DIB YATANGAZA NEEMA KWA WALIOKUWA WATEJA WA BENKI YA WANANCHI MERU (MERU COMMUNITY BANK)
ARUMERU
BODI
ya Bima ya Amana imetangaza kwamba wale wote waliokuwa wateja katika Benki ya
Wananchi Meru (Meru Community Bank) ambao hawajachukua amana zao zilizokuwa
chini ya Shilingi 1,500,000 wafike katika tawi la Benki ya Biashara Tanzania (TCB) tawi la Meru au Tawi la Benki
Kuu Arusha kwa ajili ya kurudishiwa amana zao.
Hayo
yalisemwa na Meneja Uendeshaji wa Bodi ya Bima ya Amana (DIB), Nkanwa Magina
wakati wa mfululizo wa mafunzo kuhusiana na uwepo wa DIB, Majukumu ya DIB na mfumo
wa DIB, mafunzo yakielekezwa kwa makundi mbalimbali wilayani Meru hususani kwa
viongozi wa Vijiji, na wafanyakazi wa taasisi mbalimbali za serikali,
Pia
makundi mengine ni pamoja na wafanyabiashara kwenye minada na masoko mbalimbali
ya wazi ambayo yapo katika vitongozji vya King’ori, Kikatiti, Maji ya Chai, Usa
River na Leganga.
Aidha
mafunzo hayo yaliendeshwa kwa takriban wiki nzima na kufikia tamati leo.
Akifungua
mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Arumeru Dkt. Amani Sanga, aliishuku
DIB kwa kuleta elimu hiyo katika muda muafaka.
“Wananchi
wengi waliopo katika wilaya ya Meru walikuwa wamekata tamaa ya kuhifadhi fedha
zao katika taasisi za fedha baada ya kuanguka kwa benki waliyokuwa
wanaitumainia na kuipenda ya Meru Community Bank. Mimi nikiwa mmoja wa wahanga
waliopoteza fedha zao baada ya kufungwa kwa benki yetu ya Meru, najisikia
fahari leo hii kusikia kwamba hatimae sasa ninaweza kwenda kupewa amana yangu
katika tawi la benki ya TCB.” Alisema.
Aliwaasa
wananchi wote kuziamini taasisi za fedha ambazo zina leseni ya Benki Kuu ya
Tanzania kwa sababu amana zao zinalindwa na Bodi ya Bima ya Amana.
Naye
kiongozi wa Kamati Teule ya Kusimamia Ufilisi upande wa Waliokuwa Wateja wa
Benki ya Wananchi Meru, Godwin Nderingo aliipongeza DIB kwa kufanya kazi yao
kwa waledi mkubwa ili kuwahakikishia wananchi wanapata haki zao.
“Ingawa
muda umekuwa mrefu sasa yapata miaka 6 tokea kufungwa kwa benki hii na zoezi la
ufilisi likiwa limefikia asilimia 70, ni ushauri wetu sisi tuliokuwa wateja
kuwaomba watu wote waliokuwa wanadaiwa na benki hii kurudisha fedha walizokopa ili
zoezi hili lifikie mwisho”.
Wakati wote wa mafuzno wananchi walifurahia zawadi mbalimbali zilizokuwa zikitolewa wakati wa mafunzo ikiwa ni pamoja na majibu ya maswali yao yaliyokuwa yakijibiwa kwa umahiri na wakufunzi wasaidizi, Joyce Shala na Sylvani Makole.
Meneja Uendeshaji wa Bodi ya Bima ya Amana (DIB), Nkanwa Magina, akiwasilisha mada.Mhasibu Mwandamizi wa DIB Silvani Makole akiwasilisha mada kuhusu Ufilisi wa Benki ya Wananchi Meru mbele ya wafanyakazi pamoja na viongozi wa vijiji wa Wilaya ya Arumeru.
Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Arumeru, Dkt. Amani Sanga akifungua mafunzo ya DIB kwa wafanyakazi na viongozi wa vijiji mbalimbali vya Halmashauri ya Meru.
Meneja Uendeshaji wa Bodi ya Bima ya Amana (DIB), Nkanwa Magina, akiwasilisha mada.
Wafanyakazi wa Halmashauri na Viongoxi wa vijiji wakifuatilia mada.
Mwenyekiti wa Kamati ya kuongoza waliokuwa na amana katika Benki ya Wananchi Meru, Godwin Nderingo, akitoa neno la shukuran baada ya mafunzo.
Afisa Rasilimali Watu Mwandamizi wa DIB, Joyce Shala akimuelimisha mfanyabiashara na mteja wa zamani wa benki ya Meru katika soko la Leganga - Usa river.
Wakufunzi wa DIB wakiwa wamejipanga kwa ajili ya kutoa elimu kwa Wakulima wa kijiji cha King’ori
DIB walitoa elimu kwa umma kwa kupitia redio maarufu ya Safina FM Arusha, pichani Meneja Uendeshaji Nkanwa Magina (kushoto) na Mhasibu Mwandamizi Silvani Makole wakitoa mada.
Elimu sokoni Tengeru ikiendelea
Comments
Post a Comment