Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM, Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na Wajumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM wakati wakiimba Wimbo wa Chama kabla ya kuongoza Kikao hicho cha Kamati Kuu jijini Dodoma leo tarehe 31 Agosti 2020
8/31/2020
KATIBU MKUU KILIMO GERALD KUSAYA AJADILI NAMNA YA KUINUA KILIMO CHA MBOGA NA MATUNDA (HORTICULTURE), ARUSHA
KATIBU Mkuu Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Kusaya (pichani kushoto) amefanya kikao na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Kuendeleza Mazao ya Bustani (TAHA) Dkt.Jacquline Mkindi jijini Arusha cha kujadili mikakati na mambo mbalimbali yahusuyo maendeleo ya tasnia ya mboga mboga na matunda (horticulture) nchini.
Sambamba
na kikao hicho, Katibu Mkuu Kusaya ameikabidhi TAHA zawadi ya Ramani ya
Tanzania inayoonesha viwango vya pH na Afya ya Udongo kwa nchi nzima na imepokelewa
na Mtendaji Mkuu wa TAHA, Dr. Jacqueline Mkindi.
Kusaya ameitaka TAHA kuendelea kuelimisha wakulima wengi zaidi kuzingatia kilimo cha kitaalam kwa kutambua aina ya udongo unaofaa kwa zao husika na mbolea gani itumike, ndio maana amekabidhi ramani hiyo kuwezesha utambuzi wa maeneo yanayofaa kwa mazao ya horticulture nchini.
"Tunaendelea kuishukuru Serikali kupitia Wizara ya Kilimo kwa ushirikiano mkubwa na wa muda wote inaotupatia wadau wa sekta ya horticulture " Dr Mkindi alisema.
Katibu Mkuu Kusaya alikuwa mkoani Arusha Kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kutembelea taasisi zinazojihusisha na kilimo vikiwemo viwanda vya kuzalisha mbolea kwa matumizi ya kilimo.
MSITU WA MINYUGHE ULIOPO IKUNGI MKOANI SINGIDA UPO HATARINI KUTOWEKA
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo, Edward Mpogolo (katikati) na wajumbe wa kamati hiyo na viongozi wa Kata ya Mwaru wakiangalia mkaa uliotelekezwa na wavamizi katika msitu huo.Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo, Edward Mpogolo (katikati) akiwaonesha wajumbe wa kamati hiyo mkaa uliotaifishwa na Serikali baada ya kutelekezwa na wavamizi katika Msitu wa Minyughe wilayani humo mwishoni mwa wiki wakati akikagua msitu huo. Kulia ni Mshauri wa Jeshi la Akiba wa wilaya hiyo, Capteni Gabriel Chabimia na Mkuu wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Ikungi, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Stephano Chaula.
Wajummbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Mwaru,wakimwaga mkaa uliohifadhiwa kwenye viroba na wavamizi wa msitu huo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida ambaye pia ni mkuu wa wilaya hiyo, Edward Mpogolo (kushoto) na wajumbe wa kamati hiyo na viongozi wa Kata ya Mwaru wakiangalia mkaa uliotelekezwa na wavamizi katika msitu huo.
WAZIRI UMMY ASHIRIKI HARAMBEE KANISA LA ANGLIKANA CHUMBAGENI TANGA,ATOA NENO KWA VIONGOZI WA DINI
Canon
Rev Chistopher Kiango ambaye ni Kasisi kiongozi wa Kanisa la Anglikana
Dayosisi ya Tanga akizungumza wakati wa harambee hiyo |
MKUU wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa akizungumza wakati wa halfa hiyo |
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akipokea mchango wa mtoto Nicolaus Galula wakati wa harambee hiyo
MENEJA wa Hotel ya Tanga Beach ya Jijini Tanga Joseph Ngoyo akizungumza jambo wakati wa harambee mara baada ya kukabidhi mchango wake kwa niaba ya familia yake
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu kushoto akipokea mchango kutoka kwa Catherine Kitandula wakati wa harambee hiyo |
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewataka viongozi wa dini kote nchini kuendelea kuliombea Taifa amani, umoja na mshikamano kuelekea uchaguzi mkuu.
Ummy aliyasema hayo leo wakati alipoongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Tanga Mtaa wa Mtakatifu Augustino wa Hippo Chumbageni Tanga.
Katika harambee hiyo walifanikiwa kukusanya fedha taslimu milioni 13.7 papo hapo na ahadi ikiwa ni milioni 47.2.huku mwisho wa kukusanya michango hiyo ikiwa ni Septemba 20 mwaka huu.
Katika harambee hiyo ilihudhuriwa na Mkuu wa wilaya ya Tanga Thobias Mwilapwa na viongozi wa dini wakiwemo waumini huku kwaya mbalimbali zikitumbuikza
“Lakini pia tunawashukuru viongozi wa dini kwa jinsi walivyotuunga mkono kwa sala za kila siku katika mapambano dhidi ya Corona na mungu akatuepusha na janga hili hivyo niwaombe hata wakati huu nchi ikielekea kwenye uchaguzi mkuu tuendelee kuiombea nchi”Alisema Waziri Ummy
“Nimekuwa nikipata ujumbe kutoka kwa mawaziri wa nchi nyengine Afrika tumefanya kitu gani mpaka hakuna Corona nisema kwamba ugonjwa huo umetoweka kutokana na Mungu ameipenda Tanzania”.
Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi Katibu wa Kanisa hilo Cyprian Mtweve alisema lengo la harambee ya leo katika kuadhimisha sikukuu ya Mt.Agustino wa Hippo ni kupata kiasi cha sh.milioni 125 kwa ajili ya kuezeka kanisa.
Alisema wanaamini kiasi hicho sio kikubwa kwa Mungu cha kushindwa kupatikana huku wakimshukuru mgeni rasmi kuwaongozea zoezi la harambee hiyo na kushiriki kwa moyo na kwa ukamilifu.
Aidha alisema upanuzi wa jengo la kanisa hilo umekuwa ukifanywa kwa kulirefusha kwa kiwango ambacho mawasiliano baina ya kasisi anayeongoza ibada madhabahuni na waumini wanaokaa viti vya mwishoni nyuma ya kanisa yanakuwa hafifu sababu ya umbali.
“Jengo hili limejengwa kwa kutumia teknologia ya zamani isiyohimili uwekwaji wa mifumo mbalimbali ya kisasa ikiwemo ile itakayoboresha ibada”Alisema
Miongoni mwa viongozi ambao wamechangia kwenye harambee hiyo ni Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi na Profesa Palamagamba Kabudi wakiwemo wakuu wa wilaya .
8/30/2020
MAALIM SEIF SHARIF HAMAD ACHUKUA FOMU ZA KUWANIA URAIS WA ZANZIBAR KUTOKA ZEC
WALIMU WA HEDHI RUKWA WAJA NA MUAROBAINI WA TAULO ZA KIKE
Kaimu Katibu
Tawala Mkoa wa Rukwa Winnie Kijazi akitoa nasaha wakati wa kufungua mafunzo ya
Hedhi Salama kwa baadhi ya waalimu wa Shule za Msingi Mkoani Rukwa.
Baadhi ya
Waalimu kutoka halmashauri ya wilaya ya Kalambo wakionesha vyeti vyao
baada ya kupatiwa mafunzo ya Hedhi Salama wakiwa katika picha ya pamoja na
Mratibu wa Mradi wa SWASH Mkoa Matinda Mwinuka (aliyechuchumaa kushoto) na
Mwezeshaji Jesca Lwiza (aliyechuchumaa kulia)
NA MWANDISHI WETU, RUKWA
UMOJA wa Walimu
wa Hedhi Salama kwa shule za msingi mkoani Rukwa wamepania kuhakikisha
wanapunguza fikra potofu kuhusu suala la hedhi kwa wasichana wanaovunja ungo
pamoja na kukomesha utoro kwa wananfunzi wa kike wanaoona aibu kuhudhuria shule
pindi wanapopata hedhi kwa kutoa elimu sahihi ya suala la hedhi mashuleni.
Azma hiyo imekuja baada ya waalimu hao kupewa mafunzo yanayohusu
namna ya kutengeneza taulo za kike (pedi) kwa kutumia aina mbalimbali za vitambaa pamoja na
kukabiliana na wanafunzi wanaoona aibu ama fedheha pindi wanapopata hedhi
wakiwa shuleni na hivyo kuwarahisishia Maisha yao wanapokuwa shuleni huku
wakiwahamasisha kuendelea kuhudhuria shuleni ili wasiachwe nyuma kimasomo.
Aida Mwanauta ni mwalimu wa Hedhi Salama kutoka Shule ya Msingi
Ilambila, Wilayani Kalambo, aliishukuru serikali kwa kuwapatia mafunzo hayo
muhimu kwani changamoto wanazokumbana nazo ni nyingi na mafunzo hayo
yamamsaidia kujua namna ya kuwasaidia wasichana hao pindi wanapokuwa katika
hedhi kutokana na wanafunzi wengi kutokuwa na ufahamu wa kutosha juu ya namna
ya kukabilina na hali hiyo.
“Kuna mwanafunzi anakuja shuleni hajui ni namna gani anaweza
akajistiri, mwingine anatoka nje anakimbia, huko nje anachukua hata makaratasi,
majani kwaajili ya kujistiri ambayo inaweza ikamletea matatizo baadaye, kwahiyo
katika semina hii tumejifunza mambo mbalimbali, tumejua ni mambo gani ambayo
unaweza ukamfundisha mtoto, akajua jinsi ya kujihifadhi akiwa shuleni na
hatimae akawa anasoma na asiwe mtoro shuleni, na kujiona ni sawa na wengine,”
Alisema.
Nae, Mwalimu Victoria Tanganyika alisema kuwa mafunzo hayo
yamemsaidia kujua vifaa vinavyotumika kutengeneza pedi za kike na namna ya
kuvitekeza pamoja na kujua mazungumzo anayotakiwa kufanya na matoto ili
kumshawishi aweze kujiamini na kushiriki katika michezo na masomo katika
mazingira ya shule.
Kwa upande wake Mwalimu Clifonsia Remidio ameiomba serikali
kuendelea kutumia njia mbalimbali za vipeperushi na kutoa semina kwa waalimu
wengi zaidi wanaotoa huduma ya hedhi salama mashuleni ili kuweza kuwasaidia
wanafunzi wa kike ambao wamekuwa wakipata tabu kusoma wanapokuwa katika kipindi
cha hedhi.
“kuna vitu vingi tulikuwa hatuvifahamu, kuna wakati mwingine
hata kama mimi mwalimu nimeshasoma lakini bado nitaona aibu kuenenda
kumuelekeza yule mwanafunzi, lakini ameshatuelekeza mwezeshaji tumepata mwanga
mzuri pia nimefurahi kwasababu hili suala linashirikisha pande zote mbili, upande
wa waalimu wa kiume na upande wa waalimu wa kike pia kwamba tuwasaidie Watoto
wanaposikia ile hali ya mabadiliko ya mwili,”Alisema.
Aidha, Mwezeshaji wa mafunzo hayo ya Hedhi Salama, Mwalimu Jesca
Lwiza alisema kuwa mafunzo hayo yanalenga kutoa elimu ya hedhi salama kwa
wanafunzi ili kupunguza utoro mashuleni na kuongeza kuwa wanategemea kuona
mabadiliko makubwa ya mahudhurio shule kwa shule ambazo waalimu wake
wamehudhuria mafunzo hayo.
“Kuna ukimya ambao upo katika masuala ya hedhi salama, wanafunzi
wanakosa elimu sahihi, lakini pia wanakosa namna ya kujiamini wanapokuwa katika
masomo na wakati mwingine shuleni hakuna vyumba maalum vya kujihifadhi
wanapokuwa katika hedhi, kwa kulitambua hilo tumeona serikali namna ilivyoweza
kuwezesha kwa kuwapa mafunzo waalimu lakini imeweza kuboresha miundombinu
iliyopo mashuleni kwa kuweka vyumba hivyo,” Alisema.
Wakati akifungua mafunzo hayo Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa
Winnie Kijazi alisisitiza kuwa tafiti zilizofanyika zimeonesha kuwa wasichana
wengi hawana taarifa za awali kuhusu hedhi za pia walipata hedhi ya kwanza
pasipo kuwa na uelewa wa kutosha kuhusu mabadiliko ya miili yao hivyo mafunzo
hayo yamelenga kuwajengea uwezo waalimu kufikisha elimu katika shule.
“Tafiti zinaonesha kuwa bado kuna fikra zisizo sahihi kuhusu
masuala ya hedhi hususani miiko na unyanyapaa inayosababisha wasichana na
wanawake kushindwa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo na kijamii
na wanafunzi wa kike kukosa baadhi ya siku za masomo na wengine kuacha shule
wanapokuwa kwenye hedhi. Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
kulitambua hilo imeweka jitihada kuhakikisha kuwa fursa za elimu zinapatikana
kwa makundi yote,” Alieleza.
Halikadhalika mratibu wa mradi wa School Water Sanitation and
Hygiene (SWASH) Mwalimu Matinda Mwinuka aliwaasa waalimu kuhakikisha shule
zinakuwa na vyombo maalum kwaajili ya walemavu pamoja na vyumba kwaajili ya
wasichana kubadili pedi za hedhi pindi wanapokuwa katika hali hiyo nasio
kutumia vyoo vya kawaida ambavyo havina mazingira mazuri ya kubadilishia vifaa
vyao.
“Kuna shule moja fundi kaweka shule maalum, anasema kuwa kile
ndio chumba maalum, walemavu wataingia humo humo, hedhi salama wataingia humo
humo, ametoboa tundu na kuweka ‘pipe’ anasema Watoto wa kike wakishaingia humu
ndimo watatumbukiza vile vitu vyao yaani ni vitu vya ajabu kwakweli.”
Mradi huo unatekelezwa katika halmashauri tatu za Mkoa wa Rukwa
kwa muda wa miaka minne huku kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Mkoa ulipewa kiasi
cha Shilingi 578,486,955.63/= kwaajili ya utekelezaji wa mradi huo
unaofadhiliwa na Benki ya Dunia na kutekelezwa katika mikoa 17 na Halmashauri
86 za Tanzania Bara ukiwa na lengo la kuboresha mazingira ya kufundishia,
kujenga vyoo bora shuleni na kuweka miundombinu ya maji safi na salama.
KATIBU MKUU KILIMO AKABIDHI GARI BODI YA PARETO
Mkulima wa mbegu bora za mahindi Bw.Aron Nguma (kulia) wa Arusha
akikabidhi mahindi yaliyokauka ya mbegu kwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo
Bw.Gerald Kusaya leo alipotembelea shamba hilo Ngaramtoni kukagua hali ya
uzalishaji mbegu za mahindi,maharage na ngano .Shamba hilo linamilikiwa na
Wakala wa mbegu Nchini (ASA)
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya (kushoto) akikabidhi
funguo za gari Toyota H/Top kwa Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Pareto Lucas Ayo jijini Arusha. Gari hiyo imekabidhiwa ili kusaidia bodi kuhamasisha wakulima
wengi kulima zao la pareto nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pareto Lucas Ayo akionyesha funguo za
gari mara baada ya kukabidhiwa toka kwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald
Kusaya (kushoto). Hafla hiyo ilifanyika jijini Arusha.
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (katikati) akitoa
maelekezo kwa dereva wa Bodi ya Pareto Venance Haule (kushoto) leo
alipokabidhi gari kwa bodi hiyo jijini Arusha .
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (wa saba toka kushoto)
akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa wizara na taasisi zake zilizopo
Arusha alipokabidhi gari kwa Bodi ya Pareto nchini.