Posts

DARAJA LA KIYEGEYA MBIONI KUKAMILIKA

Image
Meneja wa TANROADS, mkoa wa Morogoro, Mhandisi, Kolante Ntije, akimuonesha Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi, Dkt. Leonard Chamuriho (mwenye tai), mihimili mikuu itakayowekwa kwenye daraja la Kiyegeya, mkoani Morogoro, wakati Waziri huyo alipofika darajani hapo kujionea maendeleo yake. Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi, Dkt. Leonard Chamuriho (mwenye tai), akiangalia mihimili mikuu itakayowekwa kwenye daraja la Kiyegeya, mkoani Morogoro, wakati Waziri huyo alipofika darajani hapo kujionea maendeleo yake. Muonekano wa mihimili mikuu itayowekwa katika daraja la Kiyegeya ikiwa imekamilika.  Muonekano wa moja ya nguzo zitakazoshikilia daraja la Kiyegeya ikiwa katika hatua za mwisho kukamilika.PICHA NA WUU Serikali imesema inatarajia kukamilisha ujenzi wa daraja la Kiyegeya, mkoani Morogoro, hivi karibuni, ambalo lilibomoka mwezi Machi, mwaka jana kutokana na mvua kubwa zilizokuwa zikinyesha. Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa daraja hi

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA IRINGA LIMEPITISHA UTARATIBU MPYA WA WA VITUO VYA KUPAKIA ABILIA NA NJIA ZA BAJAJI NA DALADALA

Image
  Mstahiki Meya wa manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada akisoma maazimio yaliyotewa na madiwani wa manispaa ya Iringa wakati wakijadili namna ya kutatua mgomo wa daladala na bajaji  Baadhi ya madiwani wakiwa kwenye baraza maalumu kwa ajili ya kutafuta njia ya kutatua mgomo wa daladala na bajaji Baadhi ya madiwani wakiwa kwenye baraza maalumu kwa ajili ya kutafuta njia ya kutatua mgomo wa daladala na bajaji Na Fredy Mgunda Iringa. Baraza la madiwani manispaa ya Iringa limepitisha utaratibu mpya wa wa vituo vya kupakia abilia na barabara zitakazo kuwa zinatumiwa na bajaji na daladala zote za manispaa ya Iringa kwa lengo la kutatua mgogoro uliokuwepo baina ya daladala na bajaji. Akitoa maazimio hayo mbele ya baraza maalum la madiwa lililofanyika tarehe 28 mwezi wa nne mstahiki meya wa manispaa ya Iringa Ibrahim Ngwada alisema   kuwa baraza limetafuta njia ya kutatua mgogoro huo kwa kuangalia namna bora ya njia na vituo ambavyo vitatumika. Alisema kuwa bajaji zote za zamani zinazotoka

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI APRILI 29, 2021

Image
 

KILIMO HAI NI AJIRA YA UHAKIKA KWA VIJANA

Image
Afisa Tathmini na Ufuatiliaji wa SAT Yohana Haule akiwa amemshika mkono Mtaribu wa Mradi wa Kilimo Hai wilaya ya Mlimba Elizabeth Msobi jana wakivuka mto kwenda kukagua mashamba ya vijana wakati wa ziara ya wataalam wa Wizara ya Kilimo kutembelea vikundi vya vijana kijiji cha Kalengakelu wilaya ya Mlimba. Afisa Tathmini na Ufuatiliaji wa SAT Yohana Haule akiwa amemshika mkono Mtaribu wa Mradi wa Kilimo Hai wilaya ya Mlimba Elizabeth Msobi jana wakivuka mto kwenda kukagua mashamba ya vijana wakati wa ziara ya wataalam wa Wizara ya Kilimo kutembelea vikundi vya vijana kijiji cha Kalengakelu wilaya ya Mlimba.(Picha na Wizara ya Kilimo) Mratibu wa Mkakati wa Vijana kushiriki kwenye kilimo toka Wizara ya Kilimo Revelian Ngaiza (kushoto aliyevaa tshirt blu) akiongea na Afisa Mtathmini wa shirika la SAT wakiwa kwenye shamba la mpunga lililolimwa na vijana kwa nia ya kilimo hai jana kijiji cha Kalengakelu wilaya ya Mlimba. SAT inatekeleza mkakati huo kwa kuwaunganisha vijana na kuwapa elimu ya

MJUMBE WA KAMATI KUU YA CCM, RAIS SAMIA AUNGANA NA WAJUMBE WENZAKE KWENYE KIKAO KINACHOFANYIKA DODOMA

Image
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi CCM, na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan na wajumbe wengine wakiwa tayari kuanza kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kinachoongozwa na Makamu Mwenyekiti wake (bara) Ndugu Philip Mangula akisaidiana na Makamu wa Mwenyekiti mwenza (Visiwani) Rais Mstaafu wa Zanzibar Ali Mohamed Shein katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma leo Jumatano Aprili 28, 2021.  

AWESO ATOA SIKU 10 MRADI WA MAJI MWAKITOLYO SHINYANGA UKAMILIKE

Image
Waziri wa Maji Jumaa Aweso, (katikati mwenye shati la bluu) akiwa kwenye ziara ya kukagua mradi wa Maji Mwakitolyo wilayani Shinyanga, wa tatu kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Jasinta Mboneko.

TBS YATOA ELIMU KWA WASINDIKAJI, WAJASIRIAMALI NA WADAU WA MCHELE KAHAMA

Image
  Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limetoa elimu kwa wasindikaji, wajasiriamali na wadau wa mchele wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga katika mnyororo wa thamani kuhusu kanuni bora za uzalishaji,matakwa ya viwango,namna bora ya uhifadhi,elimu juu ya vifungashio na taarifa za msingi zinazotakiwa kuwepo kwenye vifungashio. Mafunzo hayo yamefanyika leo Jumanne Aprili 27,2021 katika ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kahama na kukutanisha wajasiriamali 100 wanaojihusisha na bidhaa ya Mchele ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Anamringi Macha. Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Anamringi Macha aliishukuru TBS kwa kukutana na wasindikaji, wajasiriamali na wadau wa mchele akieleza kuwa ni kundi la wajasiriamali ambao ni sehemu muhimu katika sekta binafsi inayochangia pato la taifa,kuongeza ajira na kuondoa umaskini nchini.  “Wilaya ya Kahama ni moja ya wilaya za kimkakati katika uwekezaji mkubwa katika sekta y