3/19/2024

KOICA KUONGEZA NGUVU UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO

Na. Saidina Msangi na Peter Haule, WF, Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Natu El- Maamry Mwamba, amesema Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA), kupitia mpango uliotiwa saini mwaka 2014 limetoa ruzuku ya jumla ya Dola za Kimarekani milioni 139.5 sawa na Sh. bilioni 356.3 kwa Tanzania kwa ajili ya kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Dkt. Mwamba alibainisha hayo jijini Dodoma alipokutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea anayeshughulikia mambo ya kimkakati (KOICA) Don Ho Kim, aliye katika ziara ya kikazi Tanzania.

Alisema kuwa kupitia fedha hizo miradi kadhaa imekamilika na mingine inaendelea ambayo ni pamoja na Mfuko wa sekta ya  Afya na Mpango Jumuishi wa Vijana Walio nje ya Shule (IPOSA).

‘‘Miradi kadhaa iko katika hatua mbalimbali za maandalizi, ikiwa ni pamoja na kuanzisha mifumo ya usambazaji maji kwa maeneo ya mijini na vijijini mjini Dodoma na kuboresha usawa wa kijinsia katika Elimu (STEM) kwa Shule za Sekondari nchini ambapo miradi hii kwa sasa inapitia michakato ya kuidhinishwa ndani ya Wizara husika’’ alisema Dkt. Mwamba.

Alisema tangu 1991, KOICA imesaidia Serikali hasa katika nyanja za afya, elimu, maji na usafiri ili kubadilisha hali ya kijamii na kiuchumi nchini.

Dkt. Mwamba alisema kuwa kupitia mipango mbalimbali ya ufadhili, usaidizi wa kiufundi na programu za kujenga uwezo, KOICA imechochea mabadiliko chanya na yaliyosaidia ukuaji na ustawi jumuishi, kupambana na umaskini na kukuza uchumi.

Aidha alieleza kuwa Agosti 2023, Wizara ya Fedha iliwasilisha ombi la miradi minne ya maendeleo kwa msaada wa KOICA ya jumla ya Dola za Kimarekani milioni 39, sawa na Sh. bilioni  98, inayotarajiwa kutekelezwa kuanzia mwaka 2025.

Dkt. Mwamba alibainisha miradi hiyo kuwa ni mradi wa kuanzisha  chuo cha ufundi Morogoro,  mradi wa kuimarisha huduma za mama na mtoto jijini Dar es Salaam, mradi wa kuanzisha mifumo ya usambazaji maji katika maeneo ya vijijini vya mkoa wa pwani na mradi wa kuanzisha mpango kabambe wa kitaifa wa barabara kuu na uboreshaji wa uwezo wa rasilimali watu.

Dtk. Mwamba aliishukuru  Serikali ya Jamhuri ya Korea kupitia KOICA kwa kuunga mkono malengo hayo ambapo imekuwa mojawapo ya vyanzo vikuu vya ufadhili wa ruzuku katika kufanikisha miradi ya maendeleo na kusisitiza kuwa Tanzania itaendelea  kuhakikisha kuwa rasilimali zote zinazopatikana kutoka KOICA zinatumika kwa uangalifu ili kufikia malengo yaliyokusudiwa ndani ya muda uliokubaliwa.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) Don Ho Kim, alisema kuwa Korea itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maendeleo ya uchumi hasa katika ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji, afya pamoja na kuwezesha wafanyabiashara wadogo kuweza kunufaika na masoko.

Kuhusu miradi iliyowasilishwa na Tanzania alisema kuwa, ipo katika mchakato wa kuidhinishwa na Shirika hilo ambapo kati ya Novemba na Desemba mwaka huu inatazamiwa kuidhinishwa na Bunge la nchi hiyo, aliahidi nchi yake kuendeleza ushirikiano na kuunga mkono mipango ya maendeleo ya  Tanzania

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, akimkabidhi zawadi yenye picha ya Mlima Kilimanjaro, Makamu wa Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) anayeshughulikia mambo ya kimkakati, Mhe. Dong Ho Kim, baada ya kumaliza kikao kilichojadili ushirikiano na utekelezaji wa miradi ikiwemo ya miundombinu, elimu na afya, kilichofanyika jijini Dodoma.

Ujumbe kutoka Tanzania ulioongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba (kushoto) na ujumbe kutoka Jamhuri ya Korea uliyoongozwa na Makamu wa Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) anayeshughulikia mambo ya kimkakati, Mhe. Dong Ho Kim ukiwa katika mkutano ulioangazia ushirikiano wa maendeleo, kilichofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba akizungumza kuhusu miradi ya maendeleo wakati wa kikao na Makamu wa Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) anayeshughulikia Mambo ya Kimkakati Mhe. Dong Ho Kim, jijini Dodoma.

Makamu wa Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA), anayeshughulikia mambo ya kimkakati, Mhe. Dong Ho Kim, akizungumza wakati wa kikao na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba ambapo alisema kuwa Korea itaendelea kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali, kilichofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba, akiagana na Makamu wa Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA) anayeshughulikia mambo ya kimkakati, Mhe. Dong Ho Kim, baada ya kumaliza kikao kilichojadili ushirikiano wa maendeleo kati ya Tanzania na Korea katika utekelezaji wa miradi mbalimbali, kilichofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-Maamry Mwamba (watano kulia), na Makamu wa Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Korea (KOICA), anayeshughulikia mambo ya kimkakati, Mhe. Dong Ho Kim (wasita kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe kutoka Wizara ya Fedha na ujumbe kutoka Korea (KOICA), baada ya kikao kilichojadili kuimarisha ushirikiano, kilichofanyika jijini Dodoma.


    

3/18/2024

KUTOKA MAHAKAMA YA WILAYA YA MULEBA - KAGERA

 Machi 15, 2024 katika Mahakama ya Wilaya Muleba mbele ya Mh Lilian Mwambeleko,  imeamriwa kesi ya Jinai namba 3/2024.

Kesi hii ni Jamhuri dhidi ya *Bw. Masanja Igolola Afisa Manunuzi VETA, Ndorage pamoja na Denis  Rwegalulila Mzabuni*.

Walishtakiwa kwa kosa la Hongo katika Manunuzi ambapo wanadaiwa kufanya 'manunuzi hewa' Mwaka 2019 ya Mashine aina ya *Porker Vibrator High F* na hivyo kujipatia manufaa yasiyo stahiki ya TZS 2,800,000/-. 

Kesi iliendeshwa na *Wakili Kelvin Murusuri*.

Mahakama imewakuta na hatia na kuwaamuru walipe faini ya shilingi Milioni Moja (1,000,000/-) au kutumikia kifungo cha miaka miwili jela.

Vilevile, Mahakama imewataka warejeshe fedha hizo zote TZS 2,800,000/- walizojipatia kwa manunuzi hewa.

Washtakiwa wamelipa faini 1,000,000/- na kurejesha TZS 2,800,000/- katika ofisi ya TAKUKURU Wilaya ya Muleba.

Wakati huo huo katika Shauri la Rushwa Na. O4$/2024.

Kesi hii ni ya Jamhuri Dhidi ya *Bw. Raysone Baliyeguje* ambaye ni mkusanyaji wa mapato kwa njia ya POS Halmashauri ya Wilaya ya Muleba. 

Alishitakiwa kwa kosa la Hongo  kinyume na Kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329/2022 kwa kujipatia manufaa  yasiyostahili wakati wa ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali TZS 5,292,900/_ on hivyo kufanya upotevu wa Shilingi 5,292,900/- mali ya Halmashauri ya Muleba. 

Kesi iliongozwa na *Wakili Kelvin Murusuri*

Mahakama imemhukumu mshitakiwa adhabu ya *kulipa faini ya Laki tano 500,000/- au kwenda jela miaka miwili na kurejesha fedha zote ndani ya miezi Mitatu.*

Mshtakiwa ameenda gerezani akisubiria taratibu za kulipa faini.

Machi 15, 2024 katika Mahakama ya Wilaya Muleba mbele ya Mh Lilian Mwambeleko,  imeamriwa kesi ya Jinai namba 3/2024.

Kesi hii ni Jamhuri dhidi ya *Bw. Masanja Igolola Afisa Manunuzi VETA, Ndorage pamoja na Denis  Rwegalulila Mzabuni*.

Walishtakiwa kwa kosa la Hongo katika Manunuzi ambapo wanadaiwa kufanya 'manunuzi hewa' Mwaka 2019 ya Mashine aina ya *Porker Vibrator High F* na hivyo kujipatia manufaa yasiyo stahiki ya TZS 2,800,000/-. 

Kesi iliendeshwa na *Wakili Kelvin Murusuri*.

Mahakama imewakuta na hatia na kuwaamuru walipe faini ya shilingi Milioni Moja (1,000,000/-) au kutumikia kifungo cha miaka miwili jela.

Vilevile, Mahakama imewataka warejeshe fedha hizo zote TZS 2,800,000/- walizojipatia kwa manunuzi hewa.

Washtakiwa wamelipa faini 1,000,000/- na kurejesha TZS 2,800,000/- katika ofisi ya TAKUKURU Wilaya ya Muleba.

Wakati huo huo katika Shauri la Rushwa Na. O4$/2024.

Kesi hii ni ya Jamhuri Dhidi ya *Bw. Raysone Baliyeguje* ambaye ni mkusanyaji wa mapato kwa njia ya POS Halmashauri ya Wilaya ya Muleba. 

Alishitakiwa kwa kosa la Hongo  kinyume na Kifungu cha 15 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura ya 329/2022 kwa kujipatia manufaa  yasiyostahili wakati wa ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali TZS 5,292,900/_ on hivyo kufanya upotevu wa Shilingi 5,292,900/- mali ya Halmashauri ya Muleba. 

Kesi iliongozwa na *Wakili Kelvin Murusuri*

Mahakama imemhukumu mshitakiwa adhabu ya *kulipa faini ya Laki tano 500,000/- au kwenda jela miaka miwili na kurejesha fedha zote ndani ya miezi Mitatu.*

Mshtakiwa ameenda gerezani akisubiria taratibu za kulipa faini.



    

DKT NCHEMBA ATETA NA BALOZI WA DENMARK NCHINI TANZANIA-MEMA YAJA

Na Benny Mwaipaja, Dodoma

WAZIRI wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameishukuru Denmark kwa kuchangia maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii pamoja na ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Singida.

Dkt. Nchemba ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mheshimiwa Mette Dissing-Spandet, Ofisini kwake Jijini Dodoma ambapo walijadili masuala kadhaa ya ushirikiano.

Alisema kuwa uhusiano wa Tanzania na Denmark umetimiza miaka 60 na katika kipindi hicho nchi hizo mbili zimekuwa na uhusiano mzuri wa kidiplomasia na kiuchumi ambapo hivi karibuni nchi hizo zilikuwa zikitekeleza miradi ambayo Denmark iliipatia Tanzania msaada wa takriban Denish Krone bilioni 2, sawa na shilingi za Tanzania bilioni 646.

Aidha, Dkt. Nchemba alisema kuwa Denmark kupitia Shirika ake la Maendeleo (DANIDA), imetoa zaidi ya shilingi bilioni 103 zinazotokana na mapato ya uwekezaji wake wa hisa katika Benki ya CRDB, ambazo zimetumika kwa ajili ya kusaidia sekta ya afya kupitia Mfuko wa Afya.

Aidha, aliipongeza Denmark kwa kusitisha uamuzi wake wa kutaka kufunga Ubalozi wake hapa nchini na kwamba hatua hiyo itaimarisha zaidi ushirikiano kwa manufaa ya wananchi wa pande hizo mbili.

Dkt. Nchemba alisema kuwa Tanzania iko tayari kushirikiana na Denmark kupitia mpango wake mpya wa ushirikiano baada ya kusitisha uamuzi huo wa kufunga ubalozi wake nchini ambapo nchi hiyo imepanga kuongeza kiwango cha ufadhili na kuelekeza fedha hizo kwenye maeneo yatakayokuza uchumi, ikiwemo nishati, kuboresha mifuko ya kodi, kilimo, elimu, afya, pamoja na kusaidia sekta binafsi.

Dkt. Nchemba pia alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wawekezaji kutoka Denmark kuja kuwekeza mitaji yao hapa nchini ikiwemo sekta ya fedha na kunufaika na vivutio vilivyowekwa na Serikali baada ya kurekebisha sheria kadhaa, lakini pia kunufaika na soko la uhakika linalopatikana katika nchi za SADC na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Aliiomba pia Denmark kupitia Taasisi yake inayohusika na masuala ya Bima na Dhamana (Danish Export Credit Agency), kushiriki katika ujenzi wa mradi wa SGR kwa vipande vilivyobaki kutokana na umuhimu wa mradi huo katika kukuza biashara na ustawi wa maisha ya watu watakao tumia reli hiyo pamoja na kukuza pato la Taifa.

Kwa upande wake, Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mheshimiwa Mette Dissing-Spandet alisema kuwa nchi yake inapongeza mafanikio makubwa ya kiuchumi na kijamii yanayoendelea hivi sasa na kwamba iko tayari kutoa ushirikiano unaohitajika ili kuimarisha zaidi uhusiano wa nchi hizo mbili.

Mheshimiwa Spandet alisema kuwa nchi yake iko tayari kushirikiana na Tanzania katika eneo la nishati jadidifu, pamoja na gesi na kusaidia kukuza sekta binafsi ili iweze kuchangia maendeleo ya nchi.

Alisema kuwa Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo Kimataifa, Mhe. Dan Jorgensen, anatarajia kufanya ziara rasmi ya kikazi hapa nchini mwanzoni mwa mwezi Aprili mwaka huu, ambapo atatumia ziara hiyo kujadiliana na Serikali maeneo ya kipaumbele ambayo nchi hizo zitajielekeza katika mpango huo mpya wa ushirikiano.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Denmark hapa nchini, Mhe. Mette Dissing-Spandet, ambapo ameishukuru nchi hiyo kwa kuchangia maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii pamoja na ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Singida. Mkutano huo umefanyika Katika Ukumbi wa Mikutano wa Waziri wa Fedha, Jijini Dodoma.

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Denmark hapa nchini, Mhe. Mette Dissing-Spandet, ambapo ameishukuru nchi hiyo kwa kuchangia maendeleo ya Tanzania katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii pamoja na ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kipande cha Morogoro hadi Makutupora mkoani Singida. Mkutano huo umefanyika Katika Ukumbi wa Mikutano wa Waziri wa Fedha, Jijini Dodoma. Kulia ni Mchumi na Mkuu wa masuala ya Biashara-Ubalozi wa Denmark nchini Tanzania, Bw. Oscar Mkude.





    

WAUMINI KANISA BAPTIST KINONDONI WAANDAA IBADA MAALUM KULIOMBEA TAIFA

 

WAUMINI wa Kanisa la Baptist Kinondoni mkoani Dar es Salaam  wakiongozwa na  Mchungaji wa kanisa hilo Samweli Kabonaki wamefanya ibada maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania katika kipindi cha majanga yakiwemo mafuriko yanayosababishwa na vua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalmbli za nchi yetu na nchi jirani.Akizungumza wakati wa ibada hiyo ,Mchungaji Kabonaki amesema Watanzania na Dunia wanajua kipindi wanachopitia kutokana na uwepo wa majnga yanayoleta madhara katika maeo mbalimbali ya nchini na nje ya nchi."Tumeona  ni vema Kanisa hilo likafanya maombi maalum kuombea nchi yetu na mataifa mengine na duna kiujumla,"amesema na kusisitiza katika kukabiliana na majanga hayo ni vema kila mmoja wetu akamtanguliza Mungu zaidi na yvema ikajulikana Mungu ambaye ndiye mwenye majibu yote na  ni mponyaji Mkuu."




Ibaada ikiendelea

Waimbaji wa kwaya ya Shalom wakiimba wakati wa ibaada ya maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania katika kipindi hiki cha majanga mbalimbali leo  Mkoa wa Dar es Salaam.













 

    

MAKALA: WANANCHI KATA 22 WASIKILIZENI WAGOMBEA, MPIGE KURA

 

Wagombea wa vyama mbalimbali wakiangalia fomu za uteuzi wa wagombea walioteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kugombea nafasi ya udiwani Kata ya Kimbiji iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Dar es Salaam. 
********"""
Na Mroki Mroki

TUME ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza Machi 20,2024 kuwa ni siku ya kupiga kura katika Uchaguzi Mdogo wa udiwani katika Kata 23 za Tanzania Bara.

 

Tume ilitangaza uchaguzi huo baada ya kuketi katika kikao chake cha Februari 15 mwaka huu na siku hiyohiyo, Mkurugenzi wa Uchaguzi, Bw. Kailima, R. K  akatoa taarifa kwa umma juu ya uwepo wa uchaguzi huo mdogo.

 

Tayari mchakato wa Uchaguzi huo umeshaanza ambapo Februari 27 hadi Machi 4, 2024 wagombea walichukua fomu za uteuzi, uteuzi ulifanyika Machi 4,2024 na kampeni za uchaguzi zilianza Machi 5,2024 na zinaendelea hadi tarehe 19 Machi, 2024.

 

Hata hivyo, baada ya hatua ya uteuzi, Kata ya Nkokwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Kyela ilipata mgombea mmoja tu aliyeteuliwa bila kupingwa hivyo hakutakuwa na kampeni kwenye Kata hiyo. Hivyo, uchaguzi utafanyika kwenye kata 22 zilizobakia.

 

Kata zitakazofanya uchaguzi huo mdogo ni Kimbiji (Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni), Kasingirima (Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji), Ndevelwa (Halmashauri ya Manispaa ya Tabora), Msangani (Halmashauri ya Mji Kibaha), Fukayosi(Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo), Mlanzi (Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti), Utiri (Halmashauri ya Mji Mbinga) na Mbingamhalule (Halmashauri ya Wilaya ya Songea).

 

Nyingine ni  Isebya (Halmashauri ya Wilaya ya  Mbogwe), Kibata (Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa), Mshikamano (Halmashauri ya Manispaa ya Musoma), Busegwe (Halmashauri ya Wilaya ya Butiama), Kamwene (Halmashauri ya Wilaya ya Mlimba), Chipuputa (Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu), Buzilasoga (Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema), Mhande (Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba), Kabwe (Halmashauri ya Nkasi), Bukundi (Halmashauri ya Wilaya ya Meatu) Mkuzi (Halmashauri ya Wilaya ya Muheza) na Boma, Mtimbwani na Mayomboni (Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga).

 

Katika Uchaguzi huu wa Kata 22, Vyama vya siasa 18 vimesimamisha wagombea 127 kati ya hao wanaume ni 89 na wanawake ni 38. Wagombea kutoka kwenye vyama hivyo walichukua fomu za uteuzi na kuzirejesha na hatimaye wakateuliwa kuwania nafasi hiyo.

 

Wagombea wa vyama mbalimbali wakiangalia fomu za uteuzi wa wagombea walioteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kugombea nafasi ya udiwani Kata ya Kimbiji iliyopo Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni, Dar es Salaam. 

Wagombea wote wameaminiwa na kupewa ridhaa na vyama vyao vya siasa kuwania nafasi zilizowazi,  kwa kufanya hivyo, vyama hivyo vya siasa  vimewatendea haki wanachama wao na wananchi kwa ujumla kwa kuwa wamepata haki ya kikatiba ya kugombea lakini pia wanachama na wananchi, watapata haki yao ya kikatiba ya kupiga kura na kuwachagua viongozi wanaowataka.

 

Wagombea walioteuliwa na Tume ni wale waliopendekezwa na vyama vyao vya siasa kugombea kiti cha udiwani ambapo pia walijaza na kuwasilisha fomu za uteuzi katika Ofisi za Uchguzi katika Kata husika.

 

Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya kata walisimamia vyema majukumu yao ya kutoa fomu za uteuzi. Fomu za uteuzi za wagombea wote ziliwasilishwa siku ya uteuzi kabla ya saa kumi kamili (10:00) jioni.

 

Wagombea hawa wote siku ya uteuzi walijaza na kusaini mbele ya Msimamizi wa Uchaguzi Fomu Na. 10 ya maadili ya uchaguzi.

 

Wagombea hawa walijaza fomu hizo   kukiri kuheshimu na kuyazingatia maadili ya uchaguzi yaliyosainiwa na  viongozi wa vyama vyao mwaka 2020 wakati wa uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Madiwani kwa Tanzania Bara.

 

Uwepo wa maadili ya Uchaguzi unalenga hasa kuwa na uchaguzi huru, wa haki, uwazi na wa kuaminika. Na kwamba amani, ustawi wa nchi, usalama wa raia, uhuru wa vyama vya siasa na utii wa sheria , kanuni na taratibu za uchaguzi ndio msingi wa uchaguzi ulio huru, haki na wenye kuzingatia ushiriki wa makundi yote ya jamii katika uchaguzi.

 

Vyama vya Siasa, Serikali na Tume walikubaliana kuwajibika kuyatekeleza Maadili hayo yanayotokana na kifungu cha 124A cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343. Viongozi hao kwa pamoja walisema “Tutafanya jitihada za wazi kuhakikisha Maadili haya yanajulikana na kuheshimiwa na wagombea pamoja na wanachama wote wa vyama vya siasa”.

 

Sheria, Kanuni na miongozo yote iliyotumika katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 bado inatumika na kufuatwa na vyama vya siasa, Tume ya Taifa ya Uchagzi na Serikali katika chaguzi hizi ndogo za udiwani.

 

Tayari Kampeni za uchaguzi zimeanza tangu siku moja baada ya uteuzi na zitaendelea hadi siku moja kabla ya siku ya kupiga kura.

 

Wakati wote wa kampeni wagombea wanatakiwa kuzingatia sheria, kanuni za uchaguzi, Maadili ya Uchaguzi na ratiba za kampeni.

 

Uzingatiaji wa Sheria, Kanuni, Maadili ya Uchaguzi na ratiba za kampeni utasaidia katika kuweka uwanja sawa katika kipindi chote cha kampeni na siku ya uchguzi.

 

Vyama vya Siasa na wagombea pamoja na wafuasi wao wanapaswa kuepuka kufanya siasa za fujo na za vitisho dhidi ya upande mwingine.

 

Aidha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa mujibu wa kifungu cha 4C cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, imepewa jukumu la kutoa elimu ya mpiga kura nchi nzima, kuratibu na kusimamia taasisi au asasi za kiraia zinazotoa elimu hiyo.

 

Tume itatoa elimu kwa wananchi katika maeneo yote ambayo yanafanya uchaguzi mdogo. Lakini pia zipo asasi ambazo zimepewa kibali na Tume kutoa elimu hiyo kwa baadhi ya maeneo.

 

Elimu hiyo inayotolewa ni ile ya kumuwezesha Mpiga Kura kutambua sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi ikiwa ni pamoja na utaratibu mzima wa kufunguliwa na kufungwa kwa vituo vya kupigia kura. 

 

Lakini pia elimu hiyo itasaidia kutoa hamasa kwa wananchi kutumia haki yao ya kikatiba katika kujitokeza kupiga kura na kuchagua viongozi wanaowataka.

 

Ni muhimu wananchi katika maeneo yote yanayofanya uchaguzi mdogo wakajitokeza kwa wingi kusikiliza sera za vyama na wagombea kisha kwa utashi wao wachague viongozi wanaowafaa kujaza nafasi zilizowazi katika Kata 23 za Tanzania Bara.

 

Mwandishi wa Makala haya ni Afisa Habari Msaidizi Mwandamizi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

    

MIAKA MITATU YA RAIS SAMIA YAIPAISHA TAWA

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

MAMLAKA ya Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), imefanikiwa kukusanya jumla ya TZS bilioni 184.74 katika kipindi cha kati ya mwaka 2020/21 hadi 2024.

Hayo yamesemwa na Kamisha wa Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Kamishna Mabula Misungwi Nyanda, Jijini Dar Es Salaam Machi 18, 2024, wakati akitoa wasilisho la mafanikio ya TAWA kwa kipindi cha miaka mitatu (2021/22-2023/24 ) ya serikali ya awamu ya sita ya uongozi wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amesema juhudi za makusudi zilizofanywa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kutangaza utalii kupitia filamu ya Royal Tour, Fedha za UVIKO 19 chini ya Mpango  wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19 (Tanzania Social Economic Response and Recovery Plan (TCRP ) ambapo TAWA imefaidika kwa kuimarisha miundombinu wezeshi ya Utalii katika maeneo mbalimbali

Ametaja maeneo hayo ni pamoja na ujenzi wa Kilomita 431.4 za barabara katika Mapori ya Wamimbiki, Mpanga Kipengere, Igombe, Swagaswaga, Mkungunero, Kijereshi, Rungwa na Pande,

Aidha TAWA pia imeweza kukarabati viwanja vya ndege vitatu (3) katika Pori Tengefu Lake Natron (Engaresero) na Pori la Akiba Maswa (Buturi na Mbono),

Pia kujenga  miundombinu ya kupumzika wageni (Bandas 13, Campsites - 6, picnic sites - 8, lounge 1) na hostel 1  katika Mapori ya Akiba Mpanga Kipengere, Mkungunero, Lukwika Lumesule, Pande Swagaswaga na Magofu ya Kilwa.

Kamishna Nyanda pia amesema, mafanikio mengine ni pamoja na ujenzi wa malango matano (5) na vituo vinne (4) vya kukusanyia mapato katika Mapori ya Akiba ya Wamimbiki, Mkungunero, Lukwika Lumesule, Swagaswaga, Mpanga Kipengere, Kijereshi na katika Pori Tengefu Ziwa Natron,

Ujenzi wa njia ya waenda kwa miguu zenye urefu wa kilometa 3.7 katika Pori Tengefu Ziwa Natron, na Mapori ya Akiba Swagaswaga, Kilwa Kisiwani  na Mpanga Kipengere,

Miundombinu mingine iliyoimariswa ni ukarabati wa mabanda sita (6) ya Utalii katika Pori la Akiba Wamimbiki.

Aidha Kamishna Nyanda amesema kumekuwepo na ongezeko la Wawindaji kutoka 355 mwaka 2020/21 hadi wawindaji 787 mwaka 2022/23 na wawindaji 481 hadi Februari mwaka 2024, lakini pia kuongezeka kwa idadi za meli za Kimataifa za utalii kutembelea eneo la Kihistoria Kilwa.

Kamisha wa Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Kamishna Mabula Misungwi Nyanda.

Kamisha wa Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Kamishna Mabula Misungwi Nyanda.

Kamisha wa Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Kamishna Mabula Misungwi Nyanda.




Viongozi wa juu wa TAWA, na mwakilishi wa TEF, Bw. Nevile Meena
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia wasilisho hilo.
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia wasilisho hilo.
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia wasilisho hilo.
Baadhi ya Wahariri wakifuatilia wasilisho hilo.
Bw. Sabato Kosuri, kutoka ofisi ya Msajili wa Hazina, akielezea dhima ya kikao hicho.
Baadhi ya maofisa wa TAWA