WAZIRI DKT. NCHEMBA AONGOZA MKUTANO WA WB KANDA YA AFRIKA
Na.
Peter Haule, WF, Dodoma
Waziri
wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), ameongoza mkutano wa Benki ya
Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato
cha Kati uliolenga kujadili namna mashirika ya fedha ya kimataifa yanavyoweza
kuongeza fedha kwa ajili ya kuzisaidia nchi za kipato cha kati ili ziweze
kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika nchi zao itakayochochea ukuaji
wa uchumi na maendeleo ya jamii.
Akifungua
mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao jijini Dodoma, Mwenyekiti wa
Mkutano huo, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba alisema kuwa Dunia inakabiliwa na
migogoro mingi na changamoto za maendeleo ya kiuchumi ambazo zinasababisha
kutofikiwa kikamilifu kwa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
Alisema
kuwa kupungua kwa nafasi ya kifedha katika kushughulikia migogoro hiyo
kunadhoofisha uwezo wa Serikali za nchi hizo kufadhili programu za kijamii,
kuharakisha ufufuaji wa Uchumi na pia kuongeza madeni katika nchi hizo.
“Mizozo
inayoendelea nchini Urusi na Ukraine, Mashariki ya Kati na baadhi ya nchi
nyingine za Afrika imechochea kupanda kwa bei ya vyakula na kuwasukuma
mamilioni ya watu kwenye uhaba wa chakula”, alisema Dkt. Nchemba.
Aidha
Dkt. Nchemba aliishukuru Benki ya Dunia kwa mchango wake wa kuzijengea uwezo
taasisi katika kuyafikia maendeleo endelevu lakini pia kufufua uchumi kutokana
na changamoto mbalimbali zinazotokea Duniani.
Vilevile
alisema kuwa kukabiliana na changamoto zinazoikumba dunia sio kazi rahisi kwa
nchi moja, hivyo ameomba kuwa na nguvu ya pamoja katika Kanda na Bara la Afrika
katika kutafuta utatuzi wa changamoto hizo.
Dkt.
Nchemba ameishukuru Benki ya Dunia kwa kummwamini kuongoza kikao hicho kikubwa
lakini pia amewashukuru viongozi mbalimbali waliotoa mada ambazo zimewafunbua
macho kwa kuona fursa zilizopo katika kukuza una kuwezesha biashara na pia kuwa
na majadiliano mazuri wakati wa mikutano ijayo ya majira ya kipupwe ya Benki ya
Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) itakayofanyika mwezi Aprili, 2024
jijini Washington D.C nchini Marekani.
Kwa
upande wake Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Mashariki na
Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria Kwaka, alisema kuwa katika kipindi cha miaka
mitano ilitoa misaada na mikopo nafuu yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni
tatu kwa nchi za Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika.
Alisema
kuwa mwaka wa fedha uliopita Benki ya Dunia kupitia Mfuko wa IDA ilitoa dola
bilioni 2.4 na kwamba kiwango cha misaada na mikopo hiyo imeendelea kuongezeka
na miongoni mwa nchi zilizonufaika na mpango huo ni Tanzania, Kenya na
Eswatini.
Aidha,
Bi. Kwakwa amevitaja vipaumbele vya Benki hiyo kuwa ni pamoja na kuhakikisha
nchi zitapata umeme wa uhakika, kuwa na maendeleo ya kidigitali, upatikanaji wa
ajira, mapinduzi ya kiuchumi, kujenga uwezo kwa rasilimali watu na masuala ya
elimu.
Baadhi
ya Viongozi walioshiriki mkutano huo ni pamoja na Makamu wa Rais wa Benki ya
Dunia anayesimamia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria
Kwakwa, Makamu wa Rais wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IFC) Kanda ya Afrika, Bw.
Sergio Pimenta, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia, Bi. Anshula Kant,
Mawaziri wa fedha na Mipango (Magavana) na wajumbe wengine.
Waziri
wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiongoza mkutano wa Benki ya
Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato
cha Kati lililolenga kujadili namna mashirika ya fedha ya kimataifa yanavyoweza
kuongeza fedha kuzisaidia nchi za kipato cha kati kufikia maendeleo endelevu ya
kiuchumi na kijamii. Mkutao huo umefanyika kwa njia ya Mtandao, kutokea Jengo
la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Makamu
wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Victoria
Kwaka, akitoa mada wakati wa mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la
Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati, ambapo Waziri wa
Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) aliongoza mkutano huo uliofanyika
kwa njia ya mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Waziri
wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akitoa wito kwa taasisi za
fedha za kimataifa kuongeza fedha kwaajili ya kuzisaidia nchi za kipato cha
kati wakati akifungua mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya
Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati lililolenga kujadili namna mashirika
hayo ya fedha yanavyoweza kuongeza fedha kwa nchi hizo. Mkutano huo umefanyika
kwa njia ya Mtandao kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Waziri
wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo,
Bi Amina Khamis Shaaban, wakifuatilia mambo mbalimbali wakati wa mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu
la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati, ambapo Mhe.
Nchemba aliongoza mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao, kutokea Jengo la
Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizaraya Fedha, Bi Amina Khamis Shaaban na Afisa Mwandamizi wa
Idara ya Fedha za Nje wa Wizara hiyo, Bw. John Kuchaka, wakifuatilia
uwasilishwaji wa taarifa wakati wa mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu
la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati, ambapo Waziri
wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) alikuwa Mwenyekiti wa mkutano
huo uliofanyika kwa njia ya mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square),
jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizaraya Fedha, Bi Amina Khamis Shaaban, akifafanua jambo wakati wa mkutano wa Benki ya Dunia wa Jukwaa la Tatu la Kanda ya Afrika Kundi la Kwanza kwa nchi za Kipato cha Kati, ambapo Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) aliongoza mkutano huo uliofanyika kwa njia ya mtandao, kutokea Jengo la Hazina (Treasury Square), jijini Dodoma.
Comments
Post a Comment