RAIS DK.MWINYI AKUTANA NA UONGOZI WA KANISA LA KILUTHERI AFRIKA MASHARIKI.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi amekutana na Makamu Askofu Mkuu wa Kanisa
la Kilutheri Afrika Mashariki (KKAM), Askofu Dk.Philemon Mollel na ujumbe wake
waliofika Ikulu Zanzibar kujitambulisha Ikulu Zanzibar tarehe: 28 Februari
2024.
Aidha, Rais Dk.Mwinyi amesema Serikali inatambua
mchango unaotolewa na Madhehebu ya Dini zote ikiwemo kuhubiri amani na
utulivu katika kuleta umoja nchini.
Kwa upande mwingine Rais Dk.Mwinyi amelipongeza
Kanisa hilo kwa utayari wao wa kushirikiana na Serikali katika kutoa huduma za
kijamii nchini ikiwemo afya na elimu.
Naye Askofu Mollel amempongeza Rais Dk.Mwinyi kwa
kuleta mabadiliko ya maendeleo na kuwaunganisha wananchi bila kujali itikadi za
chama, kabila na Dini.
Comments
Post a Comment