Posts

Showing posts from March, 2021

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AMTEUA BALOZI HUSSEIN A. KATTANGA KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI

Image
NA K-VIS BLOG RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amemteua Balozi wa Tanzania nchini Japan, Mhe. Hussein A. Kattanga kuwa Katibu Mkuu Kiongozi kuchukua nafasi ya aliyekuwa akishika wadhifa huo Balozi Dkt. Bashiru Ali Kakurwa ambaye ameteuliwa kuwa Mbunge. Rais amefanya mabadiliko hayo wakati wa hafla ya kuapishwa kwa Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Mpango Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma Machi 31, 2021. Rais pia amefanya mabadiliko kwenye baraza la Mawaziri ambapo Mhe. Mwigulu Nchemba ameteuliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango akitokea wizara ya Sheria na Katiba. Rais amemuhamisha Mhe. Ummy Mwalimu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na kumpeleka Ofisi ya Rais-TAMISEMI, huku aliyekuwa Waziri kwenye ofisi hiyo Mhe., Selemani Jafo amehamishiwa Ofisi ya Makamu wa Rais. Waziri wa Mambo ya Nje, Profesa Palamagamba Kabudi amehamishiwa Wizara ya Sheria na Katiba ambapo Waziri wa Mambo ya Nje sasa atakuwa Balozi Liberata Mulamula ambaye awali aliteuliwa na Rai

DKT. PHILIP MPANGO AAPISHWA KUWA MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA

Image
DKT. Philip Isdor Mpando ameapishwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma leo Alasiri Machi 31, 2021. Mhe, Mpango ameapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Juma mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.  Pia katika hafla hiyo Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar  MheHemed Suleiman na Spika wa Bunge Mher. Job Ndugai sambamba na viongozi wa juu wa serikali. Dkt. Mpango alikuwa WAZIRI wa Fedha na Mipango na Mbunge wa Jimbo la Buhigwe mkoani Kigoma kabla ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan hajamteua kushika wadhifa huo.  

BUNGENI DODOMA MACHI 31, 2021

Image
Waziri Mkuu,  Mheshimiwa  Kassim Majaliwa leo Machi 31, 2021 ameshiriki Mkutano wa Tatu, Kikao cha Pili cha Bunge jijini Dodoma. Pichani ni matukio mbalimbali ya Waziri Mkuu Bungeni.(Picha na OWM).  

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATANO MACHI 31, 2021

Image
 

MAKAMU WA RAIS MTEULE AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

Image
  Na Josephine Majura na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma. Makamu wa Rais Mteule, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango, amekutana na Watumishi wa Wizara ya Fedha na Mipango na kuwasisitiza kuendelea kufanya kazi kwa bidii kutokana na umuhimu wa Wizara hiyo katika maendeleo ya nchi. Mheshimiwa Philip Isdor Mpango, ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa Waziri wa Fedha na Mipango, alitoa rai hiyo jijini Dodoma alipokutana na watumishi wa Wizara hiyo katika ofisi zilizopo Treasury Square, akitokea bungeni baada ya kuteuliwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Bunge kuthibitisha uteuzi wake kwa kura za kishindo. Dkt. Mpango amewataka watumishi wa wizara hiyo kuendelea kufanya kazi kwa weledi kwa kuwa wizara hiyo ni moyo wa Serikali na kwamba wasipofanya kazi vizuri na kwa uaminifu hakuna miradi ya maendeleo itakayotekelezwa, mishahara haitapatikana wala mikopo itakayokopwa hivyo kukwamisha maendeleo ya wananchi. Alisema hana shaka na uwezo wa viongozi na wataalam

TMA YAWATOA UKUNGU WAANDISHI WA HABARI KUHUSU UTABIRI WA HALI YA HEWA NA TAFITI

Image
Ladslaus Chang"a Mkurugenzi wa Huduma za Utafiti na Matumizi Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) akifungua semina ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari kuhusu taarifa mbalimbali za utabiri wa Hali ya hewa tafiti na matumizi ya taarifa hizo inayofanyika kwenye ukumbi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) Kibaha Mkoani Pwani. Monica Mutoni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali katika semina ya waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari kuhusu taarifa mbalimbali za utabiri wa Hali ya hewa tafiti na matumizi ya taarifa hizo inayofanyika kwenye ukumbi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) Kibaha Mkoani Pwani. Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada katika semina hiyo kuhusu taarifa mbalimbali za utabiri wa Hali ya hewa tafiti na matumizi ya taarifa hizo inayofanyika kwenye ukumbi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) Kibaha Mkoani Pwani. Kulia ni Joyce Makwata Mchambuzi