Posts

Showing posts from August, 2021

SERIKALI YASHUSHA TOZO ZA MIAMALA YA SIMU KWA ASILIMIA 30%

Image
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Mwigilu Nchemba.  

WAZIRI MKUU AZINDUA TAWI LA BENKI YA MWANGA NA KUTOA MAAGIZO SABA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Tawi la Benki ya Mwanga Hakika jijini Dodoma, Agosti 31, 2021. Wengine pichani kutoka kushoto ni Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda, Waziri wa Viwanda na Biashara, Profesa Kitila Mkumbo, Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo, Ridhiwani Mringo, Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Benard Kibessa na kulia ni Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo Jagjit Singh. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).   Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua Tawi la Benki ya Mwanga Hakiki jijini Dodoma, Agosti 31, 2021.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt Benard Kibessa (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Bodi ya Benki ya Mwanga Hakika, Ridhiwani Mringo tawi la Dodoma, baada ya kuzindua tawi hilo Agosti 31, 2021.Kushoto ni Waziri wa Habari, Utama

MAJALIWA: SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA.

Image
  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa   akiongozwa na Inspekta Jenerali wa Polisi Simon Sirro (katikati) na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida ACP Stella Mutabihirwa  (kulia) wakati wa ufunguzi wa majengo ya Makao Makuu ya Polisi Mkoa na Ofisi ya Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Mkoa wa Singida, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Agosti 30, 2021 amefungua majengo ya Ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Singida na Ofisi za Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Mkoa wa Singida, miradi ambayo imegharimu shilingi bilion 1.314 Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Waziri Mkuu amesema kuwa amefurahishwa na mradi huo ambao ujenzi wake umetumia muda mfupi na umeokoa kiasi kikubwa cha fedha za Serikali. Ameahidi kuwa serikali itaendelea kuimarisha miundombinu ya vyombo vya ulinzi na usalama. “Nawapongeza sana wasimamizi wa mradi huu kwa kuhakikisha unatekelezwa vema na kuakisi thamani ya fedha za mradi yaani  value for money  sanjari na kukamilika kwa wakati.  Tumeelezwa hapa kuwa mradi huu uliotekelezwa kw

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE AGOSTI 31, 2021

Image
 

RC KUNENGE AHUZUNISHWA NA AJALI YA MOTO ILIYOTEKETEZA NYUMBA 19 HUKO RUFIJI

Image
NA MWANDISHI WETU PWANI. Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amehuzunishwa na tukio la ajali ya moto uliopelekea nyumba zaidi ya 19 kuteketea kabisa kwa moto kwenye Kitongoji cha Shaurimoyo, Kijiji cha Nyamwage Wilayani Rufiji. Ajali hiyo imetokea baada ya mwananchi mmoja aliyekuwa  akisafisha shamba lake kwa kuchoma moto na moto huo kuwa mkubwa hali iliyopelekea kushindwa kuudhibiti na hivyo kuunguza nyumba. Akizungumza kwenye eneo hilo la tukio usiku wa kuamkia leo Agosti 30, 2021 akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, ameagiza serikali ya wilaya kufanya tathmini kwa haraka ili kujua ukubwa wa athari iliyosababishwa na ajali hiyo na hivyo msaada unaohitajika utolewe haraka.  "Nimehuzunishwa sana na ajali hii na niwape pole wote mlioathirika na moto huu, na pia nawapongeza sana wananchi waliochukua hatua za haraka kwa kuwahifadhi na kuwasaidia wanakijiji wenzenu," alisema RC Kunenge na kuongeza.....naagiza tathmini ifanyike kwa haraka ili tujue namna ya kuwasa

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU AGOSTI 30, 2021

Image
 

SERIKALI YAENDELEA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU MATUMIZI YA TIBA ASILI NCHINI.

Image
Na WAMJW- DOM  Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  imeendelea na zoezi la kutoa Elimu kwa wananchi katika maeneo ya kutolea huduma za Afya juu ya umuhimu wa matumizi ya tiba asili/mbadala katika mapambano dhidi ya magonjwa mbali mbali, ikiwemo UVIKO-19.  Katika kuelekea maadhimisho ya siku ya tiba asili ya mwafrika Wadau wa tiba asili wakiongozwa na kitengo cha Tiba asili na Baraza la tiba asili kutoka wizara ya afya wameweza kutembelea na kutoa elimu katika  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Dodoma, kituo cha Afya cha Makole na Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma. Akiongea wakati wa utoaji elimu hiyo Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Tiba Asili/Mbadala  Dkt. Vumilia Liggie alisema kuwa, Wataalamu wa Tiba asili na tiba mbadala kutoka Wizarani wameongozana na Waganga wa tiba hizo kutembelea vituo vya Afya katika sehemu ya wagonjwa wa nje wa Hospitali (OPD) ambapo wameweza kuzungumza na wagonjwa na kuwapa elimu kuhusu umuhimu wa tiba asili katika mapambano dhidi ya magonjw