CRDB, KLABU YA WAANDISHI HABARI Z'BAR "WAYAJENGA"
MENEJA
wa Biashara benki ya CRDB Zanzibar, Abdalla Duchi, akifafanua jambo wakati wa mazungumzo
baina ya viongozi wa benki hiyo na wa Klabu ya Wandishi wa Habari Zanzibar
(ZPC) yaliyofanyika katika ofisi za benki hiyo zilizomo katika jengo la
Michezani Mall, Zanzibar
MENEJA wa Biashara benki ya CRDB
Zanzibar, Abdalla Duchi (kushoto) akizungumza na viongozi wa Klabu ya Waandishi
wa Habari Zanzibar (ZPC), walipofanya ziara ya kukuza mahusiano katika ofisi za
benki hiyo zilizomo katika jengo la Michezani Mall, Zanzibar.
MWENYEKITI wa Klabu ya Waandishi wa
Habari Zanzibar (ZPC), Abdallah Mfaume (kulia) na Mratibu wa klabu hiyo, Mgeni
Hamad wakimsikiliza Meneja Biashara wa benki ya CRDB Zanzibar wakati wa
mazungumzo baina ya vingozi wa ZPC na CRDB yaliyofanyika katika ofisi za benki
hiyo zilizomo katika jengo la Michezani Mall, Zanzibar.
MJUMBE wa Kamati Tendaji wa Klabu ya
Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), zuhura msabah akizungumza jambo wakati
viongozi wa klabu hiyo walipofanya mazungumzo ya kukuza mahusiano na uongozi wa
benki ya CRDB katika ofisi za benki hiyo zilizomo katika jengo la Michezani
Mall, Zanzibar. Kushoti ni katibu mkuu wa ZPC, Mwinyimvua Nzukwi.
AFISA Biashara na Mauzo, Lucy Mbuya na
Afisa Ubora wa huduma wa benki ya CRDB, Zainab Ally, wakiwa katika kikao cha
mazungumzo baina ya vingozi wa ZPC na CRDB kilichofanyika katika ofisi za benki
hiyo zilizomo katika jengo la Michezani Mall, Zanzibar.
VIONGOZI wa benki ya CRDB na klabu ya
waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya
mazungumzo baina yao yaliyofanyika katika ofisi za benki hiyo zilizomo katika
jengo la Michezani Mall, Zanzibar
Comments
Post a Comment