Posts

TANZANIA YAWA KITOVU CHA UWEKEZAJI NA UKUAJI UCHUMI NCHI KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA

Image
  * Mfumuko wa bei wadhibitiwa, Neema yaja kwa wafanyabiashara wadogo MATOKEO Mazuri yaliyotokana na jitihada za Serikali kwa kuweka mazingira bora ya uwekezaji na ufanyaji biashara zimeiweka Tanzania kuwa kitovu cha uwekezaji na kupelekea ukuaji wa uchumi katika nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka asilimia 4.7 mwaka 2022 hadi kufikia asilimia 5.0 mwaka 2023 huku matarajio ya ukuaji uchumi kwa mwaka 2024 yakiwa asilimia 5.5. Hayo yameeelezwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Mpango alipomwakilishwa Rais Samia Suluhu Hassan katika Jukwaa la Uwekezaji na Kodi 2024 lililofanyika Leo katika kituo cha mikutano cha kimataifa ya Julius Nyerere jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa Serikali imeendelea kufanya maboresho ya sera na kanuni ili kujibu changamoto za uwekezaji na wafanyabiashara ili waweze kulipa kodi kwa hiari na kuiwezesha Serikali kutekeleza mahitaji kwa Umma. Mpango amesema kuwa, Jitihada hizo za Serikali ambayo imekuwa ikishirikiana na sekta

CRDB, KLABU YA WAANDISHI HABARI Z'BAR "WAYAJENGA"

Image
  MENEJA wa Biashara benki ya CRDB Zanzibar, Abdalla Duchi, akifafanua jambo wakati wa mazungumzo baina ya viongozi wa benki hiyo na wa Klabu ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) yaliyofanyika katika ofisi za benki hiyo zilizomo katika jengo la Michezani Mall, Zanzibar MENEJA wa Biashara benki ya CRDB Zanzibar, Abdalla Duchi (kushoto) akizungumza na viongozi wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), walipofanya ziara ya kukuza mahusiano katika ofisi za benki hiyo zilizomo katika jengo la Michezani Mall, Zanzibar. MWENYEKITI wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), Abdallah Mfaume (kulia) na Mratibu wa klabu hiyo, Mgeni Hamad wakimsikiliza Meneja Biashara wa benki ya CRDB Zanzibar wakati wa mazungumzo baina ya vingozi wa ZPC na CRDB yaliyofanyika katika ofisi za benki hiyo zilizomo katika jengo la Michezani Mall, Zanzibar. MJUMBE wa Kamati Tendaji wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), zuhura msabah akizungumza jambo wakati viongozi wa klabu hiyo walipofanya mazung

JUHUDI ZA Dkt. SAMIA KUKUZA UTALII ZAONGEZA IDADI YA WAGENI NGORONGORO

Image
  Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongo (NCAA), Richard Kiiza, akitoa mada katika kikao kazi na Wahariri wa Habari kilichofanyika leo Februari 26,2024 Jijini Dar es Salaam, chini ya Uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina. Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano Ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Thobias Makoba, akizungumza alipokuwa akitoa salamu za utangulizi katika kikao hicho kilichoratibiwa na Ofisi hiyo Jijini Dar es Salaam. (PICHA NA: HUGHES DUGILO) Na: Hughes Dugilo, DAR ES SALAAM  Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongo (NCAA), Richard Kiiza, amesema kuwa juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kufufua sekta ya utalii mara baada ya UVIKO 19 kupitia filamu ya 'Tanzania the Royal Tour' zimechangia ongezeko kubwa la idadi ya wageni wanaotembelea Hifadhi hiyo, hadi kufikia wageni 752,232 kwa Mwaka wa fedha 2022/2023. Amsema kuwa ongezeko hilo la idadi ya wageni limekuwa na matokeo chanya, na kwamba mapato yatokanayo na utalii yame

KUTOKA MAGAZETINI LEO FEBRUARI 27, 2024

Image
 

DKT. MOLLEL AWAJULIA HALI MAJERUHI WA AJALI MKOANI ARUSHA

Image
  Naibu Waziri wa Afya Dkt Godwin Mollel leo Februari, 25, 2024 amewajulia hali majeruhi wa ajali iliyohusisha magari manne eneo la Ngaramtoni, Mkoani Arusha waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mount Meru. Dkt. Mollel amesema majeruhi wote wanaendelea vizuri na mmoja ndo kapewa Rufaa ya kwenda hospitali ya Rufaa ya Kanda KCMC Mjini Moshi Mkoa wa Kilimanjaro. "Rais Samia Suluhu Hassan ametuelekeza majeruhi wote wa ajali hii kupatiwa matibabu bila kulipa gharama zozote", Dkt. Mollel ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Arusha na watanzania kwa ujumla kuwa watulivu wakati wakiendelea kuwatibia majeruhi na kwa wale waliopoteza ndugu zao utaratibu wakupatiwa miili unaandaliwa na wataalamu. Aidha Dkt. Mollel kwa niaba ya Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu amewashukuru na kuwatia moyo watumishi wa afya katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mount Meru kwa kazi nzuri waliofanya katika kuwahudumia majeruhi wa ajali hiyo Kwa upande wake mmoja wa majeruhi Raia wa Togo, Apelo Apeto (3