KATIBU MKUU KILIMO ATEMBEELA KIWANDA CHA KUZALISHA MBOLEA CHA MINJINGU MKOANI MANYARA

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (kulia) akiongea na viongozi wa kiwanda cha mbolea cha Minjingu cha Manyara leo alipowatembelea kukagua uzalishaji.Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda hicho Bw.Tosky Hans

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha mbolea cha Minjingi Bw.Tosky Hans leo alipowasili kiwandani hapo mkoani Manyara kwa ziara ya kukagua hali ya uzalishaji mbolea.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (kushoto ) akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa kiwanda cha Kahela Feeders cha Arusha Bw.Alex Kahela ( kulia) kuhakikisha anasajili bidhaa zake kwenye mamlaka za ubora ili zitambulike kwenye soko .(Picha na habari Wizara ya Kilimo)

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya akiwa ameshika chupa ya mbolea ya maji (Booster) inayozalishwa na kiwanda cha Keen Feeders cha Arusha leo alipotembelea.Akiwa kiwandani hapo ameagiza bidhaa zote hizo zisajiliwe na kupata nembo ya ubora kabla hazijaingizwa sokoni ili kumlinda mkulima.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya (kulia) akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha Minjingu cha Manyara  Bw.Tosky Hans (kushoto) leo alipotembelea kukagua hali ya uzalishaji wa kiwanda hicho ikiwa ni mkakati wa wizara ya Kilimo kuhamasisha viwanda vya ndani kuzalisha mbolea bora na yenye gharama nafuu kwa mkulima.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea (TFRA) Dkt. Stephano Ngailo (aliyesimama) akitoa maelezo kuhusu viwanda vya mbolea za maji leo katika kiwanda cha Keen Feeders Arusha.Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw.Gerald Kusaya  alitembelea kiwanda hicho (katikati) na kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda cha Keen Feeders Bw.Alfred Massawe.Kiwanda hicho huzalisha lita  600,000 za mbolea maji (boosters) kwa mwaka.

 

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"