JUHUDI ZA Dkt. SAMIA KUKUZA UTALII ZAONGEZA IDADI YA WAGENI NGORONGORO
Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongo (NCAA), Richard Kiiza, akitoa mada katika kikao kazi na Wahariri wa Habari kilichofanyika leo Februari 26,2024 Jijini Dar es Salaam, chini ya Uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano Ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Thobias Makoba, akizungumza alipokuwa akitoa salamu za utangulizi katika kikao hicho kilichoratibiwa na Ofisi hiyo Jijini Dar es Salaam.
(PICHA NA: HUGHES DUGILO)
Na: Hughes Dugilo, DAR ES SALAAM
Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongo (NCAA), Richard Kiiza, amesema kuwa juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kufufua sekta ya utalii mara baada ya UVIKO 19 kupitia filamu ya 'Tanzania the Royal Tour' zimechangia ongezeko kubwa la idadi ya wageni wanaotembelea Hifadhi hiyo, hadi kufikia wageni 752,232 kwa Mwaka wa fedha 2022/2023.
Amsema kuwa ongezeko hilo la idadi ya wageni limekuwa na matokeo chanya, na kwamba mapato yatokanayo na utalii yameongezeka kutoka shilingi bilioni 31 mwaka 2020/2021 hadi kufikia shilingi bilioni 171 mwaka 2022/2023.
Kamishna Kiiza amebainisha hayo alipokuwa akitoa mada kuhusu mafanikio yaliyopatikana katika miaka mitatu ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kikao kazi na Wahariri wa Habari kilichofanyika leo Februari 26,2024 Jijini Dar es Salaam, chini ya Uratibu wa Ofisi ya Msajili wa Hazina.
(Picha za baadhi ya Wahariri na wadau, katika mkutano huo.)
Comments
Post a Comment