Posts

WCF YATWAA TUZO SIKU YA KIMATAIFA YA USALAMA NA AFYA MAHALI PA KAZI

Image
  NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, MOROGORO MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) umetwaa tuzo ya Mfuko Bora miongoni mwa Taasisi za Bima na Fidia wakati wa kilele cha Siku ya Kimataifa ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi kwenye viwanja vya Tumbaku mjini Morogoro ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Profesa Joyce Ndalichako. Kilele cha Maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Usalama na Afya mahali pa kazi hufanyika Aprili 28 kila mwaka ambapo Tanzania huungana na mataifa mengine duniani kuiadhimisha siku hii, lengo kubwa ni kuendeleza kampeni za kuhamasisha uwepo wa mazingira salama na yenye kulinda afya za watu katika sehemu za kazi ambapo kauli mbiu ya maadhimisho kwa mwakam huu ni “Mazingira salama na afya ni kanuni na haki ya msingi mahali pa kazi.”. Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Dkt. John Mduma alipokea tuzo hiyo kutoka kwa mgeni rasmi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira, na Wenye Ulemavu), Profesa Joyc

Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan Amuandalia Mgeni Wake Rais Wa Rwanda Mhe. Paul Kagame Hafla Ya Chakula Cha Jioni Ikulu Jijini Dar Es Salaam

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wageni mbalimbali waliofika kwenye hafla ya chakula cha jioni alichomuandalia mgeni wake Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023 Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akizungumza na Wageni mbalimbali waliofika kwenye hafla ya chakula cha jioni alichoandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023 Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akiwasalimia viongozi mbalimbali waliohudhuria hafla ya chakula cha jioni alichoandaliwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Aprili, 2023 Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akisalimiana na Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwenye hafla ya chakula cha jioni alichoandaliwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Ikulu Jijini Dar es Sal

TANZANIA NA JAPAN YASAINI MIKATABA YA MIKOPO YENYE MASHARTI NAFUU

Image
  Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam Tanzania na Japan kupitia Shirika lake la Ushirikiano wa Kimataifa (JICA), zimesaini mikataba mitatu ya mkopo wenye masharti nafuu na msaada, yenye thamani ya Yen bilioni 10.15, sawa na shilingi za Tanzania, bilioni 174.9, kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa Ununuzi wa pemebejeo za kilimo pamoja na kufufua Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO).  Akizungumza baada ya kusaini mikataba hiyo kwa niaba ya Serikali, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt Natu Mwamba, alisema kuwa Yen bilioni 10 sawa na shilingi za Tanzania bilioni 172.2 ni mkopo nafuu uliotolewa na Shirika la Ushirikiano la Kimataifa (JICA) kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na kiasi cha Yen milioni 150, sawa na zaidi ya shilingi za Tanzania bilioni 2.6, ni msaada uliotolewa na nchi hiyo kupitia Ubalozi wake hapa nchini.  Dkt. Mwamba, alisema kuwa mkopo huo utatumika kuongeza tija katika kilimo kwa kununua pembejeo ikiwemo mbolea, mbegu bora kwa ajili ya wakulim

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA APRILI 28, 2023

Image