WANANCHI WAFURIKA BANDA LA JKCI, MAONESHO YA OSHA ARUSHA

 

NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID, ARUSHA

WANANCHI kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha, wamejitokeza kwa wingi kwenye banda la  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), ili kupata huduma za kitabibu kwenye Maonesho ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA) katika viwanja vya General Tyre, Njiro jijini Arusha.

Miongoni mwa huduma zitolewazo na wataalamu wa JKCI wakiongozwa na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, JKCI, Dkt. Dickson Minja ni uchunguzi wa magonjwa yote ya moyo na mishipa ya damu ikiwemo upimaji wa msukumo wa damu (blood pressure), upimaji wa sukari, Echo, Uzito, BMI na urefu.

Aidha wanaanchi wanaofika kwenye banda hilo pia wanapatiwa ushauri wa kitabibu kutoka kwa Daktari huyo Bingwa, Dkt. Dickson Minja.

Huduma zote hizo za uchunguzi zinatoelwa bure.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Dickson Minja (Wapili kushoto), akiwapokea wananchi waliofika kwenye banda hilo kupata matibabu (uchunguzi) wa afya ya moyo na mishipa ya damu, kwenye Maonesho ya Wiki ya bUsalama na Afya Mahali pa Kazi, viwanja vya General Tyre, Njiro jijini Arusha Aprili 27, 2024.
Wananchi wakiwa kwenye banda la JKCI, ili kupata huduma za kitabibu.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Dickson Minja akiwa na mwananchi aliyefika kwenye banda la JKCI ili kumfanyia uchunguzi wa moyo.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Dickson Minja akimfanyia uchunguzi wa moyo (kipimo cha Echo), mwananchi aliyefika banda la JKCI, Aprili 27, 2024.
Benson Bisare, Afisa Muuguzi JKCI, akimuhudumia mwananchi huyu kwa kumpima Blood Pressure (BP) kwenye banda la Taasisi hiyo kwenye viwanja vya General Tyre, Njiro, jijini Arusha, Aprili 27, 2024.

Benson Bisare, Afisa Muuguzi JKCI, akimuhudumia mwananchi huyu kwa kumpima Blood Pressure (BP) kwenye banda la Taasisi hiyo kwenye viwanja vya General Tyre, Njiro, jijini Arusha, Aprili 27, 2024.

Odilia Njau, Afisa Muuguzi JKCI, akimuhudumia mwananchi huyu wakati anapima urefu (Weight) na uzito (BMI).

Comments

Popular posts from this blog

CV YA KOCHA MPYA WA SIMBA PABLO FRANCO MARTIN "USIPIME"