Posts

COMANDOO WA JWTZ WANOGESHA SHEREHE ZA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
Askari wa Kikundi Maalum cha Komando   cha   Jeshi   la   Wananchi   wa   Tanzania (JWTZ)   akipita mbele ya jukwaa kuu na zana zake   wakati   wa kilele   cha   Sherehe   za Miaka   60   ya   Muungano   wa   Tanganyika   na Zanzibar   katika   uwanja   wa   Uhuru   Jijini   Dar   es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024 Askari wa Kikundi Maalum cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) akishuka kwenye Helikopta kwa ajili ya kwenda kuelezea namna   mbalimbali   za   kwata   na   mapigano   ya mjini wakati wa kilele cha Sherehe za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam Maonesho   ya   Kwata   ya Kikundi   cha   Askari   wa   Jeshi   la   Polisi   Tanzania kutoka   Zanzibar   Maarufu   kama   Askari   wa Tarabushi   wakionesha   Maonesho   mbalimbali   ya aina   ya   Kwata   tangu   kipindi   cha   utawala   wa Sultan na kabla ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.   Askari   hao   walijipatia   umaarufu mkubwa   kutokana   na   uvaaji   wa   Ko

RAIS SAMIA AKUTANA NA MARAIS WA ZAMBIA, COMMORRO NA MAKAMU WA RAIS WA MALAWI

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na kuzungumza na Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na kuzungumza na Rais wa Comoro Mhe. Azali Assoumani Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Malawi Mhe. Lazarus Chakwera uliowasilishwa na Makamu wa Rais wa Nchi hiyo Mhe. Saulos Klaus Chilima Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Aprili, 2024.  

TANROADS YAENDELEA NA UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA GONGOLAMBOTO JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) imehakikisha utekelezaji wa mradi wa mabasi yaendayo haraka; barabara ya Nyerere hadi Gongo la mboto unaendelea huku barabara ya kawaida ikiendelea kupitika hata katika kipindi hiki cha mvua kubwa zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali Nchini. Akizungumza wakati alipofanya ziara katika mradi huo Meneja wa miradi ya mabasi yaendayo haraka (BRT-3) iliyopo chini ya Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mhandisi Frank Mbilinyi amesema amefanya ukaguzi wa kawaida kumuimiza mkandarasi kuhakikisha pamoja na athari za mvua lakini barabara inapitika wakati wote. “Tumeendelea kumuhimiza mkandarasi kuhakikisha maeneo yote yanayotekelezwa mradi wa ujenzi wa barabara ya Nyerere - Gongolamboto yanapitika kiurahisi pamoja na athari za mvua kila baada ya mvua kukatika ahakikishe anaziba mashimo na kusawazisha ili kuwezesha kurejesha mawasiliano ya barabara japo kuna ujenzi unaendelea” Amesisitiza na kuongeza kuwa “Tunashirikiana vizuri na mkan

KUTOKA MAGAZETINI LEO APRILI 27, 2024

Image
 

TANROADS YAWEKA KAMBI BARABARA YA MOROGORO- IRINGA KUZIBA MASHIMO MAENEO YALIYOHARIBIWA NA MVUA

Image
Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Morogoro inaendelea na kazi ya kuziba mashimo na kukarabati barabara kuu ya Morogoro – Iringa ikiwemo katika eneo la Kobogwa lilipo katika hifadhi ya Taifa ya Mikumi ambapo kumetokea shimo kubwa baada ya maji kupita pembezoni mwa Kalvati. Akizungumza na Kipindi cha TANROADS Mkoa kwa Mkoa leo tarehe 26 Aprili 2024; Meneja wa TANROADS Mkoa wa Morogoro Mhandisi Alinanuswe L. Kyamba amesema kuwa tayari Mkandarasi yupo eneo hilo akiendelea na kazi ambapo mpaka kufika leo usiku kazi hiyo utakuwa imemalizika. "Mvua zimeendelea kunyesha bila kukatika na jitihada zinaendelea kufanyika kila siku, eneo hili ambalo limeleta taharuki katika barabara hii ya Mikumi. Mashimo yametokea juzi, tukayaziba kidharura lakini unapoziba kidharura mvua zikinyesha tena zinaondoa ule mchanga ambao tumeuweka kwa sababu kipindi hiki cha mvua huwezi kuziba na lami, lami haikubali kipindi cha mvua mpaka jua liwake" Amekaririwa Mhandisi Kyamba n