Posts

Showing posts from March, 2022

KAMATI YA BUNGE YA UWEKEZAJI WA MITAJI YA UMMA YATEMBELEA KIWANDA CHA NYAMA CHA NGURU HILLS NA KURIDHISHWA NA UWEKEZAJI WA PSSSF KWENYE MRADI HUO

Image
NA MWANDISHI MAALUM, MOROGORO. KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma, ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Jerry Silaa, imeridhishwa na uwekezaji uliofanywa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF)  kwenye Mradi wa Uendelezaji wa shamba (Rachi) ya kunenepesha Mifugo na Machinjio ya kisasa wa Nguru Hills Ranch ulioko Wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro. Kufuatia kuridhishwa huko   Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Jerry Silaa alitoa maagizo matatu kwa Bodi ya Wadhamini ya PSSSF kuhakikisha inaendelea kusimamia mkataba wa uwekezaji katika machinjio hayo ya Nguru Hills kwa kushirikiana na wawekezaji wenza kwa lengo la kuhakikisha uzalishaji unaanza haraka iwezekanavyo na kupata tija iliyokusudiwa. Pia Bodi ya PSSSF imeagizwa kuongeza kipengele kwenye makubaliano ya ubia na wawekezaji wenza kwenye machinjio hayo ya kukiuzia Ngozi kiwanda cha Bidhaa za Ngozi cha Kilimanjaro Leather Industry Company Limited (KLIC) ambacho PSSSF imewekeza na hivyo kiwanda cha KL

MWENYEKITI WA CCM, RAIS SAMIA, AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU NA HALMASHAURI KUU, ATEMBELEA UKUMBI WA MKUTANO MKUU

Image
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika leo tarehe 31 Machi, 2022 katika Makao Makuu ya Chama White House Jijini Dodom a Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika leo tarehe 31 Machi, 2022 katika Makao Makuu ya Chama White House Jijini Dodom Wajumbe wa NEC Wajumbe wa NEC Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipata maelezo kutoka kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Shaka Hamdu Shaka kuhusu matayarisho ya Mkutano Mkuu Maalum wa CCM unaotarajiwa kufanyika kesho alipotembelea ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma leo tarehe 31 Machi, 2022.  

PROFESA NDALICHAKO ASHIRIKI KWENYE MKUTANO WA MAWAZIRI WA KAZI NA AJIRA WA SADC MJINI LILONGWE

Image
  NA MWANDISHI MAALUM, LILONGWE WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira, na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako ameshiriki Mkutano wa Mawaziri wa Kazi na Ajira wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) jijini Lilongwe nchini Malawi. Katika mkutano huo uliofanyika Machi 30, 2022, Profesa Ndalichako alifuatana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma, Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda na Maafisa wengine wa Serikali. Aidha jumla ya ajenda 13 zilijadiliwa na Mawaziri hao ikiwa ni pamoja na kuweka Miongozo mbalimbali ya usimamizi wa Hifadhi ya Jamii,  Miongozo ya ukuzaji wa fursa za ajira na viwango vya kazi kwa nchi Wanachama na miongozo ya usimamizi mzuri wa masuala ya usalama na afya mahali pa kazi. WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira, na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako (katikati) pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. John Mduma (wanne k

KAMATI YA MIUNDOMBINU YAPITISHA MAKADIRIO YA BAJETI YA SEKTA YA UJENZI KWA MWAKA 2022/2023

Image
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, akifafanua kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, kuhusu makadirio ya bajeti ya Sekta ya Ujenzi kwa mwaka 2022/2023, jijini Dodoma. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso akisisitiza jambo kwa Uongozi wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, wakati Wizara hiyo ilipowasilisha Makadirio ya bajeti kwa mwaka 2022/2023, jijini Dodoma. Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mfuko wa Bababara (RFB), Eliud Nyauhenga akitoa ufafanuzi kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, kuhusu matumizi ya fedha za mfuko huo wakati sekta hiyo ilipowasilisha makadirio ya bajeti ya Sekta ya Ujenzi kwa mwaka 2022/2023, jijini Dodoma. Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi (Ujenzi), Mhandisi Godfrey Kasekenya., akifafanua kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, kuhusu ujenzi wa miudombinu ya barabara, vivuko na majengo wakati sekya hiyo ilipowasilisha makadirio ya bajeti ya Sekta ya Ujenzi kwa mwaka 2022/2023, jijini Dodoma. Kaimu

KAMATI YA BUNGE YA PAC YATEMBELEA BOHARI KUU YA DAWA MSD

Image
 Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imetembelea Bohari ya Dawa (MSD) na kukagua Kiwanda cha Kutengeneza Barakoa na Kiwanda cha Dawa cha Keko vyote vya jijini Dar es Salam.

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI MACHI 31, 2022

Image
 

WAZIRI UMMY ATAKA WATUMISHI WA AFYA KUBADILI FIKRA KATIKA UTENDAJI WA KAZI

Image
 Na WAF – Dodoma Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka watumishi wa umma katika sekta ya afya kubadili fikra za utendaji kazi na kuwa wabunifu katika kutatua changamoto ili kuongeza chachu ya kufikia malengo na kutoa huduma bora kwa wananchi. Waziri Ummy amesema hayo leo wakati akifungua mkutano wa baraza kuu la wafanyakazi wa Wizara ya afya,hospitali za rufaa za mikoa pamoja na taasisi zilizo chini yake uliofanyika jijini Dodoma. “Nitoe rai kwa watumishi wote kubadili fikra zetu katika utendaji na tunatakiwa kufanya kazi kwa bidii tukilenga kufikia malengo na mafanikio tuliyojiwekea. Kila mmoja katika nafasi yake awe mbunifu katika kutatua changamoto zinazomkabili na hatimaye kutoa huduma bora”. Amesema Waziri Ummy. Waziri Ummy amesema katika kipindi cha mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan akiwa madarakani ametoa Shilingi bilioni 891.5 kwa ajili ya kuboresha miundombinu pamoja na huduma za afya hivyo amewataka watumishi watumie fursa zinazopatikana zikawe chachu za kupata maf