Posts

Showing posts from October, 2021

JK AFUNGUA TAMASHA LA KIMATAIFA LA SANAA NA UTAMADUNI MJINI BAGAMOYO

Image
Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Mhe. Jakaya Mrisho  Kikwete akifunga Tamasha la Kimataifa la Sanaa na Utamaduni la Bagamoyo Oktoba 30, 2021.  

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAPILI OKTOBA 31, 2021

Image
 

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAMOSI OKTOBA 30, 2021

Image
 

MAJALIWA: MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI KEMEENI RUSHWA

Image
 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaagiza Mawaziri na Naibu Waziri wasimamie taasisi na idara zilizopo chini ya wizara zao ili zizingatie vigezo vyote vya utawala bora pamoja na kukemesha vitendo vya rushwa ambavyo ndio adui mkubwa wa utawala bora. “Ninapenda kuwakumbusha kuwa ninyi ni nyenzo muhimu katika utendaji wa Serikali, hivyo wazembe, wezi na wabadhirifu waliopo chini ya mamlaka zenu lazima wote wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Serikali. Kila kiongozi lazima awe makini muda wote.” Waziri Mkuu ametoa maagizo hayo leo (Ijumaa, Oktoba 29, 2021) wakati alipofungua Mafunzo ya Uongozi kwa Mawaziri na Naibu Mawaziri katika Ukumbi wa Mtakatifu Gasper jijini Dodoma. Mafunzo hayo yameandaliwa na Taasisi ya Uongozi. Amesema lengo la mafunzo hayo ni kupanua uelewa wa Mawaziri na Naibu Mawaziri kuhusu masuala mbalimbali ya uongozi ikiwa ni pamoja na kuelewa majukumu, madaraka na mipaka ya nafasi zao, kuongoza watu, kufanya maamuzi ya kimkakati na kuboresha sifa bi

WAZIRI MAKAMBA AWASILISHA UJUMBE WA RAIS SAMIA KWA SERIKALI YA ALGERIA

Image
Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Mhe. Aymen Benabderrahmane mara baada ya kukabidhi ujumbe maalumu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Serikali ya Algeria.  * Asisitiza juu ya ushirikiano katika sekta ya nishati NA MWANDISHI MAALUM Ziara ya Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba nchini Algeria imefungua kurasa zilizokuwa zimefungwa kwa muda mrefu za ushirikiano baina ya Tanzania na Algeria ikiwa ni nchi marafiki tangu enzi za ukombozi wa Afrika.  Waziri Makamba ametembelea Algeria kwa lengo la kukuza uhusiano wa kisekta na pia kuwasilisha ujumbe maalumu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria. Waziri wa Nishati, Mhe. January Makamba akiwa katika mazungumzo na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Algeria, Mhe. Aymen Benabderrahmane mara baada ya kukabidhi uju

WAZIRI WA KILIMO PORF ADOLF MKENDA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MKAZI WA USAID BI KATE SOMVONGSIRI JIJINI DODOMA

Image
  Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda akifurahia jambo pamoja na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Bi Kate Somvongsiri mara baada ya kumaliza mazungumzo katika Ofisi za Wizara ya Kilimo zilizopo Jijini Dodoma, tarehe 28 Octoba 2021. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo) Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Bi Kate Somvongsiri akimkabidhi zawadi mwenyeji wake  Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda  mara baada ya kumaliza mazungumzo kuhusu ushirikiano katika sekta ya Kilimo katika Ofisi za Wizara ya Kilimo zilizopo Jijini Dodoma, tarehe 28 Octoba 2021. Waziri wa Kilimo Mhe Prof Adolf Mkenda akimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID) Bi Kate Somvongsiri mara baada ya kujadili kwa kina juu ya ushirikiano wa sekta ya kilimo katika kikao kazi kilichofanyika Ofisi za Wizara ya Kilimo zilizopo Jijini Dodoma, tarehe 28 Octoba 2021. Waziri wa Kilimo Mh

WAZIRI MHAGAMA AKEMEA UTORO WA DAWA KWA WAVIU

Image
NA. MWANDISHI WETU Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama amekea vitendo vya baadhi ya watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI nchini kukwepa na kusitisha matumizi ya dawa za kupunguza makali ya ugongwa huo huku wakipatwa na madhara zaidi. Ametoa kauli hiyo alipotembelea na kukagua shughuli za watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kutoka katika Konga Jiji Mbeya, kukagua ujenzi wa Kituo cha Tiba na Matunzo (CTC) Chimala pamoja na ujenzi wa Kituo cha Tiba na Matunzo cha Zahanati ya Igawa Mbarali oktoba 27, 2021 Jijini Mbeya. Waziri alieleza kuwa, kumekuwa na kesi za watu kutoroka na kusitisha matumizi ya dawa hizo huku akieleza kuwa ni changamoto inayokwamisha mapambana dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI. “Wanaoishi na VVU wote acheni kutoroka dawa bali endeleeni kutumia dawa hizo ili kuendelea kufubaza makali na kuwa afya njema,”alisema waziri Mhagama Alisema ni wakati sasa jamii kuwa na uelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wa

UJERUMANI YAIPATIA TANZANIA MSAADA MWINGINE WA SH. BILIONI 119 NDANI YA SIKU NNE

Image
  Na Benny Mwaipaja, Dar es Salaam SERIKALI ya Ujerumani imeipatia Tanzania msaada mwingine wa Euro milioni 45 sawa na takribani shilingi za Tanzania bilioni 119.2 kwa ajili ya kutekeleza miradi mitatu katika sekta za maji, afya na kuendeleza sekta ya maliasili na utalii. Msaada huo umekuja siku mbili tangu nchi hiyo iingie makubaliano mengine ya kutoa msaada wa kiasi cha Euro  milioni 71 sawa na zaidi ya shilingi bilioni 190.5, kwa ajili ya kutekeleza miradi kadhaa ikiwemo maji, uendelezaji wa maliasili na utalii, afya ya mama na mtoto pamoja na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia. Akizungumza baada ya kusaini mikataba hiyo mipya mitatu kwa niaba ya Serikali, na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Mheshimiwa Regine Hess kwa niaba ya Ujerumani, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Tutuba, alisema kuwa fedha hizo zitaisaidia nchi kukabiliana na athari za Uviko 19, kuboresha uhifadhi wa mazingira na huduma za jamii. Alisema kuwa Mkataba wa kwanza uliosainiwa unahusisha