Posts

WIZARA YA ARDHI YAJA NA VIPAUMBELE VYA KUONDOA CHANGAMOTO ZA ARDHI

Image
  Na Munir Shemweta, WANMM Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amesema wizara yaje imeweka vipaumbele 12 katika mwaka ujao wa fedha 2023/2024 unaoanza Julai mosi mwaka huu lengo kubwa likiwa kuondoa changamoto za sekta ya ardhi na kutilia mkazo ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya pango la ardhi. Kwa mujibu wa Dkt Mabula katika kipindi cha mwaka huo wa fedha wa 2023/2024, Wizara ya Ardhi imejipanga kuhakikisha mikakati yake inaenda vizuri hususan kuondoa kero na malalamiko ya wananchi kwani dhamira ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha nchi inakuwa kiuchumi na watu wake wanafaidika na mali waliyokuwa nayo ambayo ni ardhi. Dkt Mabula alisema hayo jana tarehe 28 Juni 2023 ikiwa ni muda mfupi baada ya kikao cha uongozi wa wizara kwa ajili ya kuweka mikakati ya kutekeleza vipaumbele vya Wizara ya Ardhi baada ya kumalizika kwa Bunge la Bajeti 2023/2024 ambapo kwa mujibu wa Waziri wa Ardhi kabla ya viongozi kuanza kusambaa maeneo mbalimbali

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA JUNI 30, 2023

Image
 

BOT YATOA KALENDA YA MINADA YA DHAMANA ZA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA WA 2023/24

Image
 

RC KUNENGE APOKEA NG'OMBE 500 ,MBUZI 1,000 KWA AJILI YA SIKUKUU YA EID AL ADHA

Image
  Na Mwamvua Mwinyi, Pwani Mkuu wa mkoa wa Pwani , alhaj Abubakari Kunenge, amepokea  Ng'ombe 500 na mbuzi 1,000 kutoka Jumuiya ya IDDEF ya nchini Uturuki wakishirikiana na Rahma Fondation ya Tanzania kwa ajili ya sadaka ya sikukuu ya Eid Al Adha . Akikabidhi Sadaka hiyo ,Sheh Bahadhir kutoka katika taasisi hiyo, katika machinjio ya Pangani, mjini Kibaha, alisema IDDEF , taasisi ya Rahmah ya nchini Tanzania wametoa ng'ombe na mbuzi hao kwa ajili ya  Sadaka hiyo hususan kwa wajane,yatima na wazee. Aidha aliishukuru serikali ya Tanzania kwa kukubali msaada huo na kutoa machinjio hiyo kwa ajili ya kuchinjia wanyama hao. Akipokea msaada huo, Mkuu wa Mkoa Kunenge, aliishukuru taasisi hizo kwa sadaka hiyo ya ibada ya kuchinjwa ya Eid Al  adha na kwamba sadaka hiyo itagawanywa kwa wahitaji ikiwemo, yatima,wajane na wazee. "Nimepokea Ng'ombe 500 na mbuzi 1,000 Kwa ajili ya sadaka ya ibada ya kuchinjwa ya EId Al Adha  naipongeza Jumuiya hii Rahma Foundation na IDDER na mashekh

MAKAMU WA KWANZA WA RAIS ZANZIBAR AONGOZA WAUKINI WA KIISLAMU KATIKA SALA YA EID AL ADHA HUKO UNGUJA

Image
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Alhaj Othman Masoud Othman, leo Alhamis Juni 29, 2023 amewaongoza Waumini mbali mbali wa Dini ya Kiislamu katika Ibada ya Sala ya Idd al Adh-ha hapo Masjid Mushawwar,  Mskiti uliopo Muembeshauri Mkoa wa Mjini-Magharibi Unguja.  Viongozi mbali mbali  wamehudhuria katika Sala hiyo akiwemo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla; Rais Mstaafu wa Awamu ya Sita (6) wa Zanzibar Dkt Amani Abeid Karume na Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kaabhi  Sikukuu ya Idd al Adh-ha inakuja baada ya kukamilika kwa Ibada ya Hijja, Nguzo ya 5 ya Dini ya Kiislamu, inayofanyika huko Makka Saudi Arabia. 

WAZIRI MKUU MAJALIWA AMUWAKILISHA RAIS SAMIA KWENYE SALA YA EID AL- ADHA

Image
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Leo 29, June 2023, amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Swala ya Eid El Adh'haa ambayo imefanyika kitaifa Jijini Dar es Salaam katika Msikiti Mkuu wa Mfalme Mohamed wa Sita, ulioko Kinondoni. NA HUKO ZANZIBAR,  Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla amejumuika na Waumini wa Dini ya kiislamu, viongozi mbali mbali wa Serikali na vyama vya Siasa Wakiongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Alhajj Othman Masoud Othman katika Ibada ya Sala ya Eid Adh' ha iliyosaliwa Masjid Mushawwar Muembe Shauri Jijini Zanzibar.  

TAASISI UHISANI ZIMEOMBWA KUONGEZA NGUVU UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA JAMII

Image
Mwandishi Wetu, Zanzibar  TAASISI zinazojishughulisha na masuala ya uhisani Afrika Mashariki, zimetakiwa kuongeza nguvu katika kutatua changamoto zinazoikabili jamii ili kuimarisha ustawi wa wananchi.Anaripoti. Wito huo umetolewa leo Jumatano, visiwani Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais, Othman Masoud Othman, akifungua mkutano wa nane wa Uhisani Afrika Mashariki (EAPC), ulioandaliwa na Mtandao wa Uhisani Afrika Mashariki (EAPN), kwa kushirikiana na Kituo cha Huduma za Kisheria (LSF). Othman amehimiza taasisi hizo kuimarisha umoja na nguvu katika kukabiliana na changamoto zinazohitaji juhudi za pamoja kuzitatua, ikiwemo mabadiliko ya hali ya hewa, umasikini, ukosefu wa usawa na athari zilizotokana na janga la Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19). “Mabadiuliko ya mifumo yenye athari yanahitaji mbinu ya kina na jumuishi ambao inavuka mipaka ya jiografia, itikadi na sekta. Ni kupitia ushirikiano thabiti wa ndani, kikanda na kimataifa ndipo tunaweza kutumia nguvu kubwa ya hatua za pamo