Posts

DC SAME AHIMIZA UBUNIFU KATIKA UKUSANYAJI MAPATO WILAYANI HUMO

Image
 NA ASHRACK MIRAJI, SAME Mkuu wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro, Mhe. Kasilda Mgeni, ameagiza Maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wilayani humo kutumia ubunifu, weledi pamoja na busara katika kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi kwa baadhi ya wafanyabiashara wasio waadilifu. Mkuu huyo wa Wilaya amebainisha hayo katika kikao cha Kamati ya Ushauri wa Kodi cha Wilaya na kusisitiza kuwa mfanyabiashara yeyote atakaye bainika kuendelea kukiuka kulipa kodi taarifa iwasilishwe Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake. Amesema suala la ulipaji kodi ni wajibu wa kila mwananchi kisheria ili kusaidia Serikali kupanga shughuli za kuwaletea wananchi wake maendeleo. “TRA fanyeni operesheni za mara kwa mara kwa wafanyabiashara wote ambao wapo ndani ya Wilaya ya Same na wanaostahili kutumia mashine za Kielektroniki (EFD) basi wanakuwa nazo na kwa wale ambao watakuwa wakaidi baada ya kuwafuatilia na kuwapa elimu basi sheria iweze kuchukua mkondo wake juu yao kwa

KUTOKA MAGAZETINI LEO MACHI 29, 2024

Image
 

WAZIRI DKT. NCHEMBA AONGOZA MKUTANO WA WB KANDA YA AFRIKA

Image
Na. Peter Haule, WF, Dodoma Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameongoza mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati uliolenga kujadili namna mashirika ya fedha ya kimataifa yanavyoweza kuongeza fedha kwa ajili ya kuzisaidia nchi za kipato cha kati ili ziweze kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika nchi zao itakayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya jamii. Akifungua mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Mkutano huo, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alisema kuwa Dunia inakabiliwa na migogoro mingi na changamoto za maendeleo ya kiuchumi ambazo zinasababisha kutofikiwa kikamilifu kwa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs). Alisema kuwa kupungua kwa nafasi ya kifedha katika kushughulikia migogoro hiyo kunadhoofisha uwezo wa Serikali za nchi hizo kufadhili programu za kijamii, kuharakisha ufufuaji wa Uchumi na pia kuongeza madeni katika nchi hizo. “Mizozo inayoe

‘TUKIIMARISHA UBORA WA HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO TUTAPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI’-UMMY MWALIMU

Image
Na WAF - Dar Es Salaam Serikali kupitia Wizara ya Afya inaendelea kuimarisha ubora wa huduma za Afya ya mama na mtoto katika vituo 25 vinavyotoa huduma ya upasuaji wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni (CEmONC) katika Mkoa wa Dar Es Salaam ili kupunguza vifo vitokanavyo na Uzazi. Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema hayo leo Machi 28, 2024 wakati akifungua mafunzo elekezi kazini juu ya huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto katika Mkoa wa Dar Es Salaam ambapo mafunzo hayo ni endelevu yanayotolewa nchini nzima ili kupunguza vifo vya mama mjamzito na mtoto. “kuimarisha ubora wa huduma za Afya ya mama na mtoto katika vituo 25 vya Afya vinavyotoa huduma ya upasuaji wa dharura wa kumtoa mtoto tumboni yaani (CEmONC) tutakua tumetatua asialimia 84 ya changamoto za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto kwa Mkoa wa Dar Es Salaam.” Amesema Waziri Ummy Amesema, mafunzo haya ni muhimu sana ambayo yamesaidia kupunguza vifo katika katika Mkoa wa Tabora ambapo kwa mwaka 2023 vifo vya watoto wachanga vimepung

RAIS SAMIA APOKEA RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI (CAG) KWA MWAKA 2022/23 PAMOJA NA TAARIFA YA UTENDAJI KAZI YA TAKUKURU

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Taarifa ya Utendaji Kazi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa mwaka 2022/2023 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo CP. Salum Hamduni Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 28 Machi, 2024.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokea Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2022/23 kutoka kwa Bw. Charles Kichere Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 28 Machi, 2024.

WAJUMBE WA KAMATI YA PIC WATEMBELEA KITUO KIKUU CHA MABASI MSAMVU

Image
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Umma (PIC), wakitembelea Kituo Kikuu cha Mabasi Msamvu mkoani Morogoro Machi 27, 2024. Kituo hicho ni mradi unaoendeshwa kwa ubia Kati ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) unaomiliki asilimia 74% na Halmashauri ya Manispaaya Morogoro asilimia 26% Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Umma (PIC), wakitembelea Kituo Kikuu cha Mabasi Msamvu mkoani Morogoro Machi 27, 2024. Kituo hicho ni mradi unaoendeshwa kwa ubia Kati ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Halmashauri ya Manispaaya Morogoro Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji Mitaji ya Umma (PIC), Mhe.Augustine Vuma, akizungumza baada ya ziara ya kamati kutembelea na kukagua Kituo Kikuu cha Mabasi Msamvu mkoani Morogoro Machi 27, 2024. Kituo hicho ni mradi unaoendeshwa kwa ubia Kati ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) na Halmashauri ya Manispaaya Morogoro Mwenyekiti