Posts

Showing posts from September, 2023

Asilimia 77.3 ya Vijiji Kagera Vyaunganishwa na Umeme wa REA

Image
 Na Lilian Lundo na Veronica Simba Vijiji 512 kati ya Vijiji 662 vya Mkoa wa Kagera ambayo ni sawa na asilimia 77.3 ya vijiji vya mkoa huo vimepata huduma ya umeme kupitia miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ikiwemo Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza, REA Awamu ya Pili na REA Awamu ya Kwanza.  Vijiji 150 ambavyo bado havijaunganishwa na umeme mkoani humo, vitaunganishwa na umeme kupitia Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili, ambapo tayari mkandarasi  anaendelea na kazi za  mradi huo. Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy amesema jumla ya shilingi bilioni 80 imetolewa na Serikali kutekeleza miradi mbalimbali ya usambazaji wa umeme vijijini mkoani humo. “Kupitia Wakala wa Nishati Vijijini ndani ya Mkoa wa Kagera imewekeza shilingi bilioni 80 kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya kusambaza umeme vijijini, na hivi ninavyoongea ndani ya mkoa huu kuna miradi mitano inatekelezwa,” amesema Mhandisi Saidy wakati wa hafla wa uwashaji wa umeme Kijiji cha Mub

TANZANIA, USWISI NA IRELAND ZASAINI MKATABA WA KUNUSURU KAYA MASIKINI.

Image
  Na Scola Malinga na Joseph Mahumi, WF, Dar es Salaam. Serikali ya Tanzania imesaini mikataba miwili ya msaada yenye thamani ya dola za Marekani milioni 20.3 sawa na shilingi bilioni 50.13 kwa ajili ya kunusuru kaya masikini awamu ya pili (PSSN II). Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba alisema msaada huo umetolewa na Serikali ya Uswisi dola za Marekani milioni 18 na Euro milioni 2.2 sawa na dola za Marekani milioni 2.3 zimetolewa na Serikali ya Ireland. "Kiasi cha misaada kilichosainiwa leo ni mwendelezo wa misaada mingine iliyopokelewa kutoka kwa serikali hizi mbili ambapo misaada ya kipindi cha nyuma kwa mpango huu wa kunusuru kaya maskini awamu ya pili ilikuwa faranga za Uswisi milioni 15.72 sawa na dola za Marekani milioni 17.1 kutoka serikali ya Uswiss na Euro milioni 2 sawa na dola za Marekani milioni 2.1 kutoka serikali ya Ireland. ," alisema Dkt. Mwamba. Alisema misaada hiyo imewezesha serikali kufanya kazi yao kuwa rahisi katika kuleta mae

RAIS SAMIA AMJULIA HALI DKT. SALIM NYUMBANI KWAKE OYSTERBAY JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amemtembelea na kumjulia hali, Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim, nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es Salaam, mara baada ya uzinduzi wa Tovuti ya Hifadhi ya Nyaraka za Kumbukumbu za Kidigitali za Mwanadiplomasia huyo mbobezi kwenye hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 30 Septemba, 2023.

NAIBU WAZIRI SAGINI AZINDUA MFUMO WA KIDIGITALI WA URA MOBILE MONEY

Image
  Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam  Jeshi la Polisi nchini limezindua Mfumo wa kidijitali wa huduma za kifedha uitwao (URA MOBILE MONEY) utakaotumika na Viongozi pia Wanachama wa URA SACCOS katika Chuo cha Taaluma ya Polisi  jijini Dar es Salaam Leo Septemba 30, 2023. Akizungumza katika hafla fupi ya Uzinduzi wa Mfumo huo Mgeni Rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini, amelipongeza Jeshi la Polisi nchini kwa kutambua umuhimu wa kuwa na huduma za kifedha zinazotolewa na kupatikana kwa gharama nafuu kwa Watumishi wake na hivyo kuanzisha Ushirika wa kuweka Akiba na Kukopa (SACCOS) miaka 17 iliyopita. "Nafahamu kama ilivyoelezwa kwamba, tangu kuanzishwa kwa Ushirika huu Tarehe 6 Septemba 2006, na kuutambua katika Kanuni za Kudumu za Utendaji za Jeshi la Polisi (P.G.O 212) fursa mbalimbali zimetolewa kwa Watumishi kama vile uwekaji wa akiba na utoaji wa mikopo yenye masharti nafuu ukilinganishwa na taasisi nyingine za kifedha," amesema Mhe. Sagini

RAIS SAMIA AZINDUA TOVUTI YA NYARAKA ZA DKT. SALIM AHMED SALIM

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tovuti ya Hifadhi ya Nyaraka za Kumbukumbu za Kidigitali za Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim iliyofanyika JNICC jijini Dar es Salaam tarehe 30 Septemba, 2023. Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan pamoja na Ahmed Salim mtoto wa kiume wa Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim, wakifuatilia kwa makini video fupi ya kumbukumbu mbalimbali (hazionekani pichani) wakati wa hafla ya uzinduzi wa Tovuti ya Hifadhi ya Nyaraka za Kumbukumbu za Kidigitali  za Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 30 Septemba, 2023. Sehemu ya wanafamilia ya Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim wakifuatilia hafla ya uzinduzi wa Tovuti ya Hifadhi ya Nyaraka za Kumbukumbu za Kidigitali za kiongozi huyo iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam Septemba 30, 2023. Viongozi mbalimbali wakifuatil

RAIS SAMIA AMPONGEZA MWADHAMA PROTASE KARDINALI RUGAMBWA KWA KUSIMIKWA RASMI NA BABA MTAKATIFU FRACISKO

Image
Rais wa Jamhuri ya Muunganio wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hasan, ametuma salamu za pongezi kufuatia kusimikwa rasmi na baba Mtakatifu Francisko kuwa Kardinali, Protase Kardinali Rugambwa (pichani) huko Vatican. Rais  ameandika kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii "Pongezi za dhati kwa  Mwadhama Protase Kardinali Rugambwa, kwa kusimikwa rasmi na Baba Mtakatifu Francisko kuwa Kardinali. Kauli mbiu ya utume wako ni "Enendeni ulimwenguni kote", ikiakisi mafundisho ya Yesu Kristo katika Injili ya Marko 16:15, juu ya utume unaojali watu wote, sehemu zote na wakati wote. Naungana na Watanzania wote kukuombea kheri, afya njema, na mafanikio katika utumishi wako.  

KUTOKA MAGAZETINI LEO SEPTEMBA 30, 2023

Image