RC KUNENGE AHUZUNISHWA NA AJALI YA MOTO ILIYOTEKETEZA NYUMBA 19 HUKO RUFIJI

NA MWANDISHI WETU PWANI.

Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge amehuzunishwa na tukio la ajali ya moto uliopelekea nyumba zaidi ya 19 kuteketea kabisa kwa moto kwenye Kitongoji cha Shaurimoyo, Kijiji cha Nyamwage Wilayani Rufiji.

Ajali hiyo imetokea baada ya mwananchi mmoja aliyekuwa  akisafisha shamba lake kwa kuchoma moto na moto huo kuwa mkubwa hali iliyopelekea kushindwa kuudhibiti na hivyo kuunguza nyumba.

Akizungumza kwenye eneo hilo la tukio usiku wa kuamkia leo Agosti 30, 2021 akiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, ameagiza serikali ya wilaya kufanya tathmini kwa haraka ili kujua ukubwa wa athari iliyosababishwa na ajali hiyo na hivyo msaada unaohitajika utolewe haraka. 

"Nimehuzunishwa sana na ajali hii na niwape pole wote mlioathirika na moto huu, na pia nawapongeza sana wananchi waliochukua hatua za haraka kwa kuwahifadhi na kuwasaidia wanakijiji wenzenu," alisema RC Kunenge na kuongeza.....naagiza tathmini ifanyike kwa haraka ili tujue namna ya kuwasaidia wenzetu hawa." Alisisitiza.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele ameeleza kuwa hakuna vifo wala majeruhi kutokana na ajali hiyo, licha ya kwamba moto umetekeleza kila kitu.

Wilaya ilichukua hatua mara moja baada ya kutokea tukio hilo na kutoa rai kwa wakazi wa wilaya hiyo kuwa makini wakati wanachoma moto kwani kwa sasa ni kipindi cha upepo mkali, alisema Mkuu huyo wa wilaya.

Wananchi wa eneo hilo nao wameeleza tukio jinsi lilivyowaathiri hivyo kuomba serikali kuweza kuwasaidia kwa haraka maana hawana mahala pa kuishi.









Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"