Posts

Showing posts from July, 2023

TAASISI YA NEPHROPLUS KUSAIDIA UPATIKANAJI WA HUDUMA ZA KUSAFISHA DAMU KWA BEI NAFUU.

Image
HYDERABAD, INDIA Waziri wa afya Mhe. Ummy Mwalimu ameueleza uongozi wa Taasisi Nephroplus kuwekeza nchini ili kusaidia kupunguza gharama za kusafisha damu. Waziri Ummy amesema hayo wakati akihitimisha ziara yake nchini India kwa kutembelea taasisi ya Nephroplus. Waziri Ummy amesema Tanzania ina uhitaji mkubwa wa huduma za kuchuja damu ndio sababu ya Serikali imeamua kutafuta wadau wa kushirikiana nao kuwezesha kupunguza gharama ili kuwafikia watanzania wengi wenye uhitaji hasa kwa watu wasio na bima ya Afya. "Serikali iko tayari kuingia makubaliano ya ushirikiano na Taasisi hii kwa kuwa mapendekezo ya gharama zao ni za chini na hivyo kila mwananchi mwenye uhitaji ataweza kumudu gharama za huduma hiyo muhimu". Amesema Waziri Ummy. Ameongeza kuwa Uwekezaji huu utasaidia kuboresha upatikanaji wa  huduma za uchujaji wa damu kwa wagonjwa wa figo kwa  gharama nafuu nchini. Taasisi ya Nephroplus iliyopo mjini Hyderabad nchini India inayojishughulisha na utoaji wa huduma za kuchuja d

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU JULAI 31, 2023

Image
 

WAZIRI MKUU MAJALIWA AHUDHURIA GWARIDE LA JESHI LA WANAMAJI, URUSI

Image
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Rais wa Urusi, Vladimir Putin wakati alipohudhuri  gwaride la Jeshi la Wanamaji la nchi hiyo lililofanyika St. Petersburg nchini Urusi, Julai 30, 2023. Kushoto ni mkewe Mama Mary Majaliwa. 

MUHIMBILI imekidhi vigezo kushughulikia dharura za AFCON 2027

Image
 NA MWANDISHI WA MNH Hospitali ya Taifa Muhimbili imefuzu kuwa na uwezo wa kushughulikia dharura za kiafya zinazoweza kujitokeza katika michuano ya Mpira wa Miguu Barani Afrika (AFCON 2027) ikiwa Afrika Mashariki itapewa ridhaa ya kuwa mwenyeji wa michuano hiyo. Haya yameelezwa na Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bw. Saidi Yakub ambaye aliambatana na jopo la Wakaguzi kutoka Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika (CAF) ambao wapo nchini kukagua miundombinu muhimu ikiwemo viwanja vya michezo, Hoteli, Viwanja vya ndege na Hospitali. Katika kukagua leo wamefika hapa hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo wamekagua Idara ya Magonjwa ya Dharura na Ajali, mashine za kisasa za uchunguzi lakini pia wamepata maelezo mazuri kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Prof. Mohamed ambaye ameeleza uwezo na utayari wa MNH katika kutatua dharura zozote zinazoweza kujitokeza” amesema Bw. Yakub Amesema ukaguzi unakwenda vizuri na kwamba Muhimbili imekidhi vigezo v

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI JULAI 30, 2023

Image