MHE. JENISTA AWATAKA WATUMISHI WA OFISI YAKE KUTOA USHIRIKIANO WA KIUTENDAJI KWA VIONGOZI WAPYA ILI KUENDELEA KUUBORESHA UTUMISHI WA UMMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akizungumza na watumishi wa ofisi yake kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wake Mhe. Ridhiwani Kikwete (wa kwanza kulia) kuzungumza na watumishi hao mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, Bw. Juma Mkomi.

Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi (wa pili kutoka kushoto) akipokea taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya ofisi yake kutoka kwa mtangulizi wake, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa kwanza kulia) mara baada ya Bw. Mkomi kuripoti rasmi katika ofisi hiyo iliyopo Mtumba jijini Dodoma. Wanaoshuhudia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma aliyemaliza muda wake, Dkt. Laurean Ndumbaro (wa kwanza kulia) akitoa neno la shukurani kwa watumishi wa ofisi hiyo alipokuwa akiwaaga. Wengine ni viongozi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akimkaribisha Naibu Waziri wa ofisi yake, Mhe. Ridhiwani Kikwete mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akimkaribisha Katibu Mkuu wa ofisi yake Bw. Juma Mkomi mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma baada ya kuteuliwa na kuapishwa na Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-UTUMISHI. Nyuma ya Mhe. Waziri Jenista ni Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Bw. Xavier Daudi.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Maadili, Bi. Leila Mavika mara baada ya Naibu waziri huyo kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi akisalimiana na watumishi wa ofisi hiyo mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama.
 Sehemu ya watumishi wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama wakati akiwakaribisha Naibu Waziri wa ofisi hiyo na Katibu Mkuu mara baada ya kuripoti rasmi katika ofisi hizo zilizopo Mtumba jijini Dodoma.

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"