PSSSF YAPOKEA GAWIO LA BILIONI 11.85 KUTOKA CRDB KWENYE UWEKEZAJI WA HISA
Waziri
wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekabidhi gawio lenye
thamani ya Shilingi bilioni 11.85 kwa
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa PSSSF CPA Hosea Kashimba kwa
niaba ya Mfuko, kwenye hafla fupi iliyofanyika leo jijini Dodoma.
Akikabidhi
hundi hiyo Mhe. Mchemba amesema,
"nimefurahishwa pia kuona taasisi na mashirika mbalimbali ya Serikali,
Halmashauri, pamoja na vyama vya ushirika wanapokea gawio la jumla ya Shilingi
bilioni 16.4. Hii inafanya jumla kuu ya gawio tunalolipokea leo kuwa Shilingi
bilioni 36.1. Ni jambo la kujivunia sana kwa Benki yetu ya kizalendo".
Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA Hosea Kashimba
Mkurugenzi wa Fedha, PSSSF, Bi. Beatrice Musa-Lupi (wakwanza kushoto) akiungana na maafisa wengine kwenye hafla ya kupokea gawio kutoka benki ya CRDB jijini Dodoma Juni 29, 2022.
Comments
Post a Comment