RAIS SAMIA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI WA CCM KWA ASILIMIA 100%
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mhe. Samia Suluhu Hassan amechaguliwa na Mkutano Mkuu Maalim wa CCM kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa kura 1862, sawa na ASILIMIA 100. Mwenyekiti wa uchaguzi, SPIKA wa Bunge, Mhe. Job Ndugai ametangaza kwenye mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma leo APRILI 30, 2021. Uchaguzi huo unafuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho hayati Dkt. John Pombe Magufuli Machi 17, 2021. RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mhe. Samia Suluhu Hassan amechaguliwa na Mkutano Mkuu Maalim wa CCM kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa kura 1862, sawa na ASILIMIA 100. Mwenyekiti wa uchaguzi, SPIKA wa Bunge, Mhe. Job Ndugai ametangaza kwenye mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma leo APRILI 30, 2021. Uchaguzi huo unafuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho hayati Dkt. John Pombe Magufuli Machi 17, 2021