Posts

Showing posts from November, 2020

WABUNGE WAWILI WALIOTEULIWA NA MHE. RAIS WAAPISHWA BUNGENI JIJINI DODOMA

Image
Wabunge wa Kuteuliwa na Mheshimiwa Rais, Mhe. Riziki Lulida na Mhe. Humphrey Polepole wakiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Bunge Mhes. Job Ndugai na Katibu wa Bunge Ndg. Stephen Kagaigai mara ya kuapishwa kwenye viwanja vya Bunge hii leo Jijini Dodoma.  (Picha na Ofisi ya Bunge) Mbunge wa Kuteuliwa na Mheshimiwa Rais, Mhe. Riziki Lulida akila kiapo mbele ya Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai katika viwanja vya Bunge hii leo Jijini Dodoma.  (Picha na Ofisi ya Bunge) Mbunge wa Kuteuliwa na Mheshimiwa Rais, Mhe. Humphrey Polepole akila kiapo mbele ya Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai katika viwanja vya Bunge hii leo Jijini Dodoma.  (P icha na Ofisi ya Bunge)  

RAIS DK.MWINYI AHUTUBIA SEMINA YA VIONGOZI WAANDAMIZI NA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI ILIOANDALIWA NA BENKI YA CRDB HOTELI YA VERDE ZANZIBAR

Image
  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akihutubia katika hafla ya Semina Maalum ilioandaliwa na Benki ya CRDB Tanzania kwa Viongozi Waandamizi na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, iliofanyika  katika viwanja vya Marina Hoteli ya Verde Mtoni Jijini Zanzibar jana usiku 28/11/2020. MAKAMU Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB Tanzania Profesa Neema Mori  akizungumza na kutowa neno la shukrani kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani)  baada ya kumalizika kwa hafla hiyo ya Semina kwa Viongozi Waandamizi na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, iliofanyika katika viwanja vya Marina Hoteli ya Verde Mtoni Jijini Zanzibar jana usiku 28/11/2020. WASANII wa Kikundi cha Siti Band wakitowa burudani wakati wa hafla ya Semina ya Viongozi Waandamizi na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar iliofanyika katika viwanja vya Marina Hoteli ya Verde Mtoni Jijini Zanzibar jan

JENERALI MABEYO ATUNUKIWA NISHANI MAALUM YA MLIMA KILIMANJARO

Image
Chuo Kikuu cha Iringa (zamani Tumaini University) kimemtunukia Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Salvatory Venance Mabeyo (pichani juu) Nishani Maalum ya Mlima Kilimanjaro (University of Iringa Miunt Kilimanjaro Award) ambayo hutolewa kwa Viongozi wa juu Serikalini ambao wametoa mchango wa kutukuka kwa Chuo au Tasnia ya Elimu kwa ujumla. Tukio hilo limefanyika wakati wa Mahafali ya 23 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika "campus" ya Chuo Mjini Iringa tarehe 28 Nov 20. Mwingine aliyetunukiwa Nishani hiyo Maalum ya juu wakati wa Mahafali hiyo ni Mkurugenzi wa TAKUKURU, Brigedia jenerali John Julius Mbungo. Kwa mara ya kwanza Nishani hiyo ilitunukiwa kwa aliyekuwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Benjamin William Mkapa na Mkewe Mama Anna Mkapa wakati wa Mahafali ya 22 ya Chuo hicho mwaka 2019. Jenerali Salvatory Venance Mabeyo  Brigedia jenerali John Julius Mbungo  

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU NOVEMBA 30, 2020

Image
 

TANESCO MSHINDI WA JUMLA MASHINDANO YA SHIMMUTA

Image
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeibuka mshindi wa jumla katika mashindano ya SHIMMUTA baada ya kunyakua vikombe tisa na kuibuka kidedea katika mashindano hayo ya michezo ya mwaka 2020, yanayofanyika Mkoani Tanga. Matokeo hayo yanaifanya TANESCO kuwa mshindi wa jumla katika mashindano ya SHIMMUTA mwaka huu yaliyomalizika Mkoani Tanga. Michezo ambayo TANESCO imeibuka na ubingwa ni wavu wanaume na wanawake, kikapu wanaume na wanawake. Aidha, TANESCO imekuwa mshindi wa pili mchezo wa pete. Hii ni mara ya nne mfululizo timu ya kikapu wanaume wanakuwa washindi, na mara ya pili mfululizo kwa timu ya wavu wanaume inaibuka na ushindi.  Kwa upande wa michezo ya jadi TANESCO imeshinda mchezo wa bao wanawake, karata wanaume na mshindi wa pili bao kwa wanaume.  Mbali ya vikombe hivyo, TANESCO pia imepata medali saba ambapo Polycaps Ernest amekuwa mahindi wa tatu mbio za mita 100 na mita 200, Kulwa Mangala mshindi wa pili mita 1500, Grace Moshi mshindi wa pili mita 400 na 800, mshindi wa tatu