Posts

Showing posts from September, 2020

HUDUMA YAMAJI YAZIDI KUIMARIKA KATAVI

Image
    Wataalam wa sekta ya maji wakikagua mfumo unaochukua maji kutoa ziwa Tanganyika katika mrdi wa maji wa kijiji cha Karema. Sehemu ya mradi huo imekamilishwa kwa kuwatumia wataalam wa Wizara ya Maji kupitia utaratibu wa force account. 1.    Mkurugenzi Msaidizi, Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Maji Bw. Alex Tarimo (kushoto) akijidhirisha kuhusu upatikanaji wa maji katika kijiji cha Werema, wilayani Tanganyika ambapo wananchi wanapata huduma hiyo katika vizimba 14 vya umma.       Mkurugenzi Msaidizi, Ufuatiliaji na Tathmini wa Wizara ya Maji Bw. Alex Tarimo (kushoto), akimsikiliza Afisa Tarafa wa kijiji cha Karema, wilayani Tanganyika Bw. Mbonimpaye Mtiyonza Nkoronko, anayeelea kuhusu huduma ya maji katika eneo lake la kazi, ambapo huduma hiyo inatolewa kwa saa 24, katika vituo 14 vya wananchi, na baadhi waliounganishiwa katika makazi yao. Huduma ya maji mkoani Katavi inazidi kuimariki baada ya miradi ya maji iliyokuwa ikitekelezwa kukamilika na wananchi kuanza kupata huduma hiyo

KATIBU WA BUNGE STEPHEN KAGAIGAI AFANYA MAZUNGUMZO NA AFISA MTENDAJI MKUU WA BENKI YA NMB JIJINI DODOMA

Image
Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kulia) akizungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Benki, Ndg. Ruth Zaipuna alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kulia) akimsikiliza Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Benki, Ndg. Ruth Zaipuna alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (wanne kulia) akizungumza na ugeni kutoka NMB Benki ulioongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo, Ndg. Ruth Zaipuna (kulia kwake) walipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma. Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai (kulia) akisalimiana na Afisa Mtendaji Mkuu wa NMB Benki, Ndg. Ruth Zaipuna alipomtembelea leo Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.(PICHA NA OFISI YA BUNGE).  

JAJI MMILLA ATAKUMBUKWA KWA KUJITOA KWAKE, MWILI WAKE WAZIKWA GOBA JIJINI DAR

Image
      ***********************************  Mwili wake Wazikwa Goba Dar es salaam  Na Mary Gwera na Lydia Churi-Mahakama Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma amemuelezea Marehemu Jaji Bethuel Mmilla kuwa alikuwa ni mchapakazi na atakumbukwa kwa utendaji kazi wake wa kujitoa na ushirikiano. Mwili wa aliyekuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mhe. Bethuel Mpakani Kasefu Mmilla umezikwa jana nyumbani kwake Goba Michungwani jijini Dar es salaam baada ya kuagwa katika viwanja vya Karimjee na baadaye kufanyiwa Ibada katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (K.K.K.T) Usharika wa Mwenge jijini Dar es salaam. Akizungumza katika hafla ya kuuaga mwili wa marehemu Jaji Mmilla aliyefariki usiku wa Septemba 24, Jaji Mkuu alisema wasifu wa marehemu Jaji Mmilla ni mfano mzuri wa namna alivyowatumikia zaidi walio wengi kuliko alivyojitumikia kwa maslahi yake binafsi au maslahi ya familia yake. “Wasifu wake unaonyesha kuwa kila kituo katika utumishi wake wa Mahakama, amekuwa n

MAJALIWA AHUTUBIA MKUTANO WA KAMPENI KATA YA KAYANGA, WILAYANI KARAGWE, MKOA KAGERA.

Image
  Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi wa Kata ya Kayanga, wilayani Karagwe, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura)  Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa akipiga magoti ya kuwaomba wananchi wa jimbo la Karagwe kupigia kura wagombea wote wa Chama Cha Mapinduzi katika Uchaguzi mkuu utakaofanyika oktoba 28, 2020, katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika  uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura) Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwakabidhi nakala ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2020-2025 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa (kushoto) na Mgombea Udiwani Kata ya Kayanga, Germanus Byabusha (katikati), katika mkutano wa kampeni, uliyofanyika uwanja wa Changarawe, Septemba 29, 2020. (Picha Eliud Rwechungura) Mjumbe wa Kamati Kuu, Kassim Majaliwa, akiwahutubia mamia ya wananchi wa Kata ya Kayanga, wilayani Karagwe, katika m

ASKARI WA HIFADHI YA TAIFA YA SAADANI KWA KUSHIRIKIANA NA JESHI POLISI PANGANI WAWAKAMATA WAHAMIAJI HARAMU 32

Image
  Kamishna  Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora akizungumza kuhusu tukio la kukamatwa kwa wahamiaji haramu karibu na hifadhi ya Taifa ya Saadani Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda akizungumza kuhusu tukio hilo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Pangani Zainabu Abdallah Issa kushoto ni Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Baraka Batenga Kamishna  Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora kushoto akimsikiliza kwa umakini Mkuu wa Polisi wilaya ya Pangani (OCD) Georgina  Matagi wakati wa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda kushoto akisisitiza jambo kwa Mkuu wa wilaya ya Pangani kulia Zainabu Abdallah Issa na anayefuatia ni Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora Kamishna  Msaidizi wa Uhifadhi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadani Grace Lobora kushoto akisisitiza  jambo wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Blasius Chatanda kuhusu namna walivyofanikisha ukamataji

LATRA YATANGAZA NAUALI MPYA YA TRENI MOSHI-ARUSHA

Image
   Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imetangaza nauli za treni ya abiria itakayofanya safari zake kutoka Moshi mjini hadi Arusha na kurudi Moshi. Akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Arusha leo tarehe 29 Septemba, 2020, Mkurugenzi Mkuu wa LATRA Gilliard Ngewe amesema nauli hizo zimetangazwa kufuatia Shirika la Reli Nchini (TRC) kuwasilisha maombi ya nauli hizo, ambapo LATRA ilifanya mikutano ya kupokea maoni ya wadau, kisha kufanya uchambuzi wa maoni hayo pamoja na kuchambua mchanganuo uliowasilishwa na TRC.  Kwa mujibu wa kifungu cha 21 (2) (b) cha Sheria ya LATRA namba 3 ya 2019, baada ya mchakato wa uchambuzi kukamilika, Bodi ya Wakurugenzi ya LATRA imeidhinisha nauli hizo na kuainisha nauli zitakazotumika kwa usafiri wa treni ndani ya mikoa hiyo na nje ya mikoa kama inavyoonekana katika jedwali. Nauli zilizoidhinishwa na LATRA zikionesha mchanganuo wa vituo vya ndani nan je ya mikoa husika KUTOKA MOSHI KWENDA Umbali (KM) NAULI KWA MADARAJA HUSIKA (SHS): Daraja la tat

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO SEPTEMBA 30, 2020

Image
 

RAIS DKT.SHEIN AFUNGUA JENGO LA ABIRIA TERMINAL III ZANZIBAR

Image
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia ikiwa ni ishara ya Ufunguzi wa jengo la Abiria la (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,hafla iliyofanyika leo Kisauni Wilaya ya Magharibi (B) Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja (kulia kwa Rais) Mgombe wa Urais Zanzibar Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi),  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(wa pili kushoto) akikata utepe kuashiria  Ufunguzi wa jengo la Abiria la (Terminal III) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar,hafla iliyofanyika leo Kisauni Wilaya ya Magharibi (B) Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja (kulia) Mgombe wa Urais Zanzibar Dk.Hussein Ali Hassan Mwinyi)akifuatiwa na Makamo wa Pili wa Rais  wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi na Balozi Mdogo wa China aliyepo Zanzibar Xe Xiaowu . Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Waziri wa Ujenzi,Usafirishaji na M

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE SEPTEMBA 29, 2020

Image