Posts

Showing posts from February, 2021

WAZIRI AWESO AAGIZA MKANDARASI KULIPWA FEDHA

Image
  Mh.Waziri akimtwisha ndoo mmoja wa wananchi wa kijiji cha kashangu Halmashauri ya Itigi mara baada ya kuzindua mradi huo. Waziri na watendaji wa RUWASA pamoja na Viongozi wengine wa Wilaya ya Manyoni wakipanda juu ya Tanki la maji linalohudumiwa na mradi wa kintinku. iongozi akiwemo Pius Chaya katikati wakiongozana na Mh.Waziri kutoka kwenye chanzo cha maji katika mradi wa kintinku Wilayani Manyoni.. Waziri akiteta jambo na Meneja wa RUWASA Mhandisi Lucas Said. Mh.Waziri akizungumza mara baada ya kukagua chanzo cha mradi wa kintinku Wilayani Manyoni.   Na Mwandishi wetu,Singida. WAZIRI wa Maji,  Jumaa Aweso ametoa siku saba kwa Meneja wa wakala wa maji na usafi wa Mazingira Vijijini na mijini (RUWASA) Mkoa wa Singida kumlipa Mkandarasi anayejenga mradi wa maji uliopo katika Kijiji cha Kintinku Wilayani Manyoni. Aweso alitoa kauli hiyo juzi wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja mkoani hapa ya kutembelea miradi pamoja na kuzungumza na wafanyakazi wa idara hiyo ya maji. Baada ya W

NAIBU WAZIRI GEKUL ATEMBELEA KAMPUNI YA TANGA FRESH NA MNADA WA NG’OMBE WA NDEREMA MKOANI TANGA

Image
  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul ( wanne kutoka kulia) akiangalia bidhaa mbalimbali za maziwa zinazozalishwa na Kampuni ya Tanga Fresh alipotembelea kukagua shughuli za Kiwanda hicho kilichopo Mkoani Tanga mapema leo. Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Ummy Mwalimu akimueleza jambo Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul (wapili kulia) walipokutana katika kikao cha Wavuvi na Naibu Waziri huyo kilichofanyika Mkoani Tanga mapema leo lengo la kikao hicho ni kusikiliza kero za Wavuvi wa Mkoani Tanga. Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul akikagua risiti aliyopewa mfanyabiashara aliyenunua Ng’ombe katika Mnada wa Nderema uliopo katika Halmashauri ya Mji, Handeni, Mkoani Tanga leo . Naibu Waziri alitembelea mnada huo kukagua shughuli zinazoendelea katika mnada huo.  Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul (katikati) akiangalia Ng’ombe waliopelekwa katika Mnada wa Nderema kwa ajili ya kuuzwa. Naibu Waziri alitembelea mnada huo uliopo

NAIBU WAZIRI MABULA AIBANA MANISPAA YA IRINGA

Image
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akimkabidhi hati ya umiliki wa ardhi Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini Jesca Msavatavangu wakati wa kikao kazi na watendaji wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki. Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akiwa katika picha ya pamoja na wananchi wa Iringa aliowakabidhi hati wakati wa kikao kazi na watendaji wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki.  (PICHA ZOTE NA MUNIR SHEMWETA) Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi katika kikao kazi wakati wa ziara yake ya siku moja katika mkoa wa Iringa mwishoni mwa wiki. Wa pili kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela Watendaji wa Sekta ya ardhi katika mkoa wa Iringa wakifuatilia maelezo ya Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula wakati wa kikao kazi kilichofanyika mkoani Iringa mwishoni mwa wiki

TAASISI TA UHASIBU SINGIDA YAZINDUA UMOJA WA WANAFUNZI WA FANI YA UNUNUZI NA UGAVI

Image
  Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania  (TIA) Tawi la Singida,  Dkt. James Mrema akisoma taarifa  wakati wa hafla ya kuzindua  rasmi umoja wa wanafunzi wanaochukua fani ya ununuzi na ugavi.  Mwenyekiti wa umoja wa wanafunzi wanaochukua fani ya ununuzi na ugavi,  Evarist Peter akisoma taarifa ya umoja huo. Mgeni  rasmi wa hafla ya kuzindua rasmi umoja wa wanafunzi wanaochukua fani ya ununuzi na ugavi  mkoani Singida,  Kaimu Afisa Vijana wa mkoa  huo, Frederick  Ndahani (katikati) akiwa na viongozi mbalimbali. Kulia ni mkuu wa Taasisi hiyo, Singida na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji  Bodi ya Ununuzi na Ugavi wa Taasisi hiyo nchini,  Godfred Mbanyi  wakifuatilia taarifa ya umoja wa wanafunzi wanaochukua fani ya ununuzi na ugavi. Mlezi wa umoja huo, Mhadhiri Msaidizi, Eliaichi Kyara, akifuatilia hafla hiyo. Mgeni rasmi akihutubia wanafunzi wanaochukua fani ya ununuzi na ugavi katika Taasisi hiyo ya Uhasibu Tawi la Singida. Mgeni rasmi Frederick  Ndahani (Wa pili kulia waliokaa) akiwa katika

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI FEBRUARI 28, 2021

Image
 

RAIS MAGUFULI, AMUAPISHA DKT. BASHIRU KAKURWA, KUWA KATIBU MKUU KIONGODI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Dkt. Bashiru Ally Kakurwa kuwa Balozi kabla ya kumuapisha tena kuwa Katibu Mkuu Kiongozi katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Februari 2021. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia Kamishna wa Maadili Jaji wa Mahakama ya Rufani, Sivangilwa Sikalaliwa Mwangesi kushoto alipokuwa akiongoza Kiapo cha Maadili kwa Viongozi wa Umma kwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa mara baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia Kamishna wa Maadili Jaji wa Mahakama ya Rufani, Sivangilwa Sikalaliwa Mwangesi kushoto alipokuwa akiongoza Kiapo cha Maadili kwa Viongozi wa Umma kwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Bashiru Ally Kakurwa mara baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Bashiru Ally Kak

RAIS MAGUFULI ASHIRIKI MKUTANO WA EAC KWA NJIA YA MTANDAO

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akishiriki  mkutano wa 21 wa kawaida wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unaofanyika leo tarehe 27 Februari, 2021 kwa njia ya mtandao.  

WANANCHI WA LUSHOTO WAISHUKURU SERIKALI KUWAREJESHA SHUGHULI ZA UZALISHAJI KATIKA KIWANDA CHA KUCHAKATA CHAI CHA MPONDE TEA ESTATE

Image
Na:  Mwandishi Wetu  – Lushoto Wananchi wa Lushoto katika Wilaya ya Bumbuli wameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwarejesha shughuli za uzalishaji katika kiwanda cha Mponde Tea Estate kilichopo kata ya Mponde, Wilayani Lushoto. Shukrani hizo wamezitoa wakati wa ziara ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama alipofanya ziara kiwanda hapo ikiwa ni maagizo yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majiliwa kuwa kiwanda hicho kianze kazi. Waziri Mhagama alieleza habari hizo njema za Serikali kwa wananchi hao kuwa hivi sasa ni kuwa Serikali yao imeamua kufufua kiwanda hicho ili wakulima wa chai waendelee kulima zao hilo la chai litakaloleta manufaa kwa wakazi wa Bumbuli na Wilaya ya Lushoto kwa Ujumla. “Serikali imeamua kurejesha matumaini kwa wakazi wa Bumbuli na Wilaya ya Lushoto kwa