CHADEMA YAZINDUA KAMPENI ZAKE MBAGALA ZAKHEM, DAR ES SALAAM
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimezindua rasmi
kampeni zake kwenye uwanja wa Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam Agosti 28,
2020.
Katika uzinduzi huo Mgombea kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, kupitia chama hicho, Tundu Lissu pamoja na mgombea mwenza wake,
Salum Mwalimu walihutubia katika wafuasi wa chama hicho na wananchi
waliokusanyika katika viwanja hivyo.
Kampeni hizo zitaendelea hadi Oktoba 27, 2020 na uchaguzi
utafanyika Oktoba 28, 2020 ili kumchagua Rais wa Jamhuri, ya Muungano wa
Tanzania, Wabunge na Madiwani.
Comments
Post a Comment