CCM WANA JAMBO LAO UWANJA WA JAMHURI JIJINI DODOMA LEO.
NA SAID MWISHEHE,MICHUZI TV CHAMA Cha Mapinduzi(CCM)kimesema kesho Agosti 29 mwaka huu wa 2020 wana jambo lao ambalo ni la uzinduzi rasmi wa Kampeni za Mgombea wa Urais wa Chama hicho Dk.John Magufuli huku kikieleza kitatumia nafasi hiyo kuielezea Afrika na Dunia mambo makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ga Tano. Akizungumza leo Agosti 28,2020, katika Uwanja Jamhuri jijini Dodoma ,Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Humphrey Polepole amefafanua maandalizi yote kuelekea uzinduzi wa kampeni za mgombea Urais na ratiba itaanza saa moja asubuhi hadi saa 12 jioni. "Watanzania na wana CCM kesho hapa uwanja wa Jamhuri tuna jambo letu tunawakaribisha wote.Kesho tunataka kuisimamisha Tanzania,Afrika na Dunia kwa kuelezea mafanikio ambayo yamepatika katika kipindi cha miaka mitano chini ya jemedari wetu Dk.John Magufuli,"amesema Polepole na kusisitiza watu watafurika uwanjani hapo kuanzia saa 12 asubuhi. Amesema kwamba baada ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC)