MBUNGE wa Viti Maalumu CCM (NGOs Tanzania Bara) Neema Lugangira akizungumza wakati wa Uzinduzi wa Wiki ya Azaki imefanyika Jijini Dar es Salaam Julai 29 Julai 2021 |
7/31/2021
MHANDISI MASAUNI ARIDHISHWA NA UTENDAJI WA SHIRIKA LA BIMA LA TAIFA
NAIBU Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni, amelipongeza Shirika la Bima la Taifa (NIC) kwa kuongeza ufani na kuboresha utendaji kazi wa Shirika hilo na kufanikiwa kuongeza kiwango cha uwekezaji kutoka sh. bilioni 85 mwaka 2018/2019 hadi kufikia shilingi bilioni 245 Mwaka 2020/2021.
Mhandisi Masauni ametoa pongezi hizo alipotembelea Makao Makuu ya Shirika la Bima la Taifa Jijini Dar es Salaam na kufanya mazungumzo na Menejimenti ya Shirika hilo ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kutembelea Taasisi zote zilizochini ya Wizara ya Fedha na Mipango, baada ya kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Wizara hiyo.
“Moja ya eneo lililonivutia ni namna Shirika hili lilivyoboresha huduma zake na mapato kwa kutumia mifumo ya TEHAMA, kutoka asilimia 10 za miaka ya nyuma hadi kufikia asilimia 95 katika kipindi cha miaka miwili tu iliyopita” Alisema Mhe. Masauni
Ameuagiza uongozi wa Shirika hilo kuongeza ubunifu na bidii zaidi na kuhakikisha kuwa linakuwa Shirika bora zaidi la Bima hapa nchini, Ukanda wa Afrika Mashariki na nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Aidha, alitoa wito kwa wananchi kutumia huduma za Bima zinazotolewa na Shirka hilo la Umma na kuahidi kuwa Wizara ya Fedha na Mipango itaendelea kuliunga mkono na kulisaidia liweze kutimiza malengo yake ya kuwahudumia wananchi kikamilifu.
Akitoa taarifa ya utendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC), Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Dkt. Elirehema Doriye alisema katika kipindi kifupi cha miaka miwili iliyopita ambacho NIC imefanya mageuzi na mabadiliko makubwa ya uendeshaji wa Shirika, Shirika limewekeza kiasi hicho cha shilingi bilioni 245 sawa na ufanisi wa silimia 136.05.
“Katika kipindi hicho pia Shirika limelipa madai mbalimbali ya Bima ya Maisha yaliyohakikiwa kwa wateja wetu, kiasi cha shilingi bilioni 15.8 kati ya shilingi bilioni 22.53 ambazo shirika linadaiwa, hatua iliyosababisha kurejea kwa imani ya wateja na kuvutia wateja wapya kujiunga na huduma zinazotolewa na Shirika, na tunatarajia kulipa madeni yote kabla ya mwaka 2021 kuisha” Alisema Dkt. Doriye
Dkt. Doriye alimweleza Mhe. Masauni kwamba Shirika lake pia linazidai Taasisi na Mashirika mbalimbali ya Umma ambazo hazijalipia Bima za Maisha za mali zao kiasi cha shilingi bilioni 34.42 na kwamba fedha hizo zikipatikana zitaongeza mtaji wa Shirika na uwezo wa kuwahudumia wateja wao.
Aidha, alisema kuwa NIC inaandaa bidhaa mpya ikiwemo kuanzisha Bima ya Mifugo na kubuni bidhaa nyingi zaidi za Kilimo ili kuchangia juhudi za Serikali za kuinua sekta za ufugaji, kilimo na viwanda.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (Mb) (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC), Dkt. Elirehema Doriye, wakiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Shirika hilo, alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea taasisi zilizochini ya Wizara ya Fedha na Mipango, jijini Dar es Salaam.
(picha na Wizara ya Fedha na Mipango, Dar es Salaam)
RAIS SAMIA APOKEA NDEGE MPYA AINA YA BOMBADIER DASH 8-Q400 ILIYONUNULIWA NA SERIKALI
USIKIVU WA TBC WAPANDA KWA ASILIMIA 14 NDANI YA MIEZI MIWILI
Mtaalam wa Mitambo akitoa maelezo kwa viongozi mbalimbali waliohudhuria kwenye ya uzinduzi wa Kituo cha kurushia matangazo ya Redio ya TBC eneo la Kisaki - Morogoro leo Julai, 2021.
SERIKALI ITAHAKIKISHA ZAO LA MKONGE LINAIMARIKA-RC MALIMA
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Adam Malima akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua ukarabati wa Mashine za kuchakata mkonge ambapo awali zilikua chakavu hali iliyokua ikisababisha kushuka kwa uzalishaji wa zao la Mkonge.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF) Balozi Alli Siwa akizungumza |
Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Sisalana Elizaberth Kalambo akielezea jambo |
SERIKALI Mkoani Tanga imesema itahakikisha zao la Mkonge linaimarika kutokana na ongezeko la mahitaji ya bidhaa zitokanazo na zao hilo duniani yanayolenga kuachana na matumizi ya bidhaa za Plastiki ambazo zina athari kwa Jamii.
Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Adam Malima wakati wa ziara yake ya kukagua ukarabati wa Mashine za kuchakata mkonge ambapo awali zilikua chakavu hali iliyokua ikisababisha kushuka kwa uzalishaji wa zao la Mkonge.
Mkuu huyo wa mkoa alisema kwa miaka mingi nguzo ya uchumi ya Mkoa huo ilikuwa zao la Katani na miaka 50 iliyopita Tanga ilikuwa inazalisha tani 150,000 lakini baada ya marekebisho na nguvu kubwa mkoa wa Tanga inazalisha tani 35000.
Alisema hivi sasa Serikali ya Tanzania chini ya Rais Samia Suluhu imeweka mkakati wa makusudi wa kuzalisha zao la Mkonge Kitaifa kutoka Tani 35,000 hadi kufikia Tani 120,000.
Aidha alisema mkakati huo unasimamiwa na Waziri Mkuu Kasim Majaliwa ambao wakuu wa mikoa na wadau wengine wote wamekuwa ni sehemu ya mpango huo mafanikio yake yapo hapa wilayani Korogwe.
Alisema ili kufikia Tani 100,000 za Mkonge wanaweza kufikia huko kwa kushirikiana na wawekezaji wakubwa wakiwemo Mohamed Interprises Limited, Amboni Platation,
Kwale, Palet.
Mkuu huyo wa mkoa aliekeza lakini bodi inajua na ina maelekezo ya Waziri Mkuu na Serikali juu ya mkakati huo maana yake wanataka kuwa na uzalishaji wa mkonge mkulima ashiriki kama mmiliki wa uzalishaji huo na sio kama manamba na namna ya kufanya hivyo ni kupitia kwa vyama vya ushirika Amcos kama serikali, Mrajis wa vyama wataanza kuwa na uwezo wa uongozi na rasimali ili iweze kuwa na uzalishaji mkubwa zaidi.
Alisema vyama vya Ushirika (AMCOS) wana ubia katika uzalishaji na Kampuni ya Sisalana ambayo inamilikiwa na Shirika la Hifadhi za Jamii (NSSF) hivyo Sisisala lazima ijengewe uwezo wa kupokea zao linalotoka kwa Mkulima kutokana na kwamba hivi sasa Sisalana wanapokea Tani 6000 kwenye Amcos zote na wana uwezo wa kupokea tani 11000
Aliseam hivyo yeye amefika na timu yake kuweza kutengeneza mkakati ili hizo tani 11000 ziwafikie Sisalana na zipate kuchakatwa na mkulima aweze kupata haki yake pamoja licha ya kwamba huko kuna changamoto za pande zote mbili za Amcos na Sisalana na nyengine ambazo lazima utatuzi wake upatikana kwa Serikali ikiwemo suala la miundombinu inayopitisha
Awali akizungumza Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi za Jamii (NSSF) Balozi Alli Siwa alisema sheria ya kuanzishwa kwa mfuko huo inawaruhusu kuingia kwenye uwekezaji ndio maana wameshiriki kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa kwenye Corona ambazo zinamilikiwa na Kampuni ya SISALANA ambayo ni kampuni tanzu ya NSSF.
Alisema kampuni hiyo imepewa dhamana ya kuendesha Corona tano kwa madhumuni ya kuweza kurejesha fedha za wanachama ambapo wanaendesha shughuli za biashara hiyo kwa kushirikiana na Amcos kazi yao kubwa ni kuchakata majani ya katani ili Amcos ziweze kuuza brashi ambayo inaitwa Singa na wao wanaweza kupata tozo kwa ajili ya kuchakata.
Alisema hilo limewapelekea kwenye biashara ya mkonge na kwao hiyo haitoshi kuchakata kutokana na kwamba itawachelewesha kurudisha fedha zao wanazotaka kuzipata na pili wanataka biashara hiyo iwe na maana katika kutunishia mfuko wa Pensheni ili waweze kuwa na uwezo mkubwa wa kulipa pensheni kila inapohitajika kwa wanachama wao.
Naye kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Sisalana Elizaberth Kalambo alisema walianza kazi yao kwa kufanya ukarabati katika mitambo katika kiwanda cha Usambara na baada ya hapo watahamia Mwelya ili kuhakikisha mitambo inakuwa katika hali nzuri.
Alisema wakati wanafanya ukarabati na matengenezo kwenye mitambo hivyo wanaomba wakulima wa mkonge wanaosimamiwa na Amcos tano za Mwelya, Magoma, Hale, Ngombezi na Magunga wanaomba wakulima wawape ushirikiano ili waweze kufanya maboresho.
Alisema kwa sababu wanapofanya matengenezo makubwa wanasimamisha uzalishaji kwa muda wa usipoungua wiki mbili mpaka tatau hivyo wanasisitiza kwa wakulima waongeze kasi ya upelekaji wa majani kwa kupeleka awamu mbili ili kuepuka hasara watakazokutana nazo wakati wanaposimamisha uzalishaji kwa siku hizo.
7/30/2021
RC KUNENGE AWAONGOZA WANANCHI MKOA WA PWANI KUCHANJA CHANJO DHIDI YA UVIKO 19 MJINI KIBAHA
MKUU wa mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amepata chanjo ya UVIKO 19 leo Julai, 30 2021. Akichanjwa chanjo hiyo katikà viwanja vya kituo cha Afya Mkoani, kilichoko Kibaha Mjini, Mhe. Kunenge amewaasa Wanachi wa Mkoa huo kuwa ugonjwa upo na kuwataka kuchukua tahadhari wakati wote, amewataka Kuvaa barako, kunawa mikono kwa maji tiririka na kuepuka mikusanyiko isiyo ya lazima.
Amemshukuru Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuonyesha njia kwa kupata chanjo. "nimechanja kwa hiari yangu mwenyewe mpaka sasa najisikia vizuri sijaona shida yeyote," alisema RC KUNENGE na kuongeza......Wananchi waje wachanje kwa hiari yao tunachotafuta ni salama tumepata chanjo kidogo tunaendelea kuratibu upatikanaji wa nyingi zaidi na tutaitoa bila usumbufu na bila malipo. "Chanjo hii kwa sasa itatolewa kwa makundi ya Kipaumbele kama vile watoa huduma ya afya, watu wenye umri kuanzia miaka 50 na kuendelea kama ambavyo muongozi wa Wizara ya Afya kuhusu Chanjo hiyo unavyosema.
RAIS SAMIA AKUTANA NA MJUMBE WA RAIS FELIX TSHESEKEDI WA DRC IKULU DAR ES SALAAM
JK ACHUKUA "USUKANI" TAASISI YA MFUKO WA WASHIRIKA WAFADHILI WA ELIMU DUNIANI (GPE)
Viongozi, Rais Uhuru Kenyata wa Kenya, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mhe. Simai Mohammed Said na Viongozi kutoka nchi mbalimbali wakiwa katika Mkutano Mkuu wa Mfuko wa Washirika Wafadhili wa Elimu Duniani ( GPE) uliofanyika London ,Uingereza
Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete ni Mwenyekiti wa Mfuko wa Washirika Wafadhili wa Elimu Duniani -Global Partnetship in Education (GPE).
RAIS MSTAAFU KIKWETE AHUDHURIA MKUTANO WA KIMATAIFA UNAOJADILI MASUALA YA ELIMU