RAIS SAMIA AMJULIA HALI DKT. SALIM NYUMBANI KWAKE OYSTERBAY JIJINI DAR ES SALAAM
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan,
leo amemtembelea na kumjulia hali, Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Dkt. Salim Ahmed
Salim, nyumbani kwake Oysterbay jijini Dar es Salaam, mara baada ya uzinduzi wa
Tovuti ya Hifadhi ya Nyaraka za Kumbukumbu za Kidigitali za Mwanadiplomasia
huyo mbobezi kwenye hafla iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa
cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 30 Septemba, 2023.
Comments
Post a Comment