RAIS SAMIA ATEUA MKUU MPYA WA MAJESHI

 


 NA MWANDISHI WETU

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amirijeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Mhe. Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo Meja Jenerali Jacob John Mkunda(pichani juu) kuwa Jenerali, kisha kumteua kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (Chief of Defence Forces – CDF).

Kabla ya Uteuzi huo alikuwa Mkuu wa Tawi la Operesheni na Mafunzo katika Makao Makuu ya Jeshi (Chief of Operations and Training) na anachukua nafasi ya Jenerali Venance Salvatory Mabeyo ambaye amestaafu kwa mujibu wa sharia.

Rais Samia pia amempandisha Cheo Meja Jenerali Salum Haji Othman kuwa Luteni Jenerali na amemteua kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (Chief of Staff – CofS).

Kabla ya uteuzi huo Meja Jenerali Othman alikuwa Kamishna wa Utafiti na Maendeleo Jeshini (Commissioner for Research and Military Development) katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Vile vile amemteua Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule kuwa Balozi ambapo kabla ya uteuzi huo alikuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Uapisho wa viongozi hao wa juu wa jeshi utafanyika Alhamisi Juni 30, 2022 Ikulu, jijini Dar es Salaam.


Brigedia Jenerali Jacob John Mkunda (aliyesimama) akionekana katika picha hii ambayo ilipigwa katika tarehe ambayo haijulikani wakati huo akichukua nafasi ya kuongoza Brigedi ya Faru akifafanua jambo wakati alipomsindikiza  aliyekuwa kiongozi wa Brigedi ya Faru, Bregedia Jenerali Antony Chacha Sibuti (wapili kulia) katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora kwa ajili ya kuaga mara baada ya kuhamia Makao Makuu ya Jeshi mjini Dodoma. Wengine ni Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu (kulia)  na pembeni ni Mshauri wa Jeshi la Akiba Mkoa wa Tabora Kanali Mussa Luka Simengwa.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiriu Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama, Mhe. Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo na kuwa Jenerali na kisha kumteua kuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi (CDF) leo Juni 29. 2022.


Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"