WAZIRI MCHENGERWA AONGOZA MKUTANO WA PILI WA MAWAZIRI WA NCHI WANACHAMA WA UMOJA WA AFRI
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati Na. 8 ya Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati Na. 8 inayoshughulika na masuala ya Utumishi wa Umma na Utawala akiongoza Mkutano wa Pili wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala Afrika kwa njia ya mtandao. Na Mary Mwakapenda-Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati Na.8 ya Kamisheni ya Umoja wa Afrika na Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati Na. 8 inayoshughulika na masuala ya Utumishi wa Umma na Utawala leo ameongoza Mkutano wa Pili wa Mawaziri wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Maadili na Misingi ya Utumishi wa Umma na Utawala Afrika kwa njia ya mtandao. Mhe. Mchengerwa ameongoza Mkutano huo ili kupitia na kuidhinisha ajenda mbalimbali zilizowasilishwa na Mkut