Posts

Showing posts from January, 2021

WILAYA ITAKAYOKUMBWA NA NJAA DC ATAONDOKA: MAGUFULI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wa Manyoni mjini mkoani Singida wakati akiondoka mara baada ya kuwahutubia leo tarehe 31 Januari 2021. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wa Manyoni mjini mkoani Singida wakati akiondoka mara baada ya kuwahutubia leo tarehe 31 Januari 2021. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na watoto mara baada ya kuwahutubia wananchi wa Manyoni mjini mkoani Singida Januari 31, 2021. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na watoto mara baada ya kuwahutubia wananchi wa Manyoni mjini mkoani Singida Januari 31, 2021.(Picha na IKULU). NA MWANDISHI MAALUM. RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewahimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii kwani kuba kila dalili ya uwepo wa uhaba wa chakula Duniani kwa vile mataifa mengi wame

NAIBU WAZIRI MABULA AWABANA WATENDAJI SEKTA YA ARDHI KUONGEZA KASI UTOAJI HATI

Image
  Na  Munir Shemweta, WANMM, MARA   Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka Watendaji wote wa sekta ya ardhi katika halmashauri kushiriki zoezi la kuandaa hati za ardhi ili kuongeza kasi ya utoaji hati katika maeneo mbalimbali nchini.   Dkt Mabula ametoa agizo hilo mwishoni mwa wiki alipozungumza na wataalamu wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Mara akiwa katika ziara ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi na kuhamasisha ukusanyaji maduhuli ya Serikali kupitia kodi ya pango la ardhi katika mkoa huo.   Alisema, baadhi ya halmashauri nchini zimekuwa na kasi ndogo ya uandaaji hati za ardhi kwa kisingizio cha kuwa na wataalamu wachache wa kuandaa hati wakati halmashauri hizo zina wataalamu mbalimbali wa sekta hiyo na kutolea mfano wataalamu wa Mipango Miji, Warasimu Ramani, Wapimaji na  Wathamani aliowaeleza wamekuwa wakisoma chuo kinachotoa taaluma ya sekta ya ardhi.   Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliongeza kwa kusema kuwa,

URASIMISHAJI WAWEZESHA WANANCHI NJOMVE KUKOPA TZS BILIONI 3.1

Image
Na Mwandishi  Wetu- Njombe WAFANYABIASHARA na wakulima waliorasimisha biashara, ardhi na makazi yao katika Halamashauri ya Mji wa Njombe, wametumia hati za hakimili za kimila kukopa zaidi ya Shilingi bilioni 3.1 katika taasisi za fedha zikiwemo benki za NBC, CRDB, NMB na Benki ya Posta kati ya mwaka 2018 na 2020. Akizungumza wakati wa ziara ya Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA) kutembea wanufaika wa Mpango huo leo Januari 29, 2021, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Balozi (Mstaafu) Daniel Ole Njoolay, amesema Halmashauri ya Mji wa Njombe ni mfano bora wa kuigwa na halmashauri nyingine kwa namna ilivyotekeleza kikamilifu dhana ya urasimishaji hali iliyowawezesha wananchi kupata mikopo katika taasisi za fedha baada ya urasimishaji tasilimali zao na kupata hati za hakimiliki za kimila. “Viwanja zaidi ya elfu 10 vimepimwa hapa katika Mji wa Njombe na hii ni ishara kuwa urasimishaji umekuwa na matokeo chanya, hivyo nawapongeza wan

WAZIRI MHAGAMA AZINDUA MPANGO KAZI WA KUSIKILIZA NA KUSHUGHULIKIA MALALAMIKO YA WADAU KATIKA SEKTA YA KAZI NA AJIRA

Image
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.  Jenista Mhagama akikata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Mpango Kazi wa Kusikiliza na Kushughulikia Malalamiko ya Wadau katika sekta ya kazi na ajira uliofanyika ukumbi wa mikutano wa NSSF mkoani Morogoro Januari 29, 2021, kulia kwake ni rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi, Tumaini Nyamhokya, kushoto kwake ni Mwakilishi wa ILO Bw. Maridadi Phanuel, wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Loata Sanare, wa pili kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Bw. Andrew Massawe na wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Dkt. Aggrey Mlimuka. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe.  Jenista Mhagama akihutubia wakati wa uzinduzi wa Mpango Kazi wa Kusikiliza na Kushughulikia Malalamiko ya Wadau katika sekta ya kazi na ajira uliofanyika mkoani Morogoro, Januari 29, 2021. Waziri

KATIBU TAWALA MKOA WA SINGIDA ATOA MAAGIZO MAZITO KWA SEKTA YA ELIMU

Image
Katibu Tawala Mkoa wa Singida  Dk. Angelina Lutambi, akizungumza na wakuu wa shule za sekondari na maafisa elimu kata katika kikao kazi kilichofanyika jana kwenye ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari Mwenge mkoani hapa. Afisa Elimu Mkoa wa Singida, Nelasi Mulungu,   akizungumza kwenye kikao hicho. Kikao kikiendelea.   Na Mwandishi Wetu, Singida KATIBU Tawala Mkoa wa Singida  Dk. Angelina Lutambi amewataka wakuu wa shule na maafisa elimu kata mkoani hapa kufanya kazi kwa bidii ili kubadilisha mitazamo ya jamii zinazozunguka shule zao.  Lutambi aliyasema hayo jana katika kikao kazi cha wakuu wa shule zote za Sekondari na maafisa elimu kata kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Shule ya Sekondari Mwenge ambacho kililenga kufanya tathimini ya matokeo ya kidato cha nne na kidato cha pili Mwaka 2020. Katibu Tawala huyo alisema wakuu wa shule ni  chachu ya mabadiliko kwenye jamii inayowazunguka ,wanafunzi wanapomaliza shule na kurudi kwa jamiii hivyo kama jamii haijabadilika ni isha

MIGODI YA BUZWAGI NA BULYANHULU YALIPA USHURU SH. BIL 2.3 MANISPAA YA KAHAMA NA MSALALA DC

Image
  Meneja Mkuu wa Migodi ya Bulyanhulu na Buzwagi, Benedict Busunzu (wa tatu kulia) akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha ( wa pili kushoto) hundi ya shilingi 744,929,725.78  kwa ajili ya Halmashauri ya Msalala ambazo ni malipo ya ushuru kwa ajili ya maendeleo leo Jumamosi Januari 30,2021. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala, Simon Berege. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

DKT.KIJAZI AWATAKA WATUMISHI KUFANYA MAZOEZI

Image
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Allan Kijazi akimvisha medali Afisa Rasilimaliwatu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Bi. Stella Msuya ikiwa ni moja ya pongezi ya kushiriki bonanza la watumishi lililoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii lililofanyika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma leo. Washiriki wa mchezo wa mbio za magunia wakichuana wakati wa bonanza la watumishi lililoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii lililofanyika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma leo. Na Happiness Shayo –Dodoma Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Allan Kijazi amewataka watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii kuwa na utaratibu wa kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zao na kujenga mshikamano na upendo katika maeneo yao ya kazi. Dkt. Kijazi ametoa wito huo wakati wa bonanza la watumishi lililoandaliwa na Wizara ya Maliasili na Utalii lililofanyika leo katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Mazoezi iwe ni sehemu ya maisha yetu na pia iwe ni sehemu ya kazi

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI JANUARI 31, 2021

Image