CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"
NA MWANDISHI WETU NA MASHIRIKA YA HABARI
KOCHA
mpya wa Simba, Pablo Franco Martin, mzaliwa wa Madrid, nchini Hispania, ndiye
kocha mwenye CV iliyosheheni kuwahi kutokea katika historia ya soka hapa
nchini.
Pablo
Franco, alizaliwa Juni 11, 1980 katika jiji la Madrid, na hadi “Anatangazwa kuja” kwa Wekundu wa Msimbazi
Simba, kocha huyo ana leseni ya UEFA Pro Licence ambayo inaelezwa
kuwa ndiyo leseni inayotolewa kwa muhitimu wa mafunzo ya juu kabisa ya Ufundishaji (Coaching) na Usimamizi (Managerial) wa wa soka barani Ulaya.
Kocha
huyo kijana ni miaka minne tu iliyopita alikuwa akifanya kazi na Kocha mwenye
mafanikio makubwa Duniani kwenye mpira wa miguu akiwa kama mchezaji na kocha, Maestro
Zinedine Zidane “Zizou” kwenye
Klabu ya Real Madrid ya Uhispania kama
kocha msaidizi.
Kocha
Pablo mbali na kuiongoza Real Madrid kam Kocha Msaidizi, aliwahi pia kufundisha
timu za Getafe CF na Getafe B zote za Hispania, pia timu za Club Deportivo
Santa Eugenia, Club Deportivo Illescas, Club Deportivo Puertollano zote za huko
huko Hispania na FC Saburtalo ya Georgia.
Kocha huyo ana shahada ya juu ya kufundisha mbinu za mpira wa miguu, utimamu wa mwili wa mwanasoka na jinsi ya kuusoma na kuuchambua mpira wa soka timu zinapokuwa uwanjani.
Kocha
Pablo anakuja Simba SC ikiwa nafasi ya pili na alama 11 kwenye msimamo wa Ligi
Kuu Soka Tanzania Bara (NBC Premier League) msimu huu wa 2021-2022,ikiwa ndiyo
timu pekee kwenye ligi ambayo haijafungwa bao hata moja.
Hata
hivyo kumekuwepo na manung’uniko kutoka kwa baadhi ya washabiki wa timu hiyo
kuwa kutokana na ukubwa wake na wachezaji ilio nao haistahili kuwa hapo ilipo
na hasa ukizingatia haikuwa na wakati mzuri kwenye Pre-Seson, na michuano ya
Ligi ya Mabingwa ambapo licha ya kupata ushindi wa ugenini w amabao 2-0 dhidi ya
Jwaneng Galaxy ya Botswana, ilikuja kuchapwa mabao 3-1 kwenye uwanja wa
nyumbani wa Benjamin Mkapa na kutolewa kwenye michuano hiyo ya mwaka huu ya
Ligi ya Mabingwa barani Afrika.
Kazi
kubwa ambayo kocha huyo Mhispania anatarajiwa kuifanya ni kuhakikisha Simba
ambayo ni mabingwa mara nne wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara na kwa sasa
anatete taji hilo inarejea kwenye hadhi yake ya kutandaza mpira kwa pasi za
uhakika na kupata matokeo yatakayoiwezesha kufanya vizuri kwenye michuano ya
Kombe la Shirikisho.
Comments
Post a Comment