Posts

CHADEMA YAZINDUA KAMPENI ZAKE MBAGALA ZAKHEM, DAR ES SALAAM

Image
CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimezindua rasmi kampeni zake kwenye uwanja wa Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam Agosti 28, 2020. Katika uzinduzi huo Mgombea kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia chama hicho, Tundu Lissu pamoja na mgombea mwenza wake, Salum Mwalimu walihutubia katika wafuasi wa chama hicho na wananchi waliokusanyika katika viwanja hivyo. Kampeni hizo zitaendelea hadi Oktoba 27, 2020 na uchaguzi utafanyika Oktoba 28, 2020 ili kumchagua Rais wa Jamhuri, ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani. Mgomeba kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA, Tundu Lissu, akihutubia mkutano w akampeni wa chama hicho kwenye uzoinduai wake uliofanyika viwanja vya Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam Agosti 28, 2020.    

OPE YAKABIDHI BAISKELI KWA WAWEZESHAJI NGAZI YA JAMII VITA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO KISHAPU

Image
  Afisa wa Miradi wa Shirika la OPE, Joseph Kasya akimkabidhi baiskeli  Mwezeshaji wa jamii kijiji cha Mwanima kata ya Busangwa Maneno Mahenge (kulia). Afisa wa Miradi wa Shirika la OPE, Joseph Kasya akimkabidhi baiskeli  Mwezeshaji wa Jamii kata ya Busangwa, Mary Solo  (kulia). Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog Shirika la Organization of People Empowerment (OPE) limekabidhi baiskeli tano kwa wawezeshaji ngazi ya jamii kata ya Busangwa wilayani Kishapu mkoani Shinyanga ili kusaidia kuifikia jamii kutoa elimu ya masuala ya ulinzi wa mtoto,mimba na ndoa za utotoni na ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Akizungumza leo Ijumaa Agosti 28,2020 Afisa wa Miradi wa Shirika la OPE, Joseph Kasya amesema shirika hilo wawezeshaji ngazi ya jamii watatumia baiskeli hizo kuifikia jamii katika kutoa elimu ya masuala ya ulinzi wa mtoto,uwezeshaji wananchi kiuchumi na kutokomeza mimba na ndoa za utotoni. “Shirika la OPE tunatekeleza mradi wa Kutokomeza mimba na ndoa za utotoni

JKCI YAFANYA UPASUAJI WA AXILLOBIFEMORAL BYPASS GRAFT SURGERY KWA MARA YA KWANZA

Image
NA MWANDISHI   MAALUM – DAR ES SALAAM MADAKTARI bingwa wa upasuaji wa moyo, mishipa ya damu na kifua wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa mara ya kwanza wamefanya upasuaji wa kupandikiza mishipa ya damu kutoka kwenye mshipa wa damu wa kifuani na kupeleka kwenye mishipa ya damu ya miguuni (Axillobifemoral Bypass Graft  Surgery). Upasuaji huo ni wa kwanza kufanyika hapa nchini ambapo mgonjwa alikuwa na tatizo la kupata maumivu makali maeneo ya miguuni, mapaja na sehemu ya kukalia kwa muda wa miezi nane baada ya uchunguzi ikagundulika mshipa wake mkubwa wa damu (Abdominal  Aorta)  umeziba kabisa na hivyo kushindwa kupeleka damu kwenye miguu  (Aortoilliac Occlusion Disease) damu ilikuwa inapelekwa  kupitia mishipa midogo (Collaterals). Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana jijini Dar es Salaam daktari bingwa wa upasuaji wa moyo, mishipa ya damu na kifua wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Alex Joseph alisema walimpokea mgonjwa huyo wiki iliyopita kutoka Hospitali

TANZANIA YAPOKEA SH. BILIONI 34 KUTOKA KUWAIT KUTEKELEZA MRADI WA UMWAGILIAJI LUICHE KIGOMA

Image
NA PETER HAULE NA JOSEPHINE MAJURA, WFM, DODOMA SERIKALI ya Tanzania imepokea mkopo wa masharti nafuu wa Dinar milioni 4.5 sawa na Shilingi bilioni 33.9 kutoka Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait (KFED), kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Umwagiliaji katika Bonde la Mto Luiche mkoani Kigoma. Hayo yameelezwa jijini Dodoma na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya fedha na Mipango, Bw. Benny Mwaipaja. Bw. Mwaipaja alisema kuwa Mkataba huo umesainiwa nchini Kuwait kati ya Balozi wa Tanzania nchini humo, Bi. Aisha Amour, kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Mkurugenzi Mkuu wa KFED, Abdulwahad Ahmed Al- Bader, kwa niaba ya Serikali ya Kuwait. “Fedha hizo za mkopo zitatumika katika uhakiki wa usanifu wa kina wa mradi na usimamizi wa ujenzi wa bwawa la maji la mita 375 lenye uwezo wa kuhifadhi lita za ujazo milioni 70 za maji”, alisema Bw. Mwaipaja. Alisema kuwa fedha hizo pia zitatumika katika ujenzi wa miundombinu kama mifereji ya maji, kinga za mafuriko, daraja na baraba

NAIBU KATIBU MKUU TAMISEMI AKUNWA NA MAFUNZO KAZINI YA OFISI YA WAZIRI MKUU

Image
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko akisisitiza kuwa Ofisi hiyo itaendelea kutoa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa kwa ufanisi na weledi. Mafunzo hayo ya siku tano, yameendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA) na kufungwa leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti, 2020. Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Uwekezaji), Dorothy Mwaluko, akimshukuru Afisa Lishe kutoka Shirika la Chakula Duniani, Neema Shosho, kwa ufadhali wa mafunzo ya kujenga uwezo kwa maafisa wa ofisi hiyo, lengo ikiwa ni kutekeleza majukumu waliyokasimiwa. Mafunzo hayo ya siku tano, yameendeshwa na Wakala ya Mafunzo kwa njia ya mtandao (TaGLA) na kufungwa leo jijini Dodoma tarehe 28 Agosti, 2020. Naibu Katibu  Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu, Gerald Mweli akisisitiza umuhimu wa ubora wa Uratibu wa shughuli za serikali wakati akifunga rasmi  mafunzo ya kujenga uwez

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMAMOSI AGOSTI 29, 2020

Image
 

CCM KUZINDUA KAMPENI ZAKE LEO JIJINI DODOMA

Image
  Majukwa yakiendelea kupambwa kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma tayari kesho Agosti 29,2020 kwa mkutano wa  uzinduzi wa  kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli pamoja na Mgombea Mwenza,  Samia Suluhu Hassan. Uchaguzi Mkuu utafanyika Oktoba 28 mwaka huu. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA. Picha za Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk. John Magufuli zikiwa zimepambwa kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma ambapo uzinduzi wa kampeni za Uchaguzi Mkuu utafanyika kesho Jumamosi. Kijana muuza korosho Jamali Mohamed, akiangalia picha ya Mgombea Urais wa Tganzania kupitia CCM, Dk. Magufuli iliyopambwa kwenye Uwanja wa Jamhuri. Mambo yalivyo Uwanja wa Jamhuri Dodoma. Bendera za Chama Cha Mapinduzi zikiwa zimelipamba Jiji la Dodoma.  

VIDONDA VYA TUMBO VYAMFANYA WAZIRI MKUU JAPAN KUJIUZULU

Image
  NA K-VIS BLOG/MASHIRIKA YA HABARI WAZIRI Mkuu wa Japan Shinzo Abe amejiuzulu wadhifa huo leo Ijumaa Agosti 28,2020. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa, Bw. Abe mwenye umri wa miaka 65, amesema kujiuzulu kwake kunatokana na sababu za kiafya. Aidha imeelezwa kuwa Shinzo Abe ambaye ndiye Waziri Mkuu wa Japan aliyekaa kwenye nafasi hiyo kwa muda mrefu zaidi katika historia ya nchi hiyo amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya vidonda vya tumbo(ulcerative colitis) kwa muda mrefu. “Nisingependa maradhi Yangu yawe mjadala wa maamuzi kwa Wajapani,na ninaomba radhi kwa kushindwa kumaliza muhula wangu wa uongozi.”. alinukuliwa na vyombo vya habari akieleza katika taarifa take ya kujiuzulu

YANGA YAPATA KOCHA MPYA ZLATKO KRMPOTIC KUTOKA SERBIA

Image
  Klabu ya Yanga, imemtangaza Zlatko Krmpotic kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo, Mkurugenzi wa Uwekezaji GSM, Injinia Hersi Said amesema hayo leo Asubuhi katika kipindi pendwa cha michezo cha Sports Arena leo asubuhi Agosti 28, 2020. Kocha huyo raia wa Serbia anatarajiwa  kuwasili nchini kesho Jumamosi, amesisitiza Injinia Hersi.

JAMBO YATOA MSAADA WA VIFAA VYA MICHEZO KWA WANARIADHA MASHINDANO YA RIADHA KITAIFA 2020

Image
  Afisa Mauzo wa  Kampuni ya  Jambo Food Products Ltd, Alodia Ladislaus akimkabidhi jezi  Kaimu Afisa Michezo mkoa wa Shinyanga Talita Lupembe (wa pili kulia) kwa ajili ya  wanamichezo mkoa wa Shinyanga watakaoshiriki Mashindano ya Riadha Kitaifa yanayotarajiwa kufanyika Mwezi Septemba 2020 jijini Dar es salaam Na Kadama Malunde- Malunde 1 blog Kampuni ya Uzalishaji na Usambazaji Vinywaji Baridi Jambo Food Products Ltd imetoa msaada wa vifaa vya michezo na fedha kwa wanamichezo mkoa wa Shinyanga watakaoshiriki Mashindano ya Riadha Kitaifa yanayotarajiwa kufanyika Mwezi Septemba 2020 katika Uwanja wa Benjamini Mkapa Jijini Dar es salaam. Akizungumza leo Alhamis Agosti 27,2020 Mwakilishi wa Wakurugenzi Kampuni ya Jambo Food Products Ltd, Halima Omary amesema Kampuni yao imetoa msaada wa vifaa vya michezo ili kuwapa ari na moyo wanariadha watatu kutoka mkoa wa Shinyanga  watakaoshiriki Mashindano ya Riadha Kitaifa mwaka 2020 . “Jambo Food Products Ltd ni wadau wakub

KAMISHNA CP LIBERATUS SABAS LEO AMEFAYA ZIARA YA KUKAGUA MPAKA WA TANZANZAIA NA ZAMBIA KATIKA MKOA WA SONGWE.

Image
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi CP Liberatus Sabas wa tatu kutoka kushoto akifuatiwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe RPC George Kiando pamoja na maafisa wengine wa Jeshi la Polisi Mkoa   wa Songwe wakiwa Wilaya ya Momba wakikagua mpaka wa Tunduma (Tanzania) na Zimbia.  Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi CP Liberatus Sabas (katikati) Afisa kutoka TRA katika picha ya pamoja na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalamamkoa wa Songwe wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kikao kazi .(PICHA NA JESHI LA POLISI) Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi CP Liberatus Sabas, katikati akionyeshwa jiwe la Mpaka wa Tanzania na Zambia na   Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe RPC George kiando wakati akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani huo leo 27/08/2020.

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA AGOSTI 28, 2020

Image