Posts
ENDELEENI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU NA KUTOA HUDUMA BORA, KM AWAASA WCF
- Get link
- Other Apps
By
K-VIS BLOG
Watumishi wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) wameaswa kuendelea kufanya kazi kwa uadilifu na kwa misingi ya uwajibikaji ili kutoa huduma bora kwa wadau wake. Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Tixon Nzunda alipotembelea ofisi za Mfuko kwa ajili ya kufuatilia shughuli zinazofanywa na WCF. “Nimefanikiwa kuzungumza na watendaji wa idara na vitengo vyote na moja ya maelekezo yangu ni kuwahimiza kutoa huduma kwa umma kwa kuzingatia misingi ya ueledi, uwajibikaji na usikivu na kuzingatia misingi na miongozo ya uendeshaji kazi serikalini”, alisema Bw. Nzunda. “Pia nawasisitiza kuhakikisha kuwa utendaji wa shughuli za umma unazingatia misingi ya kujenga ustawi wa wananchi. Tumieni rasimilimali zilizopo kwa kuzingatia thamani ya fedha na uwekezaji ufanyike katika maeneo yenye tija ili kulinda amali za fidia kwa wanachama”. Bw. Nzunda ameelekeza Mfuko kuhakikisha unaimarisha zaidi mifumo ya kielekt
DKT. NCHEMBA: SERIKALI IMESIKIA KILIO CHA WANANCHI KUHUSU TOZO ZA MIAMALA YA SIMU
- Get link
- Other Apps
By
K-VIS BLOG
Naombeni msaada wenu wandugu Na Benny Mwaipaja,Dar es Salaam WAZIRI wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amesema Serikali imesikia kilio na maoni ya wananchikuhusu tozo mpya ya miamala ya simu na kuwaomba wawe watulivu wakati jambo hilo linatafutiwa ufumbuzi. Dkt. Nchemba ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na vyombo vya habari akiambatana na Waziri wa Teknolojia ha Habari na Mawasiliano Dkt. Faustine Ndugulile. “Kwa maaneo ambayo wananchi wametoa ushauri na kuelezea namna ambavyo jambo hili linawagusa lakini pia tumepokea maeneo ambayo yanatakiwa kutoa elimu zaidi ili kujenga uelewa wa pamoja ikiwa ni pamoja na viwango vinavyokatwa kwa nayetuma na anayetoa lakini pia kuhusu mantiki ya jambo lenyewe” alisema Mhe. Mwigulu Alisema kuwa jambo la tozo za miamala linatekelezwa kupitia sheria iliyopitishwa na Bunge lakini kuna kanuni za utekelezaji zinazo mhusu yeye kama Waziri wa Fedha na Mipango na maeneo mengine yanahusu Wizara ya Teknolloj
Naibu Waziri Gekul amuibua Mbaraka Mwinshekhe mahafali ya Malya
- Get link
- Other Apps
By
K-VIS BLOG
Adeladius Makwega -Kwimba Mwanza (WHUSM) Serikali imesema kuwa Watanzania wanahitaji burudani ya muziki kwani mara baada ya kujishughulisha na shughuli za maendeleo mchana kutwa basi jioni ni muda wa kupumzisha miili na akili zao. Hayo yamesemwa Julai 17, 2021 katika mahafali ya 10 ya Chuo cha Maendeleo ya Michezo Malya ambapo Mheshimiwa Pauline Gekul Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amekuwa mgeni rasmi. “Watanzania tunapenda muziki iwe dansi, Bongo fleva, rege au muziki wa kiutamadauni, si mmeona wanachuo cha Malya walivyokuwa wakicheza muziki vizuri, huku wakinengua? huo ndiyo muziki” alisema Mheshimiwa Gekul. Yawe mashairi au ala za muziki zinaweza kumtoa nyoka pangoni alisema kwa bashasha huku akiiweka vizuri mikrofoni wakati wa mahafali hayo. Tanzania yetu ina utajiri mkubwa wa muziki mathalani nyimbo za zamani zimekuwa zikipigwa katika baadhi ya redio na kumbi za starehe. Serikali chini ya Jemedari, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan inatoa ushi
WAZIRI DKT. KALEMANI ASHUSHA UMEME TOKA 3700/- MPAKA 100/- KWA UNIT VISIWANI-MWANZA
- Get link
- Other Apps
By
K-VIS BLOG
** Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani Julai 18, 2021 amefanya Ziara katika kisiwa cha Maisome kilichopo wilaya ya Sengerema jijini Mwanza na kuagiza kampuni binafsi ya Jumeme inayosambaza Umeme katika kisiwa hicho kutoza bei elekezi ya Serikali ya Umeme Vijijini ya shilingi 100 kwa unit moja badala ya shilingi 2,000/- mpaka 3,700/- iliyokuwa ikitozwa na kampuni hiyo. Akizungumza na wanakijiji wa kijiji cha Kanoni kisiwani Maisome, Waziri Kalemani alieleza kuwa tayari Serikali imetoa bei elekezi ya umeme nchi nzima ambayo inasimamiwa na EWURA na ndio inayotumika na TANESCO katika kuuzia umeme wananchi hivyo ni vyema wawekezaji wote wakaifuata na kuizingatia. Bei ya kuwauzia umeme wananchi ni moj ambayo inatumika na TANESCO na kusimamiwa na EWURA, hivyo naagiza Kampuni ya Jumeme iwashushie wananchi wa kijiji hichi bei na ifanane na ile inayotozwa na TANESCO katika maeneno mengine na huduma ziboreshwe, umeme usikatike mara kwa mara bila sababu za msingi” Alisema Waziri Kalemani Wazi
KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMATATU JULAI 19, 2021
- Get link
- Other Apps
By
K-VIS BLOG
SIMBA YATWAA UBINGWA WA SOKA TANZANIA BARA 2020/2021
- Get link
- Other Apps
By
K-VIS BLOG
Wachezaji wa Simba na benchi la ufundi wakishangilia mara baada ya kutwaa kombe la ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2020/2021 baada ya kufikisha pointi 83 kufauatia ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Namungo kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam Julai 18, 2021. Kimainginpambano dhidi ya Namungo lilikuwa la kukamilisha ratiba.