjini asilimia ya ilipanda hadi 75 kutoka asilimia 40 ya wananchi waliokuwa wakipata huduma ya maji. Amefafanua kuwa mabadiliko hayo yametokana na baadhi ya miradi kukamilishwa na wataalam wa sekta ya maji kwa utaratibu wa force account.

Ameainisha kuwa miradi ya maji ya mjini inasimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira (MUWASA), ambapo hivi sasa mamlaka hiyo imeanza maandalizi ya kujenga mradi wa maji wa Kanoge II utakaozalisha maji mita mita za ujazo 1,200. Mradi wa Kanoge utaimarisha zaidi upatikanaji wa maji hadi kufikia mita za ujazo 8,700 hivyo kufanya kiwango cha upatikanaji maji kufika asilimia 87. 

Mhandisi Mugula amesema kuwa lengo ni kuwafikia wananchi wote katika huduma ya maji na hakuna atakayeachwa. Takwimu za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 inaonyesha kuwa mkoa wa Katavi una jumla ya watu 564, 604 na mwaka 2018 mkoa huo ulikadiriwa kuwa na idadi ya watu 738, 237.

 


    

KATIBU WA BUNGE STEPHEN KAGAIGAI AFANYA MAZUNGUMZO NA AFISA MTENDAJI MKUU WA BENKI YA NMB JIJINI DODOMA

Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kulia) akizungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Benki, Ndg. Ruth Zaipuna alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kulia) akimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Benki, Ndg. Ruth Zaipuna alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (wanne kulia) akizungumza na ugeni kutoka NMB Benki ulioongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo, Ndg. Ruth Zaipuna (kulia kwake) walipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.
Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kulia) akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Benki, Ndg. Ruth Zaipuna alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.(PICHA NA OFISI YA BUNGE).
 

    

JAJI MMILLA ATAKUMBUKWA KWA KUJITOA KWAKE, MWILI WAKE WAZIKWA GOBA JIJINI DAR

   


*********************************** 
Mwili wake Wazikwa Goba Dar es salaam 

Na Mary Gwera na Lydia Churi-Mahakama

Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amemuelezea Marehemu Jaji Bethuel Mmilla kuwa alikuwa ni mchapakazi na atakumbukwa kwa utendaji kazi wake wa kujitoa na ushirikiano.

Mwili wa aliyekuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Bethuel Mpakani Kasefu Mmilla umezikwa jana nyumbani kwake Goba Michungwani jijini Dar es salaam baada ya kuagwa katika viwanja vya Karimjee na baadaye kufanyiwa Ibada katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (K.K.K.T) Usharika wa Mwenge jijini Dar es salaam.

Akizungumza katika hafla ya kuuaga mwili wa marehemu Jaji Mmilla aliyefariki usiku wa Septemba 24, Jaji Mkuu alisema wasifu wa marehemu Jaji Mmilla ni mfano mzuri wa namna alivyowatumikia zaidi walio wengi kuliko alivyojitumikia kwa maslahi yake binafsi au maslahi ya familia yake.

“Wasifu wake unaonyesha kuwa kila kituo katika utumishi wake wa Mahakama, amekuwa ni wa kutumikia, anayetoa, na asiye wa kutumikiwa,” alisema Mhe. Jaji Mkuu.

Aliongeza kuwa Maamuzi yaliyotolewa na marehemu Jaji Mmilla yatabaki kuwa mifano hai ya mambo yote aliyoyaamini na kuyatekeleza kwa vitendo. Alisema marehemu atakumbukwa pia kwa ucheshi na utani wake wa mara kwa mara ambao uliwasaidia waheshimiwa Majaji wa Rufaa kusahau angalau kidogo, maswala magumu ya kisheria na kimaamuzi.

Kwa upande mwingine, Mhe. Jaji Mkuu amewashukuru madaktari, wahudumu wote wa Hospitali ya Jeshi Lugalo, Hospitali ya Taifa Muhimbili na wale wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakiongozwa na Prof. Mohamed Janabi kwa kuwa karibu na marehemu.

Akitoa salaam kwa niaba ya Majaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji wa Mahakama hiyo, Mhe. Augustine Mwarija alimuelezea Marehemu Jaji Mmilla kuwa alikuwa ni kiongozi mwenye ushirikiano mkubwa na wenzake na aliyekuwa akiwatia moyo katika kazi mbalimbali za utoaji haki.

Naye Mwenyekiti wa chama cha wanasheria Tanzania (Tanganyika Law Society) Mhe. Dkt. Rugemeleza Nshalla amewashauri Majaji na Mahakimu kuandika hukumu zenye mguso chanya katika maisha ya watu na utawala wa sheria.

“Marehemu Jaji Mmilla aliandika hukumu nyingi ambazo zitatumika kama rejea kwa wanafunzi wanaosoma sheria nchini, Mahakimu pamoja na Majaji” alisema Dkt. Nshalla.

Dkt. Nshalla pia aliwaasa familia ya marehemu kwa kuwasahuri kuishi kwa kupendana na kushirikiana ili kuyaenzi mazuri aliyoyafanya marehemu Jaji Mmilla.

Mazishi ya Marehemu Jaji Mmilla yalihudhuriwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, Majaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Dkt. Eliezer Feleshi, Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, wadau mbalimbali pamoja na watumishi wa Mahakama.

Jaji Mmilla alifariki dunia usiku wa Septemba 25, 2020 katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) iliyopo kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Awali marehemu alilazwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo jijini Dar es salaam Septemba 23, 2020 alipokuwa akipatiwa matibabu na baadaye kuhamishiwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) alipofariki dunia.
    

MAJALIWA AHUTUBIA MKUTANO WA KAMPENI KATA YA KAYANGA, WILAYANI KARAGWE, MKOA KAGERA.

 

Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Kata ya Kayanga, wilayani Karagwe, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)

 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa akipiga magoti ya kuwaomba wananchi wa jimbo la Karagwe kupigia kura wagombea wote wa Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi mkuu utakaofanyika oktoba 28, 2020, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika  uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)

Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwakabidhi nakala ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020-2025 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa (kushoto) na Mgombea Udiwani Kata ya Kayanga, Germanus Byabusha (katikati), katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)

Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia mamia ya wananchi wa Kata ya Kayanga, wilayani Karagwe, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)

    

ASKARI WA HIFADHI YA TAIFA YA SAADANI KWA KUSHIRIKIANA NA JESHI POLISI PANGANI WAWAKAMATA WAHAMIAJI HARAMU 32

 

Kamishna  Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora akizungumza kuhusu tukio la kukamatwa kwa wahamiaji haramu karibu na hifadhi ya Taifa ya Saadani
Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda akizungumza kuhusu tukio hilo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah Issa kushoto ni Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Baraka Batenga
Kamishna  Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora kushoto akimsikiliza kwa umakini Mkuu wa Polisi wilaya ya Pangani (OCD) Georgina  Matagi wakati wa tukio hilo
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda kushoto akisisitiza jambo kwa Mkuu wa wilaya ya Pangani kulia Zainabu Abdallah Issa na anayefuatia ni Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora
Kamishna  Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora kushoto akisisitiza  jambo wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda kuhusu namna walivyofanikisha ukamataji huo wa wahamiaji haramu
Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda kushoto akiwa na Mkuu wa Polisi wilaya ya Pangani (OCD) Georgina Matagi wakiwahoji wahamiaji haramu hao 
Mkuu  wa Polisi wilaya ya Pangani (OCD) Georgina Matagi kulia akisisitiza jambo wakati akieleza namna wahamiaji hao walivyokamatwa
Sehemu ya Wahamiaji haramu hao waliokamatwa
 

ASKARI wa Hifadhi ya  Taifa ya Saadani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wilayani Pangani wamefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu 32 waliokutwa wakiwa karibu na hifadhi hiyo wakisafirishwa kupelekwa nchi za kusini mwa Afrika.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwa wahamiaji hao Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora alisema kwamba wahamiaji hao walikamatwa Septemba 27 mwaka huu usiku.

 Alisema ukamatwa huo waliofanya baada ya kupata taarifa kutoka wananchi wa Kijiji cha Buyuni kupitia Mwenyekiti wa Kijiji hicho Diwani Akida ambaye aliwaeleza uwepo wa mazingira yasiyoridhisha kwenye eneo lake hasa eneo la bahari baada ya boti moja kukwama.

 

Alisema baada ya kupata taarifa hiyo wao kama wahifadhi wana jukumu la kulinda maliasili na kuangalia usalama kwenye miji yote inayowazunguka waliandaa kikosi kazi cha kwanza waliokwenda eneo la tukio na walipofika waliwakuta wahamiaji hao eneo la bahari karibu na hifadhi hiyo katika kijiji cha Buyuni.

 

 “Tulipofika tuliwaweka chini ya ulinzi na baadae tukawasiliana na Mkuu wa Polisi wilaya ya Pangani (OCD) Georgina Matagi ambaye alitoa ushirikiano mkubwa kwa sababu wanaandaa askari kwa kuwapa msaada baada ya kuangalia umbali kutoka Pangani mpaka eneo la tukio”Alisema

Alisema baadae hapo waliamua kutuma kikosi cha pili na ndipo walipofika na kufanikiwa kukaweka chini ya ulinzi wahamiaji 28 ambao ni raia wa Ethiopia  lakini alfarji ya leo wakapata taarifa nyengine ya uwepo wa wahamiaji wengine wanne ambao ni raia wa Somalia na wakatuma kikosi na kufanikiwa kuwaweka chini ya ulinzi.

“Kati yao wapo wahamiaji 32 raia wa Ethiopia 28 na raia wa Somalia wanne akiwemo mwanamke mmoja kwa hiyo baada ya kufanikisha tukio hilo tumewafikisha na kuwakabidhi kwenye mamlaka ya Polisi kwa ajili ya hatua zaidi”Alisema

Awali akizungumza kuhusiana na tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda aliwapongeza askari wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani kwa kazi nzuri kwa kushirikiana na askari wa Jeshi la Polisi wilaya ya Pangani.

“Kwa kweli niwapongeze askari wa hifadhi ya Taifa ya Saadani ka kazi nzuri kufanikisha kukamatwa kwa wahamiaji hao kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Pangani niwaambie tu kwamba mawakala wanaojishughulisha na usafirishaji wa wahamiaji haramu mkoani Tanga hawatasalimika tutawasaka popote iwe ni nchi kavu,majini na kisha kufikishwa mahakamani

Hata hivyo amesema kwamba hivi sasa wametangaza vita mpya kwa mawakala wanaojishuhulisha na usafirishaji wa wahamiaji haramu mkoani Tanga kwamba hawatasalimika watasakwa popote iwe ni nchi kavu, majini na kisha kufikishwa mahakamani.

Alisema juhudi hizo ni nzuri na zinapaswa kuwa endelevu ili kuweza kuhakikisha wahamiaji haramu hawapiti tena kwenye maeneo hayo ikiwemo wananchi kuendelea kuwafichua wanapowaona watu na kuwatilia mashaka.

“Labda niwaambie tu kwamba wale wanaojihusisha na usafirishaji wa wahamiaji haramu mkoani hapa hawatabaki salama kwa sababu huo ni uhalifu unaovuta mipaka na uhalifu huu hauwezi kukubalika hapa nchini”Alisema

 “Sisi sote tunafahamu kinachoendelea nchini Somalia tunauhakika gani wanaweze wakawa wanapita wakaenda hawawezi kwenda kuungana na wenzao nchini msumbiji …tuna uhakika gani hawawezi kubaki masalia nchini wakafanya wanayoyafanya huko walipotoka”Alisema 

Naye kwa upande wake Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Baraka Batenga alisema ni kweli lipo wimbo la wahamiji haramu kutoa pembe ya afrika kuja Tanzania kwa nia ya kupitia kwenda kusini mwa Afrika kwea lengo la kwenda kujitafutia maisha bora.

Alisema katikati kulikuwa kumetulia hasa kwenye kipidi cha ugonjwa wa Corona labda wanaamini hiyo ilitokana na majirani zao walikuwa wameweka vizuizi vya watu kutoka sehemu moja kwenda jengine.

Alisema lakini hivi karibuni wimbi hilo limeanza kupanda na wao wanakabilia nalo na walianza kukabiliana nalo kwa wilaya za Mkinga ambao wanaingilia maeneo ya moa,jasini kupitia mwakijembe kwa sasa wameweka task force ndogo kama sehemu ya mkakati ya kukabilia na wimbi la wahaamiaji haramu na wamekuwa na mafanikio makubwa na kuweza kudhibiti kwa kiasi kikubwa.

“Kwani Katika kipindi cha Agosti mpaka leo wilaya ya Mkinga wamekamatwa wahamiaji haramu kutoka nchini Ethiopia 37 na Muheza 7, Handeni waethipia 8 ambao walikuwa hawakutani nao ni wasomali na hivyo ni kesi ya kwanza kutokana na kwamba hawajakamtwa muda mrefu”Alisema

Hata hivyo alisema wanaofanya mambo hayo ni watanzania na kibaya zaidi hivi karibuni wilaya ya Muheza walimkamata mwenyekiti wa kijiji cha Upare naye ameingia kwenye kundi hilo hawakumuacha salama yupo kwenye mikono ya sheria .

Hata hivyo Mwenyekiti wa Kijiji cha Buyuni Diwani Akida alisema kijiji hicho kimepakana na hifadhi ya Taifa ya Saadani alisema hali ya usalama sio nzuri kiupande wao huku wanawashukuru wenzao wa hifadhi ya Taifa ya Saadani wanatoa msaada sana kwao wakati panapojitokeza matatizo yoyote wanakuwa karibu kuwasaidia.

Alisema kama  Septemba 27 mwaka huu saa moja usiku walifika wasomali na boti yao hatukujua wana silaha gani lakini walipofika ikabidhi tukawazingira na kutoa taarifa kwa Saadani kwa sababu wapo wakafika wakawadhibiti na baadae pia kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi wilaya ya Pangani walipofika wakawachukua.

    

LATRA YATANGAZA NAUALI MPYA YA TRENI MOSHI-ARUSHA

  


Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imetangaza nauli za treni ya abiria itakayofanya safari zake kutoka Moshi mjini hadi Arusha na kurudi Moshi.


Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Arusha leo tarehe 29 Septemba, 2020, Mkurugenzi Mkuu wa LATRA Gilliard Ngewe amesema nauli hizo zimetangazwa kufuatia Shirika la Reli Nchini (TRC) kuwasilisha maombi ya nauli hizo, ambapo LATRA ilifanya mikutano ya kupokea maoni ya wadau, kisha kufanya uchambuzi wa maoni hayo pamoja na kuchambua mchanganuo uliowasilishwa na TRC. 


Kwa mujibu wa kifungu cha 21 (2) (b) cha Sheria ya LATRA namba 3 ya 2019, baada ya mchakato wa uchambuzi kukamilika, Bodi ya Wakurugenzi ya LATRA imeidhinisha nauli hizo na kuainisha nauli zitakazotumika kwa usafiri wa treni ndani ya mikoa hiyo na nje ya mikoa kama inavyoonekana katika jedwali.


Nauli zilizoidhinishwa na LATRA zikionesha mchanganuo wa vituo vya ndani nan je ya mikoa husika



KUTOKA MOSHI KWENDAUmbali (KM)NAULI KWA MADARAJA HUSIKA (SHS):
Daraja la tatuPili kukaa
1RUNDUGAI221,0001,500
2KIKULETWA311,0001,500
3KIA371,0001,500
4USA RIVER621,5002,000
5TENGERU651,5002,000
6CHEKERENI751,5002,000
7NJIRO821,5002,000
8ARUSHA861,5002,000

KUTOKA ARUSHA KWENDAUmbali (KM)NAULI KWA MADARAJA HUSIKA (SHS):
Daraja la tatuPili kukaa
1NJIRO41,0001,500
2CHEKERENI111,0001,500
3TENGERU211,0001,500
4USA RIVER241,0001,500
5KIA491,5002,000
6KIKULETWA551,5002,000
7RUNDUGAI641,5002,000
8MOSHI861,5002,000


Nauli za wanafunzi kutoka mwanzo hadi mwisho wa safari ni Sh. 300.00 kwa daraja la tatu, na Sh 400.00 kwa daraja la pili kukaa.

Mkurugenzi Mkuu LATRA Gilliard Ngewe akimkabidhi Henry Machoke, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara TRC andiko la nauli zilizoidhinishwa

Wakati huo huo, LATRA imeiagiza TRC kutekeleza masuala mbali mbali ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya usalama kwa wadau husika, kutumia mfumo wa tiketi za kielektroniki, kutoa ratiba za safari kwa umma, kutekeleza hatua za usalama kudhibiti msongamano wa abiria, kuboresha miundombinu na huduma za kijamii, kuweka kitengo cha huduma kwa wateja na kutangaza nauli zilizoidhinishwa katika vyombo mbalimbali vya habari ili ziwafikie wadau wengi zaidi

    

9/29/2020

RAIS DKT.SHEIN AFUNGUA JENGO LA ABIRIA TERMINAL III ZANZIBAR

 


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia ikiwa ni ishara ya Ufunguzi wa jengo la Abiria la (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,hafla iliyofanyika leo Kisauni Wilaya ya Magharibi (B) Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja (kulia kwa Rais) Mgombe wa Urais Zanzibar Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi), 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(wa pili kushoto) akikata utepe kuashiria  Ufunguzi wa jengo la Abiria la (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,hafla iliyofanyika leo Kisauni Wilaya ya Magharibi (B) Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja (kulia) Mgombe wa Urais Zanzibar Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi)akifuatiwa na Makamo wa Pili wa Rais  wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Balozi Mdogo wa China aliyepo Zanzibar Xe Xiaowu .

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Waziri wa Ujenzi,Usafirishaji na Mawasiliano Mhe. Sira Ubwa Mamboya (katikati) wakipata maelezo kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Nd,Mustafa Aboud Jumbe (wa pili kulia) alipokagua jengo la  Abiria la (Terminal III) baada ya ufunguzi rasmi uliofanyika leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,  Kisauni Wilaya ya Magharibi (B) Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja (kushoto)Meneja wa Ujenzi Jengo Nd.Yasser De Costa 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein( katikati) akiwapungia mkono wananchi katika hafla ya  Ufunguzi wa jengo la Abiria la (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,hafla iliyofanyika leo Kisauni Wilaya ya Magharibi (B) Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja (kulia kwa Rais )  Waziri wa Ujenzi,Usafirishaji na Mawasiliano Mhe. Sira Ubwa Mamboya 

Msanii wa kizazi kipya Asley akiwaburudisha wananchi na Viongozi waliohudhuria katika sherehe za Ufunguzi wa jengo la Abiria la (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,hafla iliyofanyika leo Kisauni Wilaya ya Magharibi (B) Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja

Picha na Ikulu