WATUMIAJI HUDUMA NDOGO ZA FEDHA WAASWA KUTUMIA HUDUMA HIYO KWA TAASISI ZILIZOSAJILIWA

 NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

WATUMIAJI wa Huduma ndogo za fedha wameaswa kutotumia huduma kwa mtu au taasisi ambayo haijasajiliwa na Benki Kuu ya Tanzania.

Hayo yamesemwa na Kaimu Msimamizi wa Huduma Ndogo za fedha BoT, Bi. Mary Ngasa wakati wa majadiliano baada ya kuwasilisha mada “Usimamizi wa Huduma Ndogo za Fedha, (Microfinance Supervision)” kwenye semina ya siku moja kwa Wahariri wa vyombo vya habari kuhusu masuala ya Fedha na Uchumi iliyoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) jijini Dar es Salaam Februari 27, 2023.

Alisema hadi sasa kuna jumla ya taasisi za watoa huduma ndogo za fedha zinazofikia 1,000 ambazo zimesajiliwa na BoT, Tanzania Bara.

Akifafanua alisema “Ibara ya 12 ya Sheria hiyo imeipa mamlaka Benki Kuu ya Tanzania Kusajili, Kusimamia na Kudhibiti biashara ya huduma ndogo za Fedha Tanzania Bara, lengo kuu hasa ni kuwasaidia wananchi kuepuka changamoto za udanganyifu zilizokuwa zikiwakumba kabla ya kuanzishwa kwa sheria.” Alifafanua

Alisema Ibara ya 16 ya Sheria hiyo imetoa katazo kwa mtu au taasisi yeyote kufanya biashara ya kutoa huduma ndogo za fedha bila kuwa na leseni iliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania inayoruhusu kufanya biashara hiyo.” Alifafanua na kuongeza

“Tuwe na mazoea ya kuwafahamu watoa huduma ndogo za fedha kabla ya kufikwa na matatizo, kuna haki za msingi ambazo mwananchi anapaswa kuzifahamu ili kuepuka udanganyifu.” Aliasa.

Bi. Mary Ngasa alisema sheria imetoa tafsiri juu ya “huduma ndogo za fedha” kuwa ni biashara inayojumuisha kupokea fedha, kama amana au riba kutokana na amana au mkopo na kuikopesha kwa wanachama au wateja; kupokea amana na kutoa mikopo au huduma ya mikopo kwa wajasiriamali wadogo, kaya au mtu mmoja mmoja.

Aidha amewataka watoa huduma kufuata maelekezo ya BoT na Kanuni zilizowekwa katika uendeshaji wa shughuli zao ikiwa ni pamoja na kutoa hati ya mkataba kwa maandishi kwa watumiaji (wateja) wa huduma.

Kaimu Msimamizi wa Huduma Ndogo za fedha BoT, Bi. Mary Ngasa, akiwasilisha mada.
Wahariri wakifuatilia uwasilishwaji wa mada.







Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"