Posts

WAZIRI MHAGAMA ATATUA KERO ZA WAFANYAKAZI KATIKA SHAMBA LA MKONGE LA KIGOMBE ESTATE

Image
Na  Mwandishi Wetu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama ametatua kero na changamoto zilizokuwa zikiwakabili wafanyakazi wa Shamba la Mkonge la Kigombe Estate, Wilayani Muheza dhidi ya mwajiri wao kufuatia malalamiko ambayo yaliwasilishwa wakati wa ziara ya Waziri Mkuu. Akizungumza wakati wa ziara yake hiyo ya kikazi ambayo ilikuwa imelenga utekelezaji wa Maagizo ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa aliyoyatoa tarehe 21 Januari, 2021 alipotembelea shamba hilo la Mkonge lililopo chini ya kampuni ya Amboni Plantation Limited. Mara baada ya kusikiliza pande zote mbili Waziri Mhagama alieleza kuwa kutokana na malalamiko mbalimbali yaliyowasilishwa na wafanyakazi inadhihirisha kuwepo na mapungufu makubwa katika utekelezaji wa sheria za kazi ambazo zimechangia kwa kiasi kikubwa migogoro kutokea. “Mwajiri anawajibu wa kusikiliza kero na malalamiko ya wafanyakazi wali

WAZIRI LUKUVI AAGIZA MAENEO YA MRADI WA KIMKAKATI KUPANGWA

Image
Na Munir Shemweta, MISUNGWI Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi ameitaka halmashauri ya wilaya ya Misungwi mkoa wa Mwanza kuhakikisha inapanga na kupima maeneo yanayopitiwa na miradi ya kimkakati ya treni ya Mwendokasi (SGR) na Kivuko cha Kigongo katika halmashauri hiyo mkoani Mwanza. Akizungumza wakati wa ziara yake ya kutembelea maeneo ya miradi ya upimaji katika maeneo ya miradi hiyo leo tarehe 1 Februari 2021 Lukuvi alisema, hakuna kuendeleza maeneo yanayopitiwa na miradi ya SGR na Kivuko cha Kigongo mpaka maeneo hayo yatakapopangwa mpango wa matumizi bora ya ardhi. " Maisha lazima yabadilike na msinyang'anye wananchi maeneo yao bali maeneo hayo yapangwe na kupangiwa matumizi yatakayoendana na hadhi ya miradi" alisema Lukuvi.  Alisema, halmashauri ni mamlaka ya upangaji hivyo Misungwi inapaswa kuzuia kuendelea kwa ujenzi katika maeneo hayo mpaka yapangwe kwa lengo la kupandisha hadhi na kuwa mji wa kisasa (modern city) ambapo alisisitiza kuwa

WAZIRI SIMBA HAWENE AWASWEKA RUPANGO VIONGOZI WA VIJIJI KWA KUSHAWISHI VURUGU WAFUGAJI, WAKULIMA KITETO

Image
 Na Mwandishi Wetu, MOHA, Kiteto_  WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene ameamuru kukamatwa na kuwekwa mahabusu viongozi wa vijiji vya Miriongima na Kijungu Wilayani Kiteto kwa kosa la kushawishi wananchi kufanya vurugu na kuvamia eneo lililotengwa na Serikali kwa shughuli za mifugo. Akizungumza katika mkutano wa hadhara na Wananchi wa Kitongoji cha Miriongima, Kijiji cha Kijungu, Wilaya ya Kiteto, Mkoani Manyara, leo, Waziri Simbachawene alisema viongozi hao wa vijiji ndio wanaochochea migogoro ambayo inaendelea kwasababu wanawadanganya wananchi na kupelekea kuvamia maeneo ambayo yametengwa kwa shughuli za mifugo kwa kufanya kilimo kinyume na utaratibu.  “Nimekuja kwasababu ya uvunjifu wa amani, nimekutana na viongozi wenu wa Wilaya na Mkoa, pia nimetembelea Kijiji cha Amei, na nyie hapa nimewasikiliza, kwa wale ambao mlienda kulima kule ardhi ya Kijiji cha Amei, mkiamini kwamba viongozi hawa wa Kijiji cha Kijungu ni wakweli, sasa muelewe kuanzia leo kwamba wamewadanga

KUTOKA MAGAZETINI LEO JUMANNE MACHI 2, 2021

Image
 

WAZIRI ASHIRIKI KUTOA MAWE MRADI WA UJENZI WA SHULE

Image
Wananchi wa Kijiji cha Bambi wakishiriki zoezi la kukusanya mawe  katika eneo la  Kijiji cha  Bambi Shehia ya Bambi Kijibwemtu, wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja ambapo ni eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ili kuwaondolea adha wanafunzi ya kutembea umbali mrefu wanafunzi wa Kijiji hicho kufuata elimu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Uzini, Khamis Hamza Chilo  akishiriki zoezi la kupasua mawe katika Kijiji cha  Bambi Shehia ya Bambi Kijibwemtu, wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja ambapo ni eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ili kuwaondolea adha wanafunzi ya kutembea umbali mrefu wanafunzi wa Kijiji hicho kufuata elimu. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Uzini, Khamis Hamza Chilo  akishiriki zoezi la kupasua mawe katika Kijiji cha  Bambi Shehia ya Bambi Kijibwemtu, wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguj

OTHMAN MASOUD OTHMAN ATEULIWA KUWA MAKAMO WA KWANZA WA RAIS WA ZANZIBAR

Image
Othman Masoud  

WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI NAO WAJIONEA KWA MACHO KASI YA UJENZI MRADI WA UMEME WA MAJI WA JNHPP 2115

Image
NA K-VIS BLOG, JNHPP RUFIJI WAHARIRI wa vyombo vya habari wametembelea mradi mkubwa wa kimkakati wa bwawa la kufua umeme wa maji la Julius Nyerere (JNHPP-2115) lililoko bonde la mto Rufiji na kujionea ujenzi ukiendelea kwa kasi katika maeneo yote muhimu matano. Wakiongozwa na Mhandisi wa Bwawa, Mhandisi Kamugenyi Luteganya Februari 28, 2021 wahariri hao walitembeela eneo la ujenzi wa bwawa (Main Dam),  eneo la kuchepusha maji (Diversion tunnel), eneo la power intake na eneo la kufua umeme (Power generation). Lakini pia waandishi hao walitembelea maeneo mengine ya ujenzi kama vile eneo la kuchukulia umeme (Switch Yard) na sehemu ya mitambo ya kuchanganya zege. Mapema akizungumza na wahariri hao katika kikao kazi baina ya TANESCO ambao ndio wasimamizi wa mradi kwa niaba ya serikali na wahariri mjini Morogoro Februari 27, 2021, Waziri wa Nishati Dk. Medard Kalemani aliwahakikishia kuwa ujenzi utakamilika kama ambavyo mkataba unavyosema Juni 2022. “Napenda niwahakikishie kuwa ujenzi eneo