Posts

Showing posts from November, 2021

WAZIRI MHAGAMA AIPONGEZA WCF KWA KUIPATIA VITENDEA KAZI (COMPUTERS) TUME YA USULUHISHI NA UAMUZI CMA

Image
  NA KHALFAN SAID, K-VIS BLOG, MBEYA WAZIRI wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama ameupongeza Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) kwa kuipatia vitendea kazi (computers) Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) ili kuharakisha shughuli za usuluhishi wa migogoro ya kikazi. Pongezi hizo zimetolewa na Mhe. Waziri wakati akikabidhi computer 10 kwa Mkurugenzi Mkuu   wa CMA, Bw.Shanes Nungu katika hafla fupi iliyofanyika kwenye ofisi za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) jijini Mbeya Novemba 29, 2021. “Tunashuhudia hapa Workers Compensation Fund (Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi) unafanya kazi nzuri ya kuiwezesha CMA ili itekeleze majukumu yake sawasawa jambo hili lina tija katika utendaji.” Alifafanua Mhe. Waziri. Kipekee napenda kuwashukuru sana sana wakuu wote na viongozi wa taasisi zote Dkt. John Mduma Mkurugenzi Mkuu wa WCF na ndugu Shanes Nungu Mkurugenzi Mkuu wa CMA kwa kuona umuhimu wa kufanya kazi kama serik

RAIS MUSEVENI ATEMBELEA JENGO LA STESHENI YA SGR LA TANZANITE JIJINI DAR ES SLAAM

Image
  RAIS wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni amefanya ziara kutembelea mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa – SGR katika Stesheni ya SGR jijini, Novemba 28, 2021. Rais wa Jamhuri ya Uganda yuko nchini Tanzania katika ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia Novemba 27 – 28 Novemba 2021. Lengo la ziara hiyo ni kuona maendeleo ya mradi huo wa kimkakati ambapo alipata fursa ya kukagua jengo la Stesheni ya Dar es Salaam ambalo limejengwa kwa mfano ya Madini ya Tanzania, madini ambayo yanapatika Tanzania pekee. Akihutubia katika ziara hiyo Mhe. Rais Museveni amesema kuwa amefurahishwa na namna nchi ya Tanzania inavyosonga mbele kiuchumi katika kuboresha miundombinu na kuongeza fursa za biashara na uwekezaji, jambo ambalo limechangiwa na mwamko mkubwa ambao watanzania wameupata kwa kufanya kazi na kukuza uchumi wa nchi. Rais Museveni ameongeza kuwa "Usafirishaji wa mizigo kwa njia ya treni ni bora, rahisi na unaokoa muda zaidi kwa sababu treni ina uwezo wa kusafirisha mzigo mkubwa k

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU NOVEMBA 29, 2021

Image
 

WAZIRI MAKAMBA AIHAKIKISHIA SHELL UTAYARI WA SERIKALI KUTEKELEZA MRADI WA LNG.

Image
Na Dorina G. Makaya - Dar-es-salaam . Waziri wa Nishati Mhe. January Makamba  tarehe 26 Novemba 2021, amekutana na Ujumbe kutoka Kampuni ya SHELL ulioongozwa na Makamu wa  Rais Mtendaji anaesimamia mradi wa kusindika gesi (LNG ) kwa upande wa Mashariki ( Africa, Asia na Australia) Bwana Cederic Cremers ambae amedhuru Tanzania kwa Mara ya Kwanza tangu kuchukua wadhifa huo mapema mwezi August 2021. Katika ujumbe huo, bwana Cremers aliongozana na Makamu wa Rais na mkazi wa Shell Tanzania, bwana Jared Kuehl pamoja na mdau mwenzao bi Unni Fjaer kutoka kampuni ya Equinor. Lengo la kikao hicho ni utambulisho wa Makamu wa Rais Mtendaji wa SHELL pamoja na kumhakikishia Waziri wa Nishati kuwa, Shell pamoja na Washirika wake wamejizatiti katika kuhakikisha mradi wa LNG unatekelezwa katika ufanisi, uwazi unaotakiwa na kwa wakati uliokusudiwa. Waziri wa Nishati, ameuambia ujumbe kutoka Kampuni ya Shell kuwa, Serikali ya Tanzania ipo tayari kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati kwa manuf

MAAFISA MICHEZO WAHIMIZWA KUTUMIA UTAALAMU WAO KUENDELEZA MICHEZO NCHINI

Image
  Na Eleuteri Mangi, WUSM-Arusha Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul ameviagiza Vyama vya Michezo pamoja na Maafisa Michezo nchini washiriki mashindano yanayoandaliwa na wadau wa michezo na kutoe elimu ya michezo na utaalamu wao ili michezo hiyo iwe na manufaa kwa wachezaji na taifa kwa ujumla. Naibu Waziri Gekul ametoa agizo hilo Novemba 26, 2021 jijini Arusha wakati akizindua Taasisi ya Iyanna Foundation ya jijini humo inayojishughlisha na kutoa elimu kwa wanafunzi wa kike kuhusu stadi za maisha ikiwemo kujilinda dhidi ya tatizo la mimba za utotoni. Uzinduzi huo umeendana pia na mshindano ya michezo ya mpira wa miguu kwa wanafunzi wa kike na wa kiume, mchezo wa kamba kwa wanafunzi wa kike na kiume, mchezo wa kurusha yai kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari za jijini humo. “Kama mdau yeyote anaandaa mashindano ya michezo yeyote ikiwa mpira wa miguu, netiboli, riadha wawajulishe Maafisa Michezo, TFF, Cheneta, chama riadha na mashirikisho mengine waje

RAIS SAMIA AMPOKEA MGENI WAKE RAIS WA UGANDA ALIYEWASILI NCHINI KUANZA ZIARA YA KISERIKALI YA SIKU TATU

Image
  Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni amewasili nchini kwa Ziara ya Kitaifa ya siku 3 yenye lengo la  kuimarisha uhusiano baina ya nchi yake na Tanzania kufuatia mualiko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan . Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam, Mhe. Rais Museveni amekagua gwaride la heshima lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa ajili yake pamoja na kupigiwa mizinga 21. Mhe. Rais Museveni alipowasili Ikulu Jijini Dar es Salaam amefanya mazungumzo na mwenyeji wake Mhe. Rais Samia pamoja na    kuzungumza na vyombo vya habari kuhusu masuala mbalimbali ya uhusiano na ushirikiano wa nchi hizi mbili. Katika mazungumzo yake na vyombo vya habari, Mhe. Rais Samia amesema Tanzania inaridhishwa na uhusiano mzuri na wa kindugu uliopo kati yake na Uganda na kusisitiza kuwa uhusiano huo utaendelea kudumishwa. Mhe. Rais Samia amesema yeye na Rais Museven