Posts

Showing posts from April, 2021

RAIS SAMIA ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI WA CCM KWA ASILIMIA 100%

Image
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mhe. Samia Suluhu Hassan amechaguliwa na Mkutano Mkuu Maalim wa CCM kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa kura 1862, sawa na ASILIMIA 100. Mwenyekiti wa uchaguzi, SPIKA wa Bunge, Mhe. Job Ndugai ametangaza kwenye mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma leo APRILI 30, 2021. Uchaguzi huo unafuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho hayati Dkt. John Pombe Magufuli Machi 17, 2021. RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mhe. Samia Suluhu Hassan amechaguliwa na Mkutano Mkuu Maalim wa CCM kuwa Mwenyekiti wa chama hicho kwa kura 1862, sawa na ASILIMIA 100. Mwenyekiti wa uchaguzi, SPIKA wa Bunge, Mhe. Job Ndugai ametangaza kwenye mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma leo APRILI 30, 2021. Uchaguzi huo unafuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho hayati Dkt. John Pombe Magufuli Machi 17, 2021

KAMPUNI YA GREEN MILE SAFARI YAREJESHEWA KITALU CHA LAKE NATRON EAST.

Image
Na Mwandishi Wetu - Dodoma Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro ametoa hukumu ya Kitalu cha uwindaji cha cha Lake Natron East kilichoko wilayani Longido mkoani Arusha na kuagiza kampuni ya Green Mile Safari irejeshewe leseni ya umiliki wa kitalu hicho iliyofutwa mwaka 2019. Akitoa maamuzi hayo Dkt. Ndumbaro amesema kitalu hicho kinarejeshwa kwa Kampuni hiyo hadi mwaka 2022 kufuatia kufanyika kwa maombi ya mapitio ya hukumu iliyoifanya Kampuni ya Green Mile ifutiwe umiliki wa kitalu hicho.  Aidha,Dkt. Ndumbaro amesema kufuatia uchambuzi uliofanyika kuhusu uamuzi wa kufutiwa umiliki wa kitalu cha Lake Natron – East, amejiridhisha kuwa malalamiko ya muomba mapitio ambayo ni kampuni ya Green Mile Safari yana msingi wa kisheria, na barua ya Mhe. Waziri ya kufuta umiliki wa kitalu haikuzingatia sheria na misingi ya utawala bora “Iandaliwe rasimu itakayotumiwa katika umilikishaji wa vitalu itakayoonesha masharti ya kufuata ‘Terms and condition’ za kufuatwa na wawekezaji wakati w

WAZIRI MCHENGERWA AONGOZA MKUTANO WA PILI WA MAWAZIRI WA NCHI WANACHAMA WA UMOJA WA AFRI

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati Na. 8 ya Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati Na. 8 inayoshughulika na masuala ya Utumishi wa Umma na Utawala akiongoza Mkutano wa Pili wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala Afrika kwa njia ya mtandao. Na Mary Mwakapenda-Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati Na.8 ya Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati Na. 8 inayoshughulika na masuala ya Utumishi wa Umma na Utawala leo ameongoza Mkutano wa Pili wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala Afrika kwa njia ya mtandao. Mhe. Mchengerwa ameongoza Mkutano huo ili kupitia na kuidhinisha ajenda mbalimbali zilizowasilishwa na Mkut

RAIS MWINYI AFUTURISHA DODOMA

Image
  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, leo amejumuika na mamia ya waislamu katika Iftari aliyoiandaa kwa ajili yao na kufanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Conversion centre, Jijini Dodoma,  Katika hafla hiyo viongozi mbali mbali wa Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) walihudhuria, akiwemo Rais mstaafu wa awamu ya saba ya Serikali ya Mapinduzi ya    Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, Mama Maryam Mwinyi na Mama Mwanamwema Shein .  Wengine ni pamoja na Makamo wa Pili Rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hemed Suleiman Abdalla, Mawaziri na Manaibu Mawaziri wa Serikali za SMZ na SMT, Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Said Ahmeid,    Wabunge, Wawakilishi, Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa pamoja na wageni mbali mbali.  Akitoa shukran kwa waalikwa, Dk. Mwinyi amesema amefarikijika sana na muitikio wa waumini hao, mbali na mialiko kutolewa katika kipindi kifupi.  Amesema ameamua kuandaa futari hiyo

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA APRILI 30, 2021

Image
 

UZINDUZI WA MKUTANO WA WADAU WA AFUA ZA VVU NA UKIMWI DODOMA

Image
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Protabas Katambi akikagua banda la Epidemic Control (EPIC) wakati wa Mkutano wa Mwaka wa wadau wanaotekeleza Afua za VVU na UKIMWI zinazowalenga wasichana Balehe na Wanawake Vijana unaofanyika leo April 29 jijini Dodoma. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Protabas Katambi akizungumza na Vijana wakati wa Mkutano wa Mwaka wa wadau wanaotekeleza Afua za VVU na UKIMWI zinazowalenga wasichana Balehe na Wanawake Vijana unaofanyika leo April 29  jijini Dodoma. Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Protabas Katambi akikagua banda la Amref Tanzania wakati wa Mkutano wa Mwaka wa wadau wanaotekeleza Afua za VVU na UKIMWI zinazowalenga wasichana Balehe na Wanawake Vijana unaofanyika  April 29  jijini Dodoma. Picha na Raymond Mushumbusi WAMJW Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Protabas Katambi akikagua banda la Tanzania Youth Alliance (TAYOA) wakati wa Mkutano wa Mwaka wa wadau wanaotekeleza Afua za VVU na UKIMWI zinazowalenga wasichana Balehe na Wanawake Vijana unaofany