WAHARIRI WA VYOMBO VYA HABARI NAO WAJIONEA KWA MACHO KASI YA UJENZI MRADI WA UMEME WA MAJI WA JNHPP 2115

NA K-VIS BLOG, JNHPP RUFIJI

WAHARIRI wa vyombo vya habari wametembelea mradi mkubwa wa kimkakati wa bwawa la kufua umeme wa maji la Julius Nyerere (JNHPP-2115) lililoko bonde la mto Rufiji na kujionea ujenzi ukiendelea kwa kasi katika maeneo yote muhimu matano.

Wakiongozwa na Mhandisi wa Bwawa, Mhandisi Kamugenyi Luteganya Februari 28, 2021 wahariri hao walitembeela eneo la ujenzi wa bwawa (Main Dam),  eneo la kuchepusha maji (Diversion tunnel), eneo la power intake na eneo la kufua umeme (Power generation).

Lakini pia waandishi hao walitembelea maeneo mengine ya ujenzi kama vile eneo la kuchukulia umeme (Switch Yard) na sehemu ya mitambo ya kuchanganya zege.

Mapema akizungumza na wahariri hao katika kikao kazi baina ya TANESCO ambao ndio wasimamizi wa mradi kwa niaba ya serikali na wahariri mjini Morogoro Februari 27, 2021, Waziri wa Nishati Dk. Medard Kalemani aliwahakikishia kuwa ujenzi utakamilika kama ambavyo mkataba unavyosema Juni 2022.

“Napenda niwahakikishie kuwa ujenzi eneo la mradi unaendelea usiku na mchana na kuongeza mradi huu ambao unafadhiliwa kwa asilimia 100 na Serikali kwa thamani ya Shilingi Trilioni 6.5 ni wa kwanza kwa ukubwa katika nchi za Afrika Mashariki na wanne kwa ukumbwa barani Afrika, utaleta manufaa makubwa siyo tu ya kuzalisha umeme Megawati 2115 bali pia utunzaji wa mazingira, kilimo cha umwagiliaji na ufugaji.

Mhandisi Kamugenyi Luteganya, akiwapatia maelezo wahariri hao.
Wahariri eneo la ujenzi wa bwawa kuu (main dam)
Mhandisi Kamugenyi Luteganya, akiwapatia maelezo wahariri hao.
Wahariri katika ziara hiyo
Mitambo ikiendelea kuchoronga miamba
eneo la bwawa kuu (main dam)

Wahariri eneo la bwawa kuu (main dam)
Wahariri eneo la bwawa kuu (main dam)
Wahariri eneo la bwawa kuu (main dam)
Meneja Uhusiano TANESCO 
Eneo la kuchepusha maji likiwa tayari
Wahariri ziarani JNHPP 2115
Wahariri ziarani JNHPP 2115
Wahariri ziarani JNHPP 2115
Matundu ya kupitishia maji kuingia kwenye mitambo ya kufua umeme. Kutakuwa na jumla ya mitambo tisa (Tibines) ya kufua umeme.
Mitambo ikichoronga miamba eneo la ujenzi
Bw. Ali Masoud maarufu Kipanya  mwandishi wa Clouds Media Group akiwa kazini
Wahariri wakitembelea eneo la mradi huku magari makubwa yakiwa kazini
Eneo la ujenzi wa sehemu ya kuchota umeme  unaotoka kwenye mashine z akufua umeme (tibines) (Switch yard) tayari umeanza
Picha ya pamoja ya wahariri

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"