Posts

KUTOKA MAGAZETINI LEO IJUMAA JANUARI 1, 2021

Image
 

RAIS MAGUFULI AWASILISHA FOMU YAKE TUME YA MAADILI YA VIONGOZI WA UMMA

Image
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 31 Desemba, 2020 amewasilisha fomu zake za maadili katika ofisi ya makao makuu ya Sekratarieti ya Maadili ya viongozi Jijini Dodoma. Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike (pichani chini). amekabidhi fomu hizo kwa Kamishna wa Maadili, Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesi. Leo ni siku ya mwisho ya kuwasilisha fomu za maadili kwa viongozi wote kwa mujibu wa Sheria namba 13 ya mwaka 1995 ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

ZIARA YA NAIBU WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU AKITEMBELEA MIRADI YA UZALISHAJIMALI YA WATU WENYE ULEMAVU JIJINI DAR ES SALAAM

Image
Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara wenye Ulemavu (UWAWADA) akieleza jambo kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga (wa pili kutoka kushoto) alipofanya ziara katika eneo la Machinga Complex ya kutembelea vikundi vya watu wenye ulemavu ambavyo vinajihusisha za shughuli za uzalishajimali. Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga (wa pili kutoka kushoto) akizungumza na Ndg. Galus Buriani (aliyekaa wenye ulemavu) wakati wa ziara yake ya kutembelea vikundi vya watu wenye ulemavu ambavyo vinajihusisha za shughuli za uzalishajimali na kuona namna walivyonufaika na mikopo inayotolewa na serikali kupitia halmashauri 10% (Wanawake 4%, Vijana 4% na Watu wenye Ulemavu 2%). Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Wenye Ulemavu) Mhe. Ummy Nderiananga (kulia)akimsikiliza Meneja Karakana ya Disabled Aid & General Engineering (DAGE), Ndg. Henry Chacha (katikati wenye ulemavu) wakati wa ziara yake ya kut

WAZIRI WA NISHATI ATINGA SHINYANGA, AONYA KATA KATA HOVYO YA UMEME

Image
  Waziri wa Nishati Dkr Medard Kalemani akizungumza na watumishi wa Shirika la umeme Tanzania TANESCO Mkoa wa Shinyanga. Na Marco Maduhu  -Shinyanga.  Waziri wa Nishati Dk. Medard Kalemani, amelionya Shirika la umeme Tanzania (TANESCO), kuacha tabia ya kukata kata umeme hovyo.

WANAVYUO JIAMININI ELEZENI VITENDO VYA UKATILI NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA UNAOTOKEA MAENEO YENU.

Image
Mkuu wa dawati la jinsia na watoto mkoa wa Arusha mrakibu msaidizi wa Polisi (ASP)  Happiness Temu  akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha ufundi Arusha kuhusiana na ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na uhalifu unaohusisha makosa ya mitandao katika kikao kilichofanyika katika bwalo la chuo hicho Jijini la Arusha. Mlezi wa wanafunzi Bi.  Stella Ngowa  (aliyekaa katikati), Rais wa serikali ya wanafunzi katika chuo cha ufundi Arusha (aliyevaa koti jeusi) Bwana  Issa Mohamed  wakifuatilia mada zilizokuwa zinatolewa katika kikao kilichojadili masuala ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na uhalifu unaohusisha makosa ya mitandao kilichofanyika katika bwalo la chuo hicho mapema leo Jijini Arusha. Mmoja wa mshiriki akichangia mada katika kikao kilichojadili masuala ya ukatili na unyanyasaji wa kijinsia na uhalifu unaohusisha makosa ya mitandao kilichofanyika katika bwalo la chuo cha ufundi Arusha  Jijini Arusha. Baadhi ya washiriki wakifuatilia kwa makini mada zilizokuwa zinatolewa katika kika

KUTOKA MAGAZETINI LEO ALHAMISI DESEMBA 31, 2020

Image
 

DKT. NDUGULILE AZIPA SIKU 30 TAASISI ZA UMMA ZINAZODAIWA NA TTCL KULIPA MADENI

Image
Na Prisca Ulomi, WMTH Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile amezipa siku 30 taasisi za umma zinazodaiwa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kulipa madeni kwa Shirika hilo ili liweze kujiendesha, kutekeleza majukumu yake ya kutoa huduma ya mawasiliano ya sauti na data kwa taasisi za Serikali, sekta binafsi na wananchi ili kukuza uchumi na kuchangia pato la taifa. Dkt. Ndugulile ameyasema hayo wakati wa ziara yake alipotembelea TTCL kwa lengo la kufahamiana na kuzungumza na wajumbe wa Bodi, Menejimenti na wafanyakazi wa TTCL, Dar es Salaam ambapo aliambatana na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhandisi Kundo A. Mathew na Mejimenti ya Wizara hiyo Ameongeza kuwa zaidi ya taasisi 20 za Serikali zinadaiwa na TTCL zaidi ya kiasi cha shilingi bilioni 30 ambapo zipo taasisi zinatumia huduma za mawasiliano za TTCL na zinakusanya mapato ya zaidi ya shilingi bilioni moja kwa mwezi ila hawako tayari kulipa huduma za TTCL Vile vile, ametoa onyo kali kwa kampuni zin