Posts

Showing posts from May, 2022

WANACHUO WA CHUO CHA UHASIBU, IAA JIJINI ARUSHA WACHANGAMKIA "BOOM VIBES NA NSSF" KWA KUJIUNGA NA MFUKO

Image
NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, ARUSHA KAMPENI ya “BOOM VIBES NA NSSF”  yenye lengo la kuhamasisha Wanachuo kuhusu Hifadhi ya Jamii na Uwekaji Akiba imefanyika kwenye Chuo cha Uhasibu jijini Arusha (IAA) leo Mei 31, 2022. Kampeni hiyo ni mkakati wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) chini ya Mpango wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii kwa sekta isiyo rasmi kutembelea taasisi mbalimbali za elimu ya juu na kati nchini ili kuhamasisha wanachuo kujenga tabia ya kujiwekea akiba kwa kujiunga na Mfuko na kuchangia kila mwezi ili hatimaye wanufaike na mpango wenyewe, Meneja wa Sekta Isiyo Rasmi, NSSF Bi. Rehema Chuma amewaambia wanachuo hao wakati akitoa  Elimu ya Hifadhi ya Jamii. Alisema wanachuo ni wanufaika wakubwa wa mpango huo kutokana na kipato wanachokipata wanaweza kutenga ziada na kujiwekea akiba NSSF kwa manufaa ya sasa na baadaye. “Ni muhimu wewe kama mwanachuo kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba kupitia NSSF, ukianza kuweka akiba mapema itakuwezesha kuwa na akiba ya kutosha

UWEKEZAJI WA MIUNDOMBINU KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA MAWENZI UTASAIDIA UPATIKANAJI WA HUDUMA BORA ZA MATIBABU

Image
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini – Wizara ya Afya Bi. Catherine Sungura akifafanua jambo kwa waandishi wa habari mara baada ya kufanya ziara ya kutembelea miradi ya ujenzi inayoendelea kufanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi, Kilimanjaro. Kaimu Mganga Mfawidhi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mawenzi, Kilimanjaro Dkt. Jonas Kessy akisema jambo kwa waandishi wa habari kuhusu miradi ya ujenzi inayoendelea katika Hospitali ya Mawenzi. Jengo la Huduma za Dharura katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mawenzi, Kilimanjaro ambalo limekamilika kwa asilimia 95 huku tayari huduma zikiwa zimeanza kutolewa. Ujenzi wa jengo hili umegharimu kiasi cha Milioni 764. Jengo la Huduma za Mama na Mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mawenzi, Kilimanjaro ambapo ujenzi wake umefikia hatua ya nane sasa.   Na WAF-Moshi. Serikali kupitia Wizara ya Afya imewekeza fedha kwa ajili ya kuboresha miundimbinu ya kutolea huduma za afya ikiwemo hospitali za rufaa za mikoa ambapo Hosp

SHAKA AWASHA RASMI MTAMBO WA KUSAMBAZA MAJI PAMOJA NA KUSHIRIKI UJENZI WA SHULE MAALUM YA SEKONDARI YA WASICHANA .

Image
  Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, leo amewasha mtambo wa maji na tone la kwanza la maji likatoka kwa wakazi wa eneo Mitwero mkoani Lindi . Akizungumza baada ya kuwasha mtambo huo, Shaka alisema kukamilika kwa mradi huo ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025 na jitihada za Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan katika kufikisha huduma za kijanii kwa wananchi. Mbali na mradi huo, pia shaka ametembelea na kushiri ujenzi wa Shule Maalumu ya Sekondari ya Wasichana Mkoa wa Lindi inayojengwa katika Kata ya Kilangala, Manispaa ya Lindi. Akizungumza kuhusu ujenzi wa Shule hiyo, shaka amewataka wananchi kuungana katika kupiga vita mambo yote yanayodhalilisha na kukatisha mdoto za mtoto wa kike kupata elimu. "Nichukue fursa hii kumpongeza Rais Samia kwanza kwa namna ambavyo amekuwa kinara wa usawa wa kijinsia nchini. Tangu ameingia madarakani moja ya jambo ambalo amejipambanua nalo na lazima tukiri hatukuwa

RC KUNENGE AWAASA WATAALAMU WA AFYA KUJA NA MIKAKATI YA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO

Image
 Mkuu wa Mkoa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amewataka watalaam wa afya Mkoani hapo kutumia  utaalamu wao na kuja na Mikakati  ili kuleta matokeo katika kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa  kujifungua. Kunenge ameyasema hayo Mei 30, 2022 wakati akifungua kikao kazi cha Wataalamu na Wadau wa Utekelezaji wa Mradi wa KOFIH Wilayani Bagamoyo ukumbi wa Millennium beach Resort Kunenge amewataka Wataalamu hao kushirikisha Wananchi katika uaandaaji wa mipango yao. "Lazima mjipange mumize Vichwa tupate Mikakati yenye matokeo chanya" alisema Kunenge.Kunenge amewaeleza kuwa tayari "Matarajio yanafahamika katika Sera na ilani ya chama cha mapinduzi nini kifanyike kufikia malengo hayo ni kazi yenu Wataalamu" alisema Kunenge. Kunenge ameeleza kuwa kupitia mradi huo Mkoa umeweza kupunguza Vito vya akina mama vitokanavyo na uzazi toka 82 mwaka 2015 hadi 51 mwaka 2021 na vifo vya watoto wachanga vimepungua kutoka 887 mwaka 2015 hadi 392 mwaka 2021. Kunenge amewashukuru wadau hao

KATIBU MKUU CHONGOLO AZUNGUMZA NA WANANCHI WA OLD SHINYANGA

Image
    Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akiwasalimia wakazi wa kata ya Old Shinyanga waliojitokeza kumlaki.   Katibu Mkuu anatarajiwa kumaliza ziara ya mkoa Shinyanga leo tarehe 30 Mei, 2022 katika wilaya ya Kishapu ambapo atakagua na kuhimiza Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020 – 2025 pamoja uhai wa Chama.

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE MEI 31, 2022

Image