PSSSF YAWAKARIBISHA WANACHAMA NA WANANCHI KUTEMBELEA BANDA LAO MAONESHO YA SABASABA

 NA MWANDISHI WETU, SABASABA

MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umewaalika wanachama wake na wananchi kwa ujumla kutembeela banda la Mfuko huo kwenye Maonesho ya 46 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yaliyoanza Juni 28, 2022 kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa.

Afisa Uhusuano Mwandamizi wa PSSSF, Bi. Fatma Elhady amesema imekuwa ni fursa nzuri kwa Mfuko kushiriki katika Maonesho hayo ili kuwawezesha Wanachama na wananchi kwa ujumla kupata taarifa za huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko.

“Tunawakaribisha sana Wanachama wetu na wananchi kutembelea Banda namba 13 la Ushirikiano lililoko mtaa wa Mabalozi.” Alisema.

Kauli mbiu ya Maonesho hayo ni "Tanzania Mahali Sahihi Pa Biashara na Uwekezaji."

Afisa wa Kitengo cha Nyaraka, PSSSF, Bw. Gabriel Maro (kushoto), akifafanua jambo kwa Mwanachama wa Mfuko aliyetembelea Banda la Mfuko huo Juni 29, 2022. Katikati ni Afisa Uhusiano Mkuu, PSSSF, Bw. Abdul Njaidi.
Afisa Uhusuano na kwa Wanachama Mkuu wa PSSSF, Bi. Fatma Elhady, na Afisa Uhusiano Mwandamizi,Bi. Coleta Mnyamani wakimsikiliza mwanachama wa Mfuko huo aliyefika kupata huduma.
Afisa Miliki Mwandamizi wa PSSSF, Bi. Vivian Mtatifikolo (kulia), akimuhudumia mwanachama wa Mfuko.
Afisa Uhusiano Mkuu, PSSSF, Bw. Abdul Njaidi Akitoa elimu ya Hifadhi ya Jamii kwa Mwanachama huyu aliyetembelea Banda la Mfuko huo Leo Juni 29, 2022.
Wafanyakazi wa PSSSF na NSSF, wakiwa eneo la mapokezi kuwahudumia Wanachama na wananchi wanaotembelea Banda hilo la Ushirikiano.
Picha ya pamoja ya kikosi kazi cha PSSSF kilichoweka kambi Sabasaba ili kuwahudumia wanachama na wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"